- Thread starter
- #161
Zaidi ya sanaAwe makini
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Zaidi ya sanaAwe makini
They want to kill him scientifically while kissing him, a purpose is to silence other messengers.Yaaani uhuru wote huu wa kutoa maoni bado kuna watu wanatengeneza hadithi? Katoa maoni Jaji Warioba, Profesa Shivji, Profesa Lipumba, BAKWATA, TEC na Mbowe ambaye alitumia maneno baadhi ya kuudhi hakuna alietishwa iweje kwa wakili flan mmoja tu? TLS imezungumza hawakutishwa. Hebu tuache kutaka kuichafua nchi. Uhuru wa maoni ni mkubwa mno. Muhimu tuutumie kwa maendeleo na nidhamu.🙏🙏🙏
Wewe unayo mkuu?Utafanya nini? msitafute kick mijini nani anashida na mtu hana impact yoyote. Eti vyanzo kuna watu watafuta kick tu ndio kwanza namjuwa leo.
Dah💔💔💔Taarifa kwa nani? angemwambia mkewe sisi anatuhusu nini.
Huyo wakili anatumia ngao ya kuaminisha watu hivyohahahh
Na wewe ni Mtanzania?!Huyu amevurugwa tu. Sifa moja juu ya msomi ni kudhibiti hasira zako. Kama vipi aende kwao Burundi
Hivi mama samia alikuwa na akili timamu wakati anasaini hii laana(mkataba)?alishikiwa bunduki?nini kiko nyuma ya huu mkataba ambapo SSH haoni mapungufu makubwa?ninapata ukakasi mama samia na Magufuli walikuwa ni hasi na chanya Kwa maslahi ya Tanzania.kama kweli haoni tatizo kwenye hii tuhuma..basi yahitajika kujitafakari.Daah, hatari, ila..
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa
1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)
2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?
3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?
4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!
6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
Tanganyika wazanzibar wanachukua Mali yetu kisa Cha muwekezaji jamani.
WHY WHY BANDARI ZA ZANZIBAR No. KUWA FAIDA WACHUKUE WAO TU YOTE HATA TANGANYIKA ISIPATE FAIDA YA 0TZS. HUKU MASIKINI WAKIUMIZWA NA KODI YA MIAMALA NA KILA SEHEMU IMEJAA KODI WHY HUYO ASEMEHEWE KODI HAMUONI KUWA HAO JAMAA WANAJILIPA KWENYE BANDARI KAMA WENGINE WALIVYOKWISHAJILIPA KWENYE UMEME, GESI NA MAFUTA WAO TU NDIO MADILA BASI PAMOJA NA SUKARI.
WATU MMELALA SIJUI MTAJUJA KUWAAMBIAJE WAJUKUU ZENU WATAKAPOKUWA HAWANA PA KWENDA NA KUTUMIKISHWA KAMA PUNDA NA HUKU WEWE UMESHIBA LEO PEKEE.
JAMANI ACHENI UOGA KIZAZI CHA AKINA NYERERE WALITESEKA SIE TUWE HURU WHY SIE TUNAKUWA WAOGA NA ASKARI ANAGANYA KAZI KAMA ROBOTI ANAUA MTU ANAYETETEA TAIFA KISA CHA AJIRA YAKE AMBAYO KWANZA INAMFANYA AWE MASIKINI.
ANGALIENI NCHI YETU IMESHAUZWA IMEISHA PORI TENGEFU, MADINI YAMEISHA YOTE WANAWAPA WATU KWA GAWIO LA SIRI KIVYAO NA SIO LA SERIKALI.
BAADAYE UNAKAMULIWA KODI MPAKA VIMA YAISHE.
YAANI HUJIULIZI UNALIPWA SALARY KODI, UKITOA HELA BANK KODI, UKIITUMA KODI, UKIITOA ULIYOTUMIWA KODI, UKINUNUA KITU KODI , YAANI KUNA KODI NYINGI MNO UNALIWA MPAKA UNAKUJA KUIPATA HELA YAKO.
HUKU WATU WAKIWAPA MA EX WAO GARI ZA 500M.
ASKARI usifanye kazi Kama roboti kuwa Ni amri unaumiza wananchi wanaotetea maisha mpaka ya mjukuu wako. Usiwaze tumbo lako Leo tu.
Unataka wazanzibar WACHUKUE bandari yetu mbona wao za kwao hazimo.
Yaani wasamehewe Kodi asilimia kweli afande wewe unayetumwa jamani na huku sie kila kona Kodi na maisha ya wananchi hawapati huduma za muhimu. Haya tuueni Mana nyie mtaishi milele.Ivi kweli kuwa jamaa wasemehewe Kodi ili iweje na kwa faida ya Nani na bandari inachukuliwa Kama shamba la mtu milele ,
Ila kweli kuwa mwanasiasa hata jambazi anao uafadhali
Mtaua wangapiHuyo wakili anatumia ngao ya kuaminisha watu hivyo
Kwa nn asiwataje hao watu waliomtishia?
