Pre GE2025 Dkt. Slaa ashindwa kufikishwa Mahakamani kutokana na changamoto za usafiri

Pre GE2025 Dkt. Slaa ashindwa kufikishwa Mahakamani kutokana na changamoto za usafiri

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Linus w slaa

New Member
Joined
Jan 29, 2025
Posts
4
Reaction score
7
Kutoka Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo unatarajiwa kusomwa uamuzi juu ya uhalali wa hati ya mashtaka kwenye kesi zinazomkabili mwanasiasa mkongwe nchini Dkt. Wilbroad Slaa.

Dkt. Slaa hajafikishwa mahakamani hapa na sababu iliyoelezwa na upande wa jamhuri kuwa ni uwepo wa changamoto ya usafiri(gari) ambalo lingetakiwa kuwaleta washtakiwa katika mahakama hiyo.

Jibu hilo limetolewa baada ya wakili wa Dkt. Slaa, Peter Madeleka kuhoji juu ya kutofikishwa mahakamani kwa Dkt. Slaa.

Pia soma > Pre GE2025 - Mahakama Kuu yaagiza dhamana ya Dkt. Slaa ishughulikiwe haraka

IMG_20250131_112112_888.jpg

photo_2025-01-31_12-45-34.jpg

photo_2025-01-31_12-45-57.jpg

Kesi ya Dk. Slaa yaendelea bila kuwepo Mahakamani, Wakili wa Jamhuri asema gari lililotakiwa kuleta washtakiwa limepata tatizo la kiufundi

Licha ya Kesi namba 993 ya Mwaka 2025 inayomkabili Dkt. Slaa kutajwa leo Januari 31, 2025 lakini mshtakiwa huyo hajafikishwa Mahakamani kutokana na kilichodaiwa kuwa kumetokea na changamoto ya kiufundi kwenye gari la liliotakiwa kuwaleta watuhumiwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Baada ya Mawakili wa Upende wa utetezi wakiongozwa na Wakili Hekima Mwasipu kutaka kufahamu sababu za mteja wao kutolewa Mahakamani, Wakili wa Jamhuri amejibu kwa kusema kwamba kumetokea tatizo la kiufundi kwenye gari ambalo lilitakiwa kuwaleta washtakiwa mahakamani ikiwemo Dkt. Slaa.

Kesi hiyo inaendelea kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ikiwa ni siku moja baada Mahakama Kuu Tanzania, Masijala Kuu Dar es Salaam kuagiza shauri la Dkt. Wilbroad Slaa lirejeshwe Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwaajili ya kushughulikiwa kwa dhamana yake.

Dkt. Slaa kupitia Mawakili wake walifungua shauri la mapitio la kesi yake katika Mahakama Kuu kupinga mwenendo wa Mahakama ya Kisutu kuahirisha usikilizwaji wa dhamana yake kutokana na maombi ya kupinga dhamana yaliyotolewa na Jamhuri.

Itakumbukwa Dkt. Slaa alikosa dhamana tangu alipofikishwa Mahakamani Januari 10, 2025 kusomewa shtaka linalomkabili la kusambaza taarifa za uongo kupitia Mtandao wa X.
 
Hivi Samia haoni hata aibu?
Magufuli alikua na aibu? Yaani Samia na huyo babu Slaa nani alipaswa kuwa na aibu?? Akae mitandaoni kuzusha hovyo achekewe?? Hivi zile tuhuma nzito mnawaweka kwenye nafasi gani waliodhalilishwa akiwemo Mbowe??

Nyie Hayawani mna akili gani?? Kwamba kuna watu wana exptional right ya kuumiza wenzao ila sio wao??

Ningekua na uwezo wa kuwa nyapala ningeingia alipo huyo mzee nimfanyizie vibaya sana ili akinywee kikombe aone uchungu wake.
 
Lissu ndiyo anamponza ni bora angepotezea atupie mashambulizi akiwa nje ya mahakama kwa kuwapa vifungu mawakili wake.. Hapo akiletwa harudi tena mahabusu. Lissu atapiga spana...
 
CCM A na CCM B.
Mtawakula upinzani kisha mtaanza kulana wenyewe kati yenu nani kanona?
KAZI ni kipimo cha UTU
 
Naunga mkono hoja Lisu angenyuti tu yeye ni Mwanasiasa kwasasa Awe makini yumkini msaada wake, ukawafanya wenzie Wakaaangwe Zaidi!!!!!
 
Ila V8 na mabasi ya kwenda Dodoma kwenye mkutano yapo muda wote na mafuta yamejazwa full.
 
Magufuli alikua na aibu? Yaani Samia na huyo babu Slaa nani alipaswa kuwa na aibu?? Akae mitandaoni kuzusha hovyo achekewe?? Hivi zile tuhuma nzito mnawaweka kwenye nafasi gani waliodhalilishwa akiwemo Mbowe??

Nyie Hayawani mna akili gani?? Kwamba kuna watu wana exptional right ya kuumiza wenzao ila sio wao??

Ningekua na uwezo wa kuwa nyapala ningeingia alipo huyo mzee nimfanyizie vibaya sana ili akinywee kikombe aone uchungu wake.
Kwa hiyo makosa ya serkali ya Samia lazima umhusishe Magufuli?
Au ndo hivo dish lishayumba maana ulivyobweka hapa atadhani umeingiziwa mashine kwenye kinyeo!
Tulia acha uchawa jadili mambo kwa mantiki!
 
Back
Top Bottom