Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 378
- 766
Seif Kisauji 'Babu wa TikTok'
Waziri Ndumbaro ametoa uamuzi huo leo Jijini Dodoma baada ya kusikiliza rufaa ya msanii huyo ya kupinga adhabu aliyopewa na Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ya kufungiwa kujihusisha na shughuli za sanaa kwa miezi sita pamoja na kulipa faini ya TZS milioni 3 kutokana na kurusha mtandaoni picha za video zinazokiuka maadili.
Aidha, kufuatia rufaa hiyo, msanii Seif Kisauji amekiri kosa la kusambaza maudhui hayo na kuomba apunguziwe adhabu, hatua iliyomfanya Waziri Dkt. Ndumbaro amuondolee adhabu ya kifungo cha cha miezi 6 cha kutojihusisha na shughuli za sanaa huku akimuongezea kiwango cha faini kutoka milioni 3 hadi 5.
PIA SOMA
- Kisauji (babu wa TikTok) afungiwa miezi sita