Dkt. Tulia Ackson amekutana na kufanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu

Dkt. Tulia Ackson amekutana na kufanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
240b6b31-6e8f-43e9-94e5-8ddd63205ee2.jpeg

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 17 Septemba 2024, amekutana na kufanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu, Saqr Ghobash, katika Ofisi za Bunge hilo zilizopo Abu Dhabi.

Katika mazungumzo yao, Viongozi hao wamejadiliana kwa kina kuhusu namna bora ya kuimarisha na kuendeleza ushirikiano mzuri uliopo kati ya Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu pamoja na kuangazia mahusiano kati ya Tanzania na nchi za Umoja wa Falme za Kiarabu.

Mazungumzo hayo yameangazia masuala ya ushirikiano wa kiuchumi, kijamii na kisiasa kati ya pande zote mbili huku lengo likiwa ni kukuza mafanikio ya pamoja na ustawi wa wananchi wao.

5ccae893-5f3b-4ef3-ad7c-3cc54602c4f5.jpeg

e2c195dd-2888-4d1d-aabb-aa9c4ee4c707.jpeg
 
Back
Top Bottom