Dkt. Philip Mpango maneno uliyotamka siku unaapishwa yalitoka ndani ya moyo wako? Ulikuwa unawakebehi Watanzania?

Dkt. Philip Mpango maneno uliyotamka siku unaapishwa yalitoka ndani ya moyo wako? Ulikuwa unawakebehi Watanzania?

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Wahenga wanasema tembea uone. Ndio maana hata mzee Mwinamila alipokuwa hai aliwahi kutunga wimbo akimwambia Mwl Julius Nyerere atembee aone ili ajionee kwa macho yake nchi anayoitawala na watu wake wanaishi kwa namna gani.

Nimepafanya kijiziara kidogo suo moto, maana sijapangiwa na mtu. Ila nimeshuhudia kuwa watanzania bado wana hali mbaya sana kiuchumi. Watanzania wanaishi maisha duni, kula ni kwa tabu,kulala kwa tabu kwa kweli inasikitisha sana.

Ukweli ni kwamba watanzania sio wavivu, wanapenda kazi, maana nimeshuhudia kwa macho yangu, wanalima, wanachimba madini tena kwa mikono, wanafanya biashara. Kwa ujumla wanajituma japokuwa wapo baadhi ni wavivu na matapeli.

Lakini huu umaskini unatoka wapi? Fikiria mama ana mtoto mgongoni anajishughulisha kuosha vyombo kwa mama ntilie na analipwa shilingi elfu mbili, kwa jinsi pesa isivyo na thamani ataishi vipi?

Dkt. Mpango siku unaapishwa ulikiri kwa kinywa chako, ulipokuwa unafanya kampeni umeshuhudia umaskini mkubwa sana wa wananchi wa jimbo lako. Na ukweli ni kuwa hali uliyoishuhudia ndio hali halisi ya watanzania 75%.

Dkt. Mpango kama mchumi, unatusaidia vipi sisi watanzania kuepukana na hii hali? Je, huwa unamueleza ukweli mkuu wa nchi juu ya hii hali uliyoishuhudia? Una mpango gani wa kuleta sera nzuri za kiuchumi kuwaokoa hawa watanzania wanaoteseka?

Au uliongea kama unajikosha tu mbele ya umma,maana hatuoni ukichukua hatua ili kutunusuru.
 
Mpango atakuja na njia gani kutatua ya umasikini uliopo, wakati yeye mwenyewe hawezi kuendesha maisha yake nje ya ajira?
We jamaa una matatizo? Mtu mwenye PHD ya uchumi hawezi kujiaajiri?
 
Ahaaa, hii karii,kwani kabla ya kuwa waziri alikuwa wapi?

Alikuwa ameajiriwa Tanroads. Nitajie mahali alipowahi kujiajiri na mafanikio yake kabla ya kukabidhi maisha yake kwenye ajira. Waziri wa fedha ambaye anajua mambo ya fedha na ana PhD, asingekubali wafanya biashara wa Bureau de change kuporwa fedha zao.
 
Wahenga wanasema tembea uone. Ndio maana hata mzee Mwinamila alipokuwa hai aliwahi kutunga wimbo akimwambia Mwl Julius Nyerere atembee aone ili ajionee kwa macho yake nchi anayoitawala na watu wake wanaishi kwa namna gani.

Nimepafanya kijiziara kidogo suo moto, maana sijapangiwa na mtu. Ila nimeshuhudia kuwa watanzania bado wana hali mbaya sana kiuchumi. Watanzania wanaishi maisha duni, kula ni kwa tabu,kulala kwa tabu kwa kweli inasikitisha sana.

Ukweli ni kwamba watanzania sio wavivu, wanapenda kazi, maana nimeshuhudia kwa macho yangu, wanalima, wanachimba madini tena kwa mikono, wanafanya biashara. Kwa ujumla wanajituma japokuwa wapo baadhi ni wavivu na matapeli.

Lakini huu umaskini unatoka wapi? Fikiria mama ana mtoto mgongoni anajishughulisha kuosha vyombo kwa mama ntilie na analipwa shilingi elfu mbili, kwa jinsi pesa isivyo na thamani ataishi vipi?

Dk. Mpango siku unaapishwa ulikiri kwa kinywa chako, ulipokuwa unafanya kampeni umeshuhudia umaskini mkubwa sana wa wananchi wa jimbo lako. Na ukweli ni kuwa hali uliyoishuhudia ndio hali halisi ya watanzania 75%.

Dk. Mpango kama mchumi, unatusaidia vipi sisi watanzania kuepukana na hii hali? Je, huwa unamueleza ukweli mkuu wa nchi juu ya hii hali uliyoishuhudia? Una mpango gani wa kuleta sera nzuri za kiuchumi kuwaokoa hawa watanzania wanaoteseka?

Au uliongea kama unajikosha tu mbele ya umma,maana hatuoni ukichukua hatua ili kutunusuru.
Hivi inakuwaje waimba mapambio wakuu leo mnakuja na hoja mlizo hubiri kwenye mapambio yenu miaka na miaka au baada ya kufanikisha malengo yenu mnatuletea kejeli?Naomba majibu
 
Hivi inakuwaje waimba mapambio wakuu leo mnakuja na hoja mlizo hubiri kwenye mapambio yenu miaka na miaka au baada ya kufanikisha malengo yenu mnatuletea kejeli?Naomba majibu
Mapambio gani? Au fikra zako fupi zinakufanya ushindwe kufahamu kuwa kueleza uhalisia wa mambo ni jambo jema kwa mustakabari wa taifa la Tanzania na watanzania.
 
Mapambio gani? Au fikra zako fupi zinakufanya ushindwe kufahamu kuwa kueleza uhalisia wa mambo ni jambo jema kwa mustakabari wa taifa la Tanzania na watanzania.
Huna uhalisia,hujawahi kuwa nao na utausikilizia tu mtaa was kijani na hauta upata kamwe.
 
Alikuwa ameajiriwa Tanroads. Nitajie mahali alipowahi kujiajiri na mafanikio yake kabla ya kukabidhi maisha yake kwenye ajira. Waziri wa fedha ambaye anajua mambo ya fedha na ana PhD, asingekubali wafanya biashara wa Bureau de change kuporwa fedha zao.
Usikurupuke mithiri ya mtu anatapika au anahara, hana historia ya kuwa Tanroads zaidi ya kuwa mchumi mbonezi, ofisi ya rais na world bank.
 
Back
Top Bottom