Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Maafisa wa Polisi nchini wametakiwa kuimarisha uelewa wao kuhusu sheria zinazohusiana na uchaguzi ili kuepuka ushawishi wa kisiasa wa wanasiasa wanaojaribu kupotosha sheria hizo kwa maslahi yao.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima Ramadhani, alitoa wito huu wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Wakuu wa Upelelezi wa Wilaya yaliyofanyika Oktoba 17, 2024, mkoani Dodoma.
Kailima alisisitiza umuhimu wa mafunzo haya katika kipindi hiki ambapo kuna Sheria Mpya mbili zinazosimamia masuala ya uchaguzi, ambazo ni Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya mwaka 2024, pamoja na Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 2 ya mwaka 2024.
Kailima alisema kuwa, mafunzo haya yatasaidia Wakuu wa Upelelezi kuwa mabalozi wa kuhamasisha wananchi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Soma pia: Tume Huru ya Uchaguzi yakamilisha mchakato wa kutoa elimu kwa wananchi Zanzibar. Mchakato wa uandikishaji umeanza rasmi leo!
Aidha, washiriki walijifunza wajibu wa Jeshi la Polisi wakati wa uchaguzi, utambuzi wa bidhaa bandia, pamoja na masuala mengine muhimu yanayohusiana na mchakato wa uchaguzi. Lengo la mafunzo ni kuwajengea uelewa wa haki za vyama, wananchi, na makundi mengine katika kipindi chote cha uchaguzi.
PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - INEC watoa elimu kwa Wakuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) ili kuliweka tayari Jeshi la Polisi wakati wa mchakato wa Uchaguzi
Source: Tovuti ya INEC
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima Ramadhani, alitoa wito huu wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Wakuu wa Upelelezi wa Wilaya yaliyofanyika Oktoba 17, 2024, mkoani Dodoma.
Kailima alisisitiza umuhimu wa mafunzo haya katika kipindi hiki ambapo kuna Sheria Mpya mbili zinazosimamia masuala ya uchaguzi, ambazo ni Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya mwaka 2024, pamoja na Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Na. 2 ya mwaka 2024.
Kailima alisema kuwa, mafunzo haya yatasaidia Wakuu wa Upelelezi kuwa mabalozi wa kuhamasisha wananchi kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Soma pia: Tume Huru ya Uchaguzi yakamilisha mchakato wa kutoa elimu kwa wananchi Zanzibar. Mchakato wa uandikishaji umeanza rasmi leo!
Aidha, washiriki walijifunza wajibu wa Jeshi la Polisi wakati wa uchaguzi, utambuzi wa bidhaa bandia, pamoja na masuala mengine muhimu yanayohusiana na mchakato wa uchaguzi. Lengo la mafunzo ni kuwajengea uelewa wa haki za vyama, wananchi, na makundi mengine katika kipindi chote cha uchaguzi.
PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - INEC watoa elimu kwa Wakuu wa Polisi wa Wilaya (OCD) ili kuliweka tayari Jeshi la Polisi wakati wa mchakato wa Uchaguzi
Source: Tovuti ya INEC