EINSTEIN112
JF-Expert Member
- Oct 26, 2018
- 21,711
- 35,644
Kufuatia mashambulio makubwa ya anga kote Ukraine leo, Rais wa zamani wa Urusi Dmitry Medvedev alionya "kutakuwa na mengine". Akiandika kwenye mitandao ya kijamii, mshirika wa karibu wa Rais wa Urusi Vladimir Putin aliashiria kwamba kuongezeka kwa mashambulizi kunaweza kuwa mwanzo wa kuongezeka zaidi kwa vita kwa upande wa Urusi.
"Ukraine itakuwa tishio la mara kwa mara, la moja kwa moja na la wazi kwa Urusi," aliandika. "Lengo la hatua zetu za siku za usoni lazima liwe kuuvunja kabisa utawala wa kisiasa nchini Ukraine."
Mhariri wa BBC wa Urusi Steve Rosenberg anasema taarifa ya aina hii inaonyesha kwamba, ikiwa kweli huu ndio mtazamo wa Kremlin, Urusi inaweza kutaka kuendelea na vita hadi ihakikishe Ukraine nzima imerejea katika mzunguko wa Urusi.
Urusi ilituma makombora katika maeneo mbalimbali ya Ukraine siku ya Jumatatu
Mashambulizi hayo yanajiri siku mbili baada ya daraja pekee linalounganisha Urusi na Crimea inayokaliwa kimabavu na nchi hiyo kushambuliwa.
Hapo jana, Rais Vladimir Putin alilaumu idara za ujasusi za Ukraine kwa kile alichokiita kitendo cha kigaidi.
Anatarajiwa kuongoza kikao cha baraza lake la usalama leo kujadili mlipuko huo.
Maafisa wa Ukraine wanasema idadi kubwa ya watu wamejeruhiwa katika mashambulizi ya makombora huko Zaporizhzhia usiku kucha.
"Ukraine itakuwa tishio la mara kwa mara, la moja kwa moja na la wazi kwa Urusi," aliandika. "Lengo la hatua zetu za siku za usoni lazima liwe kuuvunja kabisa utawala wa kisiasa nchini Ukraine."
Mhariri wa BBC wa Urusi Steve Rosenberg anasema taarifa ya aina hii inaonyesha kwamba, ikiwa kweli huu ndio mtazamo wa Kremlin, Urusi inaweza kutaka kuendelea na vita hadi ihakikishe Ukraine nzima imerejea katika mzunguko wa Urusi.
Urusi ilituma makombora katika maeneo mbalimbali ya Ukraine siku ya Jumatatu
Mashambulizi hayo yanajiri siku mbili baada ya daraja pekee linalounganisha Urusi na Crimea inayokaliwa kimabavu na nchi hiyo kushambuliwa.
Hapo jana, Rais Vladimir Putin alilaumu idara za ujasusi za Ukraine kwa kile alichokiita kitendo cha kigaidi.
Anatarajiwa kuongoza kikao cha baraza lake la usalama leo kujadili mlipuko huo.
Maafisa wa Ukraine wanasema idadi kubwa ya watu wamejeruhiwa katika mashambulizi ya makombora huko Zaporizhzhia usiku kucha.