Dkt. Tulia: Nyanda za Juu tumechoka kuwa washangiliaji na sisi tunataka treni ya umeme kama 'Wenzetu'

Kipindi jiwe anapeleka miradi isiyo na idadi chato wala hakuyasema haya.

Zaidi walishangilia na kuunga mkono
Na angekuwepo Mwendazake huyo Yulia asingesubutu kiongea chochote,maana hata huo ubunge aliupata ni wa promotion.
 
Kwahiyo katiba mpya ndio suluhisho?

Pale Kenya haijawasaidia chochote wako kwenye BBI mahakamani!

..unahitaji katiba nzuri.

..vilevile unahitaji wanasiasa wenye utu, watakaoheshimu katiba.

..Kenya wasingekuwa na katiba nzuri wangekuwa ktk matatizo makubwa kuliko waliyonayo sasa hivi.

..Marekani pia wangekuwa na katiba ya hovyo hovyo Trump asingeondoka madarakani.

..Trump alijaribu kumshinikiza msimamizi wa uchaguzi jimbo la Georgia ambaye ni mwanachama wa Republican amsaidie kuiba kura.

..Katiba ingekuwa ya hovyo, na msimamizi wa uchaguzi jimbo la Georgia angekuwa haheshimu sheria Trump angeiba uchaguzi.
 
Mi kweli tusije ondoa focus ya madai ya wana Mbeya ya muda mrefu kupuuzwa na serikali za Awamu zote.

..tazara ni reli nzuri. Inachohitaji ni ukarabati.

..na siyo lazima iwe reli ya umeme. Angola wamejenga upya reli yao ya kwenda Benguela Port kwa standard sawa na Tazara ambayo ni Cape Gauge Rail.

..kwa maoni yangu, reli ya Dar-Kilimanjaro haina umuhimu kulinganisha na reli ya Tazara. Serikali ilifanya makosa kukarabati reli hiyo sasa hivi, kabla ya kuikarabati na kuifufua reli ya Tazara.

..Dr.Tulia na wabunge wenzake wa Mbeya walitakiwa waishauri vizuri serikali kuhusu reli ipi ilikuwa muhimu zaidi, na ilistahili kutengewa fedha kwanza.
 
Swadakta mkuu.
Lakini ukweli uko palepale Serikali karibia awamu zote hazijawekeza mkoani Mbeya.
Sijui ni kwa sababu zipi.

Hili la Mbeya kweli ni kama Halmashauri, Halina hadhi ya Jiji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…