Doctors mnavunja sana maadili yenu!!


Hapa umegeneralize na kwenda kwenye extremes...
 

To generalize is to be an idiot.
 
To generalize is to be an idiot.

kuna vitu huwa vinaongelewa na watanzania kama kawaida wanasahau na kurudi kule kule! Kuna uzi jf photo unahusu HIV watu wamepost picha mbali mbali ambazo kwa sehemu kubwa zimevunja maadili ya fani ya udaktari. Na waliopost zile picha ni madaktari tu. Kuna picha huwezi kuzikuta kwa mtu wa kawaida ambaye siyo mdau wa wodini. Sasa zile ndo medical ethics mnazofundishwa?? Watu tulishaachana na vita ya kutishia watu waliokonda nyie mnaturudisha kwenye unyanya paa?? Mbona nyie ndo mnatakiwa muwe watunzaji wa siri za wagonjwa wenu? Kuna jamaa pale ameshatambuliwa na kama yumo humu mnadhani atafurahi? Nashukuru mods wameufunga, maana mnazidi kujivunjia heshima mbele ya jamii.
 
Mkuu Usungilo,

1. Sijui ni uzi upi(ila nakumbuka ule wa mtu aliyekuwa amelala kitandani na nguo ya blue nadhani), ila sijui una uhakika gani kusema ni "madokta tu", kama ulivyosema katika post yako hapo juu, ni watu wengi wanaofanya kazi hospitalini.

2. Nadhani si sahihi kutumia kigezo kimoja tu cha kukonda kama ndiyo uthibitisho kuwa mtu ana UKIMWI, kuna magonjwa mengi ambayo yanaweza kusababisha mtu kukonda sana (saratani/cancer, utapiamlo/adult malnutrition to be specific)..

Sina uhakika kama daktari aliyesoma ethics na mwenye kukutana na wagonjwa mbalimbali kila leo anaweza kupost picha za mgonjwa..hii haimaanishi haiwezekani but personally i think it is next to impossible, kwani sioni sababu za kufanya hivyo, ..yaani a_post hizo picha za mfano wa wagonjwa anaowaona kila leo kwa lengo gani?
But regardless of who did it it's not morally acceptable mkuu.
 
Ukimwi haubagui, sisi tunabagua... Ugonjwa una umri wa karibu miaka 30; lakini watu wanataka bado uwe siri...siri ya nini?
 
Ukimwi haubagui, sisi tunabagua... Ugonjwa una umri wa karibu miaka 30; lakini watu wanataka bado uwe siri...siri ya nini?

kila mtu atajitangaza kwa mdomo wake na sio mtu mwingine amtangaze bila ridhaa yake. Ndo maana hata msibani ndugu ndo wanaoruhusu huo utangazaji wa chanzo cha kifo cha marehemu. Angekuwa ndugu yako anaanikwa akiwa amelazwa ungefurahi?
 
Mkuu hippo..., kuna uzi umefungwa na mods zilikuwa zinawekwa picha za namna hiv inavyojitokeza kwa watu. Sizikatai zile picha,ugomvi wangu ni kwa nini uoneshe na sura ya mtu? Kwa nini usifiche sura, tena na ndugu yake kabisa??? Yes nakubaliana na wewe, wanaofanya kazi hospitali sio drs tu lakini kuna vitu ni classical from a doctor!! Naomba usiwatetee wote kuna vyuo wanachakachuliwa siku hizi, no ethics kabisa! Wapo wenye heshima zao, salute kwao! Ila hawa product za siku hizi wakikosa muvi ndo mambo wanayoyafanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…