Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Kunaanza kunoga huko😂😂😂.
=====
Wamachinga wa Soko la Wazi la Machinga Complex, jijini Dodoma, wameandaa sherehe ya kipekee kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, itakayofanyika Januari 27, 2025.
Katika kusherehekea tukio hilo, wamachinga hao wametangaza punguzo la asilimia 30 kwa bidhaa zote sokoni hapo.
Mwenyekiti wa soko hilo, Nyamageni Kingamkono, amesema hatua hiyo ni njia ya kumshukuru Rais Samia kwa jitihada zake za kuboresha maisha ya wafanyabiashara wadogo.
Pia soma: Wafanyabiashara Dodoma Wamshukuru Rais Samia kwa Ujenzi wa Machinga Complex
Sherehe hiyo itapambwa na burudani za kipekee kutoka kwa wasanii wa soko hilo, ambapo mfanyabiashara Shehani Edwards amesema kuwa itakuwa ni siku ya pekee kwa taifa.
Wafanyabiashara hao wamesisitiza kuwa hatua hiyo ni