Dkt. Tulia Ackson alikuwa chaguo la Magufuli, hafai kuwa Spika wa Bunge litakalosimamia Serikali ya awamu ya 6

Dkt. Tulia Ackson alikuwa chaguo la Magufuli, hafai kuwa Spika wa Bunge litakalosimamia Serikali ya awamu ya 6

Fundi Madilishi anasema Dr. Tulia alikuwa chaguo la Magufuli na hafai kuwa spika, tukia-assume logic ya Madilisha iko sawa, madam SSH alikuwa mteule wa JPM kama running mate, ushindi wa urais ulikuwa wa JPM kuwa rais na SSH kuwa VP, hivyo kufuatia kifo cha JPM, kikatiba VP anatakuwa kuapishwa na kuwa Rais wa nchi.

Mpango alikuwa mteule wa JPM kama kamishina mkuu wa TRA, mbunge na baadae waziri wa fedha, akagombea ubunge akawa aziriwa fedha tena. Baada ya msiba ilitulazimu tuwe na VP, basi Mpango nae awe haafai kwa logic za Madilisha.

Tanzania ni ya Watanzania wote. Dr. Tulia alikuwa Deputy AG wakati wa JK, ni Mtanzania, mifumo ya uteuzi kwenye chama wakiona anakidhi kuwa spika watampitisha.

Isifikie tukabaguana kisa kwa kuwa fulani alikuwa mteule wa fulani hafai. At some point ni lazima tuishi leo; kama kuna mtu au kundi la watu lina tofauti binafsi na JPM isiwe msingi wa kuwaharibia wengine.

Siko hapa kumpingia debe Tulia, ila yeye kuwa Mtanzania wasitokee wachache wakambagaza kwa kuwa tu aliteuliwa na JPM.

Tukifuata logic yako itabidi serikali yote iondoke ikiwamo wakuu wa vyombo vya dola kwa kuwa majority walikuwa wateule wa JPM.

Jana SSH kaongea kitu kizuri sana, Urais ni taasisi ambayo at some point lazima awepo wa kuiongoza, alianza JKN, AHM, BWM, JMK, JMP na leo tuna SSH na ipo siku atakuwa yule ambae zamu yake itafika.
Inategemeana na tulia anaamini kwenye nn
Kama anaona Mama hatoshi anawezaje kumpa ushirikiano wa kutosha.?
Hii hoja ina macho kuwa ili pasiwepo na lawama aje mpya aendana nae
 
Inategemeana na tulia anaamini kwenye nn
Kama anaona Mama hatoshi anawezaje kumpa ushirikiano wa kutosha.?
Hii hoja ina macho kuwa ili pasiwepo na lawama aje mpya aendana nae
Bunge halipaswi kuwa rubber stamp ya serikali.
Tulia ametokea Serikalini akiwa Deputy AG na lazima atakuwa soft ili apate mafungu kwa wakati ya kuendesha Bunge.
Sio sawa kumtoa kwa kuwa mama anataka mtu mpya.
Job ashaondoka, kama kuna uwezekano aje mtu kama Chenge ambae hawezi kuwa driven na gov machinery.
Awe ni mtu anaejiamini na kusisitiza autonomy ya bunge.

Sina "mahaba" na hoja ya Tulia aondoke kwa kuwa alikuwa mtu wa JPM, hapa tunakosea.
Aje mtu ambae ikitokea mawaziri "wanakomba mboga mpaka wanavimbiwa" anaweza kutaka bunge lichunguze na ikithibitika litoa hoja ya kuondokewa "wanaokomba mboga jikoni"
 
Tunatoa sana ushauri humu JF na wakati mwingine tunaonekana kama wavurugaji waliotumwa na wapinzani au watu tusiokuwa na uzalendo na taifa letu, mwisho wa siku ushauri inapuuzwa na kumsikia mama analalamika kua wapo watu ndani ya serikali hawako naye na wengine hawaelewi.

Tulishauri kwamba Mama anapoanza awamu yake ya 6 aingie na damu mpya itakayomfanya na mifumo yake ya utawala. Mtangulizi wake alikua na mifumo yake na watu wake, watu wake si rahisi sana kwenda na mfumo wa Mama. Kwahiyo mabadiliko ilikua ni muhimu sana katika kila wizara na kila taasisi ili mambo yaweze kwenda sawa sawa.

Turudi kwenye bunge letu la sasa ambalo kimsingi ni sawa na la chama kimoja kutokana na wingi wa wabunge wa CCM. Kiti cha spika kwa sasa kipo wazi, nafasi hii inatakiwa kujazwa na mtu ambaye ni mpya kabisa ambaye hana chembe kabisa za utawala wa awamu ya 5. Dkt Tulia alikua ni Mteule wa JPM, naamini kabisa kwa zaidi ya 90% bado kichwa chake kipo kwa JPM, si rahisi kwenda na mifumo ya Mama. Baadaye anaweza kuja kuwa kikwazo katika bunge na serikali. Tunamjua Dkt Tulia hua ni mbishi, anajua kila kitu hasa sheria, sasa akipewa uspika wenye mamlaka na Kinga itakuwaje?

Chama cha mapinduzi chini ya Mwenyekiti wake mpya wawe makini sana kwenye hii nafasi. Atafutwe mtu mpya mwenye sura ya utawala wa awamu ya 6. Awe mtu wa Makamo, mwenye busara na hekima,awe kama Baba/Mama, mlezi, asiwe kijana na anayejua sheria .

Kwangu mimi kwa hakika Mama Majina angechukua form,huyu Mama ameshakua Mwenyekiti wa bunge akiisimamia vizuri. Mzee Zungu ni mlezi na anajua pia kutoa ufafanuzi kwa kina ikiwa kuna tatizo. Mtu mwingine ambaye Kama angeshauriwa achukue form ya uspika wa bunge ni Mama Dr Asharose Migiro, naye busara zimemjaa sana. Mzee vijisenti naye yupo vizuri sana kwa shughuli za kuendesha bunge.

Chonde Chonde CCM msijidanganye mkaweka Spika kijana mtakuja kujuta, zikianza kelele hataheshimika na wala hatasikilizwa, ataishia kufukuza na kutisha tu kama Ndungai ambaye alilivuruga sana bunge. Naibu Spika abakie kua Dkt Tulia aendelee kujifunza ili akifikisha angalau miaka 50 busara zitakuwepo na atapewa nafasi.
Mwenendo wa Tulia Ackson kama Naibu Spika unaonyesha kwamba yupo tayari kukandamiza demokrasia kwa kumfurahisha mkubwa aliyempa uteuzi. Tulia ni opportunist tu
 
Back
Top Bottom