Anatengeneza uungwaji wa kiki
Flan flan
Ninaimani mama Samia anaufuatilia huu uziNimemsikia sana huyu Wakili Msomi. Naamini kama Rais Samia atasikiliza hii link ya youtube atabadili mawazo yake kuhusu mkataba wa DP WORLD!! Itakuwa ni ni NUKSI kubwa kwake kama raia wa Tanzania atapoteza maisha sababu ya kutetea raslimali za nchi.
Labda kuwe na nguvu nyingine nyuma yake ambayo ni sadist. Naamini hata hao wanaowatisha hawa mawakili wasomi kuwatoa uhai hawajatumwa na Rais Samia bali na makundi masilahi yanayomzunguka Samia.
Samia amka jitoe kwenye hayo makundi ya akina Rostam na JK, wanakutumia tu ili kufanikisha masilahi yako. Usikubali kumwaga damu ya Mtanzania yeyote kama alivyofanya Magufuli!! Ukikaidi na wewe pia hutadumu kwenye kiti hicho kama mtangulizi wako alivyofanya
Hususani wengi wetu sisi watanganyika.sijui nani katuharibu ufahamu na kutupofusha macho jamani🥹🥹🥹🥹🥹Kuna swali huwa najiulize sana I wish ningepata majibu, kwanini watu weusi huwa hatujipendi? Hatuangalii vizazi vyetu vijavyo? tunaishi kama sisi ndio watu wa mwisho kuwepo?
Hii ndiyo legacy ya Magufuli. Huyo Mwamakula anajipendekeza kwa rais. Kwani rais hawezi kuua iwapo alishafanya hivyo kwa wengi waliopotea akiwa makamu wa rais?Habari wasomaji na wananchi wote.
Je, tumekuwa Taifa la ovyo hivi.
Je, hili ni suluhisho la mjadala katika mambo ya Kitaifa?
Akiuawa, tunatuna ujumbe gani.
Pia soma
-
- Mwanasheria Dkt. Nshala Rugemeleza: Mkataba wa bandari ni wa kiuhaini, Umevunja katiba ya nchi na utakwenda kuvunja sheria za nchi
- Rugemeleza Nshalla: Tutafungua Kesi kupinga Mkataba wa DP World na Tanzania
Kwa mujibu wa ibara ya 14 ya katiba ya nchi yetu kila mtu ana haki ya kuishi na kwamba anapaswa kupata hifadhi ya maisha yake kutoka kwenye jamii hiyo.
Maneno yaliyosemwa dhidi yake na watu wengine waliojiita masheikh yalikuwa yanasikitisha kwa mtu ambaye anamfahamu Profesa Issa Shivji kwa uzalendo wake na utumishi wake uliotukuka na kujitoa kwake kwa nchi yetu, wale watu walikuwa wanaongea kana kwamba ni maneno yao bali kulikuwa na watu ambao walikuwa nyuma yao.
Damu yangu kama itamwagika basi ikapalilie mapambano ya kulinda rasilimali za nchi yangu Tanzania.
Mtu hawezi kuishi katika nchi ambayo ni Jamhuri na watu wengine wakawa na leseni ya kuondoa uhai wao. Mwenye leseni, ruhusa na mamlaka pekee ya kuondoa uhai wa mtu hapa duniani ni Mwenyezi Mungu pekee.
Kiukweli kuua watu kupo na watu wamefariki, watu wamejeruhiwa na kupata matatizo makubwa. Kufuatia hilo nimeamua kuja mbele ya umma wa Watanzania kuwaambia kwamba mimi Rugemeleza Nshala maisha yangu yako hatarini. Kuna maagizo kutoka ndani kwamba nitakapopatikana niteketezwe, niangamizwe na kuitwa marehemu.
Mkataba huu wa bandari umesainiwa au umepewa kibali kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kibali hiko kinaonekana katika kiambatanisho kimojawapo katika mkataba huo ambacho kina saini ya Rais Dkt. Samia
===
Wakili wa kujitegemea Dkt.Rugemeleza Nshala amesema amepokea taarifa kutoka vyanzo vya kuaminika ndani ya mifumo kuwa anatakiwa kuuwawa kwa kile alichokieleza kuwa ni kutokana na msimamo wake dhidi ya watu waliojitokeza kumshambulia kwa maneno ya kejeli na kuudhi Prof.Issa Shivji baada ya msomi huyo wa sheria kutoa maoni yake dhidi ya sakata la uwekezaji wa Bandari linaloendelea sasa hapa nchini
Akizungumza na Wanahabari kwenye ukumbi wa Mesuma Hotel, Makumbusho Jijini Dar es Salaam, Dkt.Nshala ambaye pia amewahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) ameeleza kuwa hivi karibuni kupitia jukwaa la 'club house' alitoa maneno makali ambayo kiuhalisia amedai kuwa ndio msimamo wake dhidi ya watu hao ambao anaamini kuwa walichokizungumza si maneno yao bali wanatumiwa na watu wenye mamlaka nchini kutoa lugha za kashfa na kuudhi dhidi ya mtu mwenye umri mkubwa na anayestahiki heshma kubwa dhidi yao kwenye jamii
Dkt.Nshala aliyefika kwenye Kikao hicho akiwa amebeba Vitabu viwili alivyoeleza kuwa anavyoviamini zaidi (Biblia na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) amesema anawaeleza wenye mamlaka walio nyuma ya mpango huo kuwa yuko tayari kufa kwaajili ya nchi yake
Ikumbukwe kuwa kupitia jukwaa hilo ambalo lilijadili mjadala wa kina kuhusiana na uwekezaji wa Kampuni ya DP World ya Dubai kwenye Bandari, Dkt.Nshala alitoa kauli zolizoonekana kuwashambulia zaidi viongozi waandamizi serikalini akiwemo Rais Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof.Makame Mbarawa nk
---
Ndugu Watanzania!
Dkt. Rugemeleza Nshala ametujulisha kuwa maisha yake yako hatarini. Wakili Dkt. Nshala anasema kuwa ametaarifiwa juu ya mipango ya kutaka kumuua (assassination) inayopangwa dhidi yake! Vitisho dhidi ya maisha ya Wakili Dkt. Nshala vinakuja muda mfupi tu baada ya yeye kutoa maoni yake kwa hisia kali akipinga Mkataba wa Bandari kati Serikali ya Tanzania na Ufalme wa Dubai.
Dkt. Rugemeleza Nshala, ambaye alikuwa Rais wa Tanganyika Law Society (TLS) ni wakili na mwanasheria mbobevu anayejua vema mipaka yake kikatiba na kwa nafasi yake anao wajibu wa kutoa ushauri na maoni kwa Watanzania katika masuala ya sheria na katiba ya nchi.
Sisi Askofu tumepata muda wa kuomba na Dkt. Nshala na kumtia moyo kuwa asiogope kwani alitoa maoni yake kama raia anayeipenda nchi yake na hakuvunja sheria ye yote ya nchi. Kwa maoni yetu, watu wanaomtisha Dkt. Nshala au wanaotaka kuondoa uhai wake ni watu waoga ambao wanataka kumchafua Rais Dkt. Samia ili dunia ifikiri ameanza kuwaua wakosoaji wake.
Kwa hiyo, sisi Askofu Mwamakula tunatoa wito kwa watu, kikundi, vikundi hata taasisi ambao wanapanga kutoa uhai wa Dkt. Nshala pamoja na wanaharakati wengine wanaotoa maoni yao au hata kuikosoa Serikali kuhusiana na suala la Mkataba wa Bandari waache mara moja. Kama wao wanafikiri kuwa Dkt. Nshala na wenzake wamefanya kosa lo lote kisheria, wawapeleke mahakamani badala ya kuanza kuwatisha.
Kutisha watu na kutaka kuwaondoa au kuwaua watu nje ya mfumo wa kisheria ni uhaini, uuaji, unyama na ujambazi bila kujali mtu anayefanya matendo hayo. Sisi Askofu tunatoa tahadhari hii kama kukinga mapema ili watu hao wajue kuwa wanachokipanga kufanya hakikubariki. Kama Dkt. Nshala na wenzake watadhulika kwa lolote, watu waliowahi kutoa kauli zao kwa lengo la kuwatisha, hao watawajibika. Kukinga ni bora kuliko kutibu! Tumetimiza wajibu wetu!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Dar es Salaam, 6 Julai 2023; 09:39 am.
View attachment 2680028
Mimi sina hata nikiita press watajiuliza huyu naye ni nani. Impact ninayo kwa family yangu tu lakini kuna wengine hata kwenye family zao wanaondoka kama hajaondoka mtu.Wewe unayo mkuu?
Dp wameingia mkataba wa miaka mingapi na Tanzania?naomba jibu mkuuAcheni kauli za kibaguzi!
DP World ni wawekezaji. Kuwaita waarabu ni kauli za ubaguzi.
Acheni pia upotoshaji. Hakuna bandari iliyouzwa,itakayouzwa wala ardhi aliyopewa muwekezaji.