Dkt. Slaa Afuatiliwa na watu wasiojulikana kutoka Iringa hadi Dar Es Salaam

Mama zitto amelalamika kuvamiwa na kutishiwa kifo ameonekana mwehu, leo wewe kufuatana na watu barabarani unajifanya umefatiliwa...nani apoteze muda na mafuta kuhangaika na ww...ilikuwa mrema bana enzo zake sio nyie, na hajatishiwa
 

Hyo Nimeipenda Mkuu. Mi napitiaga tu na kuelewa. Jamaa anajitia hajaelewa wakt ameelewa. Istoshe ameelewa then aka comment!
 


mama salma naona leo umechachamaa
 
Je, kuna mke wa mtu yeyote mliyempa lift?

Hata Mahimbo enzi zile angekuwa anafuatilia nyendo za mke wake Josephine wangesingiziwa TISS...
 
CCM wameshindwa kuendesha siasa za majukwaani badala yake wameamua kutumia Ulimboka Style

Wanafanya yote haya wakiwa chama tawala, je wakijikuta kwenye upinzani si ndio itakuwa balaa zaidi? nafuu pekee itapatikana ikiwa CCM itasambaratika pale ikishindwa uchaguzi,
 
Well said mazee,

Naona huu mchezo wao umeosoma vizuri.

Wameona juzi kuna shutuma za mama Zitto wamerudi na hii kutupoteza malengo.
Umeona eenh, hakuna hata mdomo ulionyanyuliwa kuongelea lile suala la mama zitto, wanachosubiri, likiripuka la chadema, basi wanatafuta skendo ya kuhamisha mawazo ya wananchi......na huyu zitto anaujua ukweli wa CDM, nadhani hadi siku wamguse patakapomuuma ndiyo atatoka na kueleza madudu ya cdm, and trust me, hata zitto akieleza hayo..bado wale vijana wasioona mbele wala nyuma watamtukana....tumeshashuhudia hilo, tena si mara moja wala mara mbili...kipind kile zitto haelewani na uongozi wa CDM, walikuwa na migogoro ya ndani..unakumbuka?? Mwanahalisi, Tanzania Daima na Jamii forums ndiyo zilikuwa zinaongoza kuanika mabaya ya zitto, mwanahalisi walienda mbali hadi kuanika mazungumzo kwa njia ya simu kati ya zitto na January makamba enzi zile yupo ikulu...so to make the story short...these CDM guys are loosing it....they are like a group of people in very deep water struggling to survive.....
 
Tatizo ni TISS mnapojiingiza kwenye siasa za vyama.Fanyeni kazi kwa uadilifu na hamtapa wasiwasi kama ccm ikiondolewa madarakani.
niamini ndugu, wakati wa kufa, mtu atatafuta wakumlaumu kwa nguvu zote, mnahitaji ushahidi gani muamini kuwa CDM wana uchu wa madaraka, and for that wako tayari kufanya lolote, kujeruhi yoyote, kuua yoyote kuhakikisha wanakamata madaraka, hivi ni akili mgando kiasi gani kufikiria kumpa lema jambazi mstaafu wizara ya mambo ya ndani?? na nyi vijana wa nchi hii, mnaojiita wasomi mpo tu?? afu kila siku, TISS, Polisi, Jeshi wote ni magamba?? hamjui vyombo vyote hivyo moja ya kazi zake ni kuilinda serikali iliyoingia madarakani kihalali bila ya kujali inatoka chama gani?? mmepewa akili mzitumie, sio mfanye mapambo...
 
UKIWA DEREVA WA GARI BOVU, HATA UKIWA UNATEMBEA KWA MGUU, UKIONA TRAFFIC POLICE LAZIMA UJIFICHE.........huu ni ujumbe kwa dr slaa, wengine hauwahusu....yeye amenielewa
 
Slaa anatakiwa akue sasa
Mmeanikwa mchana kweupe
Hapa dr haponi kuna ma GT wanao fikiria na kuanalyse issues critically sanasana ataungwa mkono wale Brainwashed only. Au ban kutupunguza ndio zitawasaidia.
Great thinkers na wewe ni miongoni mwao?
Huwezi kuwa seriuos hata kidogo, ufuatiliwe na gari kutoka iringa hadi dar usiweze kuchukua hata namba ya gari, ndio mana tunasema hii habari ina mashaka mengi ya wazi na yafaa kuipuuza
Namba imetajwa hapo juu.Halafu huna haja ya kushughulika kufungua ID nyingi mpya humu namna hiyo
Mama zitto amelalamika kuvamiwa na kutishiwa kifo ameonekana mwehu, leo wewe kufuatana na watu barabarani unajifanya umefatiliwa...nani apoteze muda na mafuta kuhangaika na ww...ilikuwa mrema bana enzo zake sio nyie, na hajatishiwa
Kumbe huku ndiko ulikokua unaelekea?Pole sana
Kulinda serikali?Hiyo nadharia unaitoa wapi?

Inawezekana ninyi ni miongoni mwao maana taarifa za karibuni ni kuwa mmevamia JF kwa wingi kuja kupambana na stori zinazoumbua taasisi yenu pale madudu mnayofanya yanapoanikwa.Kwa bahati mbaya vijana wameamka sasa hivi na wanajua mnachofanya ndiyo maana wengine hatuogopi kuingia na Verified ID's.

Haya uliyoandika hapo juu unaweza kuja kuthibitisha?
 
sema chochote ili uendelee kujiaminisha kuwa mkombozi wako ni slaa na CDM....if u r waiting for a miracle to happen, utasubiri sana....kitu cha muhimu, u hav to be the miracle, F.Y.I, si kila asiyeunga mkono hoja za slaa na CDM ni mtu wa Magamba, ama serikali!!, wengine wanaweka taifa mbele, vyama na dini nyuma...mnaojiita wanaharakati na wazalendo huku mko tayari kuyafumbia macho mabaya yanayofanywa na CDM kwa ujumla wake, si wazalendo na wala si wanaharakati wa kweli!! mapinduzi ya kimaendeleo na kiutawala hayaletwi kwa matusi kwa fujo wala kwa vurugu......na si kila asiyekubali hoja zenu ni mbaya wenu, sometimes, mnatakiwa kubadilika na kukubali ushauri, muone kama hamtopata washabiki wengi zaidi.....
 
Huyu babu hakuwa na mke wa mtu humo kwenye gari? Maana sasa watu hawatamvumilia tena kupoka wake za zao.
 
Unaweza kuthibitisha hili?Njoo uthibitishe kuhusu hii ID hapa la sivyo.....

CC: Paw Moderator, PainKiller
Namba ya gari ipo hapo juu.Jifunze kusoma acha uvivu
simbilisi,

Pamoja na kuwa watu wengi wamekupuuza ila mimi sitakupuuza.

-Ni jambo gani linaloshindikana kufanyika ikiwa usalama wa taifa umeruhusu Twiga kusafirishwa mchana kweupe?

-Usalama wa Taifa una umakini gani katika kutekeleza mipango yao ikiwa waliruhusu kurekodiwa na vijana wa CHADEMA Sea Cliff Hotel mchana kweupe?

-Usalama wa taiafa una umakini gani ikiwa Ramadhani Ighondu aliweza kuanikwa kweupe?

Unauliza ni nani wa kumuua Dr.Slaa? Ni nani asiyejua usalama wa taifa unatafuta nafasi kukiangamiza na hata kudhuru viongozi wa CHADEMA usiku na mchana kwa kuwa kuna waziri ambaye alisema Chadema kitasambaratika(kauli ya serikali) na Mwingine aliyethibitisha kuwa Dr.Slaa ndiye mgombea tishio kwa uchaguzi mkuu 2015(kauli ya serikali kwa kuwa ni waziri)

-Leo vijana wanahongwa kutoa ushahidi wa uongo dhidi ya viongozi wa Chadema halafu unataka kuonekana great thinker kwa kuwatetea kuwa ni usalama makini? You should grow up

NB:Hebu fanyia kazi jinsi ya kuandika maana mpangilio wa sentesi zako unatisha.
 
Last edited by a moderator:
Mzalendo ni yule anayetaka tuwe na taasisi imara zinazofanya kazi kwa weledi.Unasema unapinga udini na vyama kuwa mbele ya maslahi ya taifa lakini wakati huo huo unaitetea taasisi ya usalama inayotanguliza maslahi ya chama mbele na kutumika kupandikiza mbegu za udini kwa maslahi ya kisiasa na kushindwa kutoa ushauri makini kwa rais.

Taasisi ambayo inamuelekeza waziri kwenda kutoa tamko juu ya nani achinje?

Taasisi iliyoruhusu fedha za EPA zichotwe na kutumika kwenye kampeni za uchaguzi kwa chama tawala huku wakishindwa kumshauri rais juu ya umuhimu wa kufuata utawala bora wa sheria ili wahusika waburuzwe mahakamani badala yake Rais akawaambia warudishe.Ni picha gani hii iliyojengwa kwa vibaka wa mitaani?

Kwamba unasema tukubali ushauri?Nitakishangaa CHADEMA kama kitakubali kila ushauri hata ule wa kipumbavu,tutakua hatuna tofauti na watawala tulio nao wanaoshauriwa kutoa maagizo ya kiserikali kwenye masuala ya dini na kusamehe wazi wa mali za umma.

CHADEMA kinapenda ushauri wenye tija ndiyo maana kuna kitengo cha utafiti na sera ambacho kinaongozwa kwa weledi.Professional consultancy ni nguzo kuu katika utendaji wake hasa yale yanayohitaji professionalism.Make no mistake!

Hilo la CHADEMA kuchukua madaraka linakutisha sana unaandika kwa jazba.Mtaumia wengi ila ni suala la muda tu....na bado.
Huyu babu hakuwa na mke wa mtu humo kwenye gari? Maana sasa watu hawatamvumilia tena kupoka wake za zao.
Nduka,

Hebu soma kwa sauti kubwa hicho ulichoandika hapo.Sometimes it's better to be silent kuliko kujidhalilisha hata kama unatumia ID fake
 
Last edited by a moderator:
Awali ya yote CDM lazima wawe na timu imara yenye ueledi plus 6 senses! Mlichelewa sana kuipiga picha ikiwa ni pamoja na kuiripoti hiyo gari! kuna police wengi sana wanawapenda na kuishabikia CDM. ...Mlipo amua kuweka Mafuta na wao wakawafuata ilikuwa ni wakati muafaka wa kukabiliana nao vilivyo! ...Ninamashaka kidogo na hawa watu maana kama walikuwa na lenngo la kuwadhuru wasinge wafikisha hadi Kibaha! Anyway labda ilikuwa wafanya uharamia wao kwenye Jimbo la Ndugai!!!!
 

Wewe kijana unadahani utawadanganya watu wote, mda wote?. Hivi wewe unauchungu na nchi kuliko watuwote?
Hivi Slaa anapotudanganya mchana kweupe hivi inaingia akilini?
1. Baada ya kuona anafuatiliwa alichukua hatua gani? je aliwatarifu wanausalama wengine wa CDM au alikaa kimya?
2. Hiyo picha mliyoipiga mmeiweka wapi, Mbona hamuibadiki hapa sasa?
3. Inasemekana hilo gari lilokuwa linawafuatilia ni gari la wanausalama la CDM. Ambalo huwa linatumiwa mara chache.
4. Kwanini Mnasema ni Slaa alikuwa anafuatiliwa na sio wengine?
5. kufuatiliwa kuanzia Iringa hadi Dar? dah hii haiingii akilini. So mmechukua hatua gani sasa?

Usipojibu maswali yangu nitakuona Wewe na Slaa ni wajinga.
 
Kawaida ya watu wanaofaidika na mfumo wa kifisadi wako radhi kufanya lolote ilmradi wanalinda maslah yao lakini kwa bahati mbaya wanasahau kuwa watanzania wa sasa wameelimika wanafahamu suluhisho ni CHADEMA Kamanda Ben tuendelee kuwaelimisha kwa hoja watanzania wazalendo wa taifa hili wanaoathirika na mfumo wa kidhalimu wa ccm.
 
Last edited by a moderator:

Huu muda wa kujibu maswali haya ya kipuuzi niupate wapi?Usiwe mvivu wa kusoma.Yote hayo uliyouliza usingekurupuka kuyarudia wakati yalishajibiwa tangu mwanzo wa thread.Labda kichwa chako ni kizito sana kuelewa.Pole
 
Huu muda wa kujibu maswali haya ya kipuuzi niupate wapi?Usiwe mvivu wa kusoma.Yote hayo uliyouliza usingekurupuka kuyarudia wakati yalishajibiwa tangu mwanzo wa thread.Labda kichwa chako ni kizito sana kuelewa.Pole
Kijana saa nane.
Naona unasema huna mda wa kujibu na umesema huu ni upuuzi. sasa wewe kama sio mjinga kwanini muanzishe thread halafu msijibu vitu vya msingi?
Hivi unadhani watu wote wanachukuliwa kirahisi kwa maneno yako yasio na mantiki yeyote.
Sikia kijana Mimi wala sio mgomvi nilivyosema msipo jibu hayo wewe na Slaa mtakuwa wajinga Full stop.
Thread hii nimeifuatilila mwanzo mwisho majibu hayajatolewa.
Hebu kanusha kuwa hili gari ni la CDM.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…