Dkt. Samizi achangia Bungeni, aiomba Serikali kutatua kero Jimbo la Muhambwe

Dkt. Samizi achangia Bungeni, aiomba Serikali kutatua kero Jimbo la Muhambwe

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2019
Posts
377
Reaction score
435
Mbunge wa Jimbo la Muhambwe mkoani Kigoma Mhe. Dkt. Florence George Samizi leo amechangia Bajeti ya Wizara ya TAMISEMI Bungeni Jijini Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine ametoa hoja mbalimbali kwa ajili ya kutatua kero na kusukuma maendeleo Jimboni kwake.

Kwanza; Dkt. Samia amempongeza Rais Samia kwa kupeleka fedha nyingi za miradi ya maendeleo ambapo Jimbo la Muhambwe katika mwaka huu wa fedha limepata Bilioni 18 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Pili; ameieleza Serikali changamoto ya ajira na uhaba wa watumishi katika sekta ya elimu na afya Jimboni kwake akiomba Serikali itatue changamoto hii kwa haraka ili wananchi wapate huduma bora zaidi.

Tatu; ameeleza changamoto ya uhaba wa watumishi kwa walimu wa shule za msingi na sekondari akiomba walimu kuongezwa.

Nne; ameomba shule za kidato cha 5 na 6 kuongezeka kutoka 3 zilizopo sasa hadi 5 lakini hata zile 3 zilizopo Serikali iongeze madarasa maana bado kuna changamoto kubwa ya madarasa. Pia amemuomba Waziri afike Kumkugwa sekondari ya kidato cha 5 na 6 ambayo ilikuwa kambi ya wakimbizi ajionee uchakavu na uhaba wa miundo mbinu ya madarasa

Tano; aomba Serikali kupitia TARURA kujenga barabara ili kuunganisha barabara za Jimbo ili kuharakisha shughuli za wananchi.

Sita; mahitaji ya madaraja ya mawe yaongezeke haraka kutatua kero hii Jimboni.

Saba; kumalizia maboma ya zahanati na kumalizia madarasa.

Nane; mwisho, Dkt. Samizi amemalizia kwa kuitaka Wizara ya TAMISEMI kutekeleza ahadi za Viongozi wa Juu wa Nchi walizotoa Jimboni ikiwemo kumalizia maboma ya vituo vya afya, zahanati na madarasa kama boma la kituo cha afya Kizazi.

 
Mbunge wa Jimbo la Muhambwe mkoani Kigoma Mhe. Dkt. Florence George Samizi leo amechangia Bajeti ya Wizara ya TAMISEMI Bungeni Jijini Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine ametoa hoja mbalimbali kwa ajili ya kutatua kero na kusukuma maendeleo Jimboni kwake.

Kwanza; Dkt. Samia amempongeza Rais Samia kwa kupeleka fedha nyingi za miradi ya maendeleo ambapo Jimbo la Muhambwe katika mwaka huu wa fedha limepata Bilioni 18 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Pili; ameieleza Serikali changamoto ya ajira na uhaba wa watumishi katika sekta ya elimu na afya Jimboni kwake akiomba Serikali itatue changamoto hii kwa haraka ili wananchi wapate huduma bora zaidi.

Tatu; ameeleza changamoto ya uhaba wa watumishi kwa walimu wa shule za msingi na sekondari akiomba walimu kuongezwa.

Nne; ameomba shule za kidato cha 5 na 6 kuongezeka kutoka 3 zilizopo sasa hadi 5 lakini hata zile 3 zilizopo Serikali iongeze madarasa maana bado kuna changamoto kubwa ya madarasa. Pia amemuomba Waziri afike Kumkugwa sekondari ya kidato cha 5 na 6 ambayo ilikuwa kambi ya wakimbizi ajionee uchakavu na uhaba wa miundo mbinu ya madarasa

Tano; aomba Serikali kupitia TARURA kujenga barabara ili kuunganisha barabara za Jimbo ili kuharakisha shughuli za wananchi.

Sita; mahitaji ya madaraja ya mawe yaongezeke haraka kutatua kero hii Jimboni.

Saba; kumalizia maboma ya zahanati na kumalizia madarasa.

Nane; mwisho, Dkt. Samizi amemalizia kwa kuitaka Wizara ya TAMISEMI kutekeleza ahadi za Viongozi wa Juu wa Nchi walizotoa Jimboni ikiwemo kumalizia maboma ya vituo vya afya, zahanati na madarasa kama boma la kituo cha afya Kizazi.

View attachment 2592299
Ni kweli tatizo la watumishi lipo kila sehemu ila kigoma na wilaya zake watu huogopa uchawi tu

USSR

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Muhambwe tena...😳
Basi hii nchi bado haijaisha kabisa...
 
Muhambwe tena...[emoji15]
Basi hii nchi bado haijaisha kabisa...

Wilaya ya kibondo ilikua na majimbo mawili yaani muhambwe na buyungu, sasa baada ya kibondo kubaki wilaya pale ikaitwa muhambwe na kakonko ilivokua wilaya ikabaki na jimbo la buyungu, watu wa kule wahambwe ni wenyeji wa kibondo na wayungu ni wenyeji wa kakonko, wenzao kasulu walibaki na kasulu mjini na kasulu vijijini na nadhani mkoa wa kigoma una majimbo 10 au 9 ya uchaguzi kama sijasahau
 
Ila hawa wabunge wa CCM hata siwaelewi wanavyochangia.
Hivi mtu unawezaje kuanza kupongeza Kwa utendaji mzuri wa kazi za serikali ( Rais ) halafu ukashukuru Kwa kuletewa fedha nyingi.
Baada ya hapo anaanza malalamiko hakuna hiki, hakuna kile na matakataka na mapungufu mengine kibao.
Halafu anamalizia na kuunga mkono hoja.
Kwa Mimi niliyesoma philosophy hususani (Logic, Argumentation & Reasoning ) siwaelewi kabisa hawa watu.
Nyie wabunge wa CCM tambueni mnachoongea huko bungeni asilimia kubwa ni fallacies na invalid inference.
Embu acheni hayo mambo , mnatumia vibaya kodi zetu
 
Back
Top Bottom