Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es salaam imemuachilia huru Dkt. Wilbord Slaa baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini DPP kueleza kuwa hana nia ya kuendelea na shauri hilo.
Shauri Na.993 la mwaka 2025 lilidai Dkt. Slaa ameshtakiwa kwa kuchapisha taarifa za uongo kupitia ukurasa wa X (zamani Twitter).
Leo February 27,2025, Wakili wa Serikali Mwandamizi Job Mrema amewasilisha nia ya DPP mbele ya Hakimu Mfawidhi Franco Kiswaga .
Wakili Mrema ameieleza Mahakama kuwa DPP ameamua kutoaendelea na shauri hilo kwa mujibu wa kifungu cha 91 (1) cha mwenendo wa makosa ya jinai.
Huyu mzee tangia lile tukio la 2015 kuhama chama dkk za jion, na ushawishi wote ule sijawah kumuelewa tena ,,,, Badae akalamba ubaloz kwa JPM, badae karudi, mara anachukizwa na wanaosema FAM sio gaidi, then mara tena anaonekana yupo against government, anakamatwa,,, kwa kifupi haeleweki ! Hivi lile lijanamke alilioa uzeeni alienda nalo Canada bado wapo ama ! Tumepitia mengi sana kama nchi
Kulikuwa na haja gani ya kumshikilia huyo mzee wa watu siku zote hizo, au kuna somo alikuwa anafundishwa kaelewa ndiyo kaachiwa?
Hapo brake ya kwanza iwe hospital akafanye body check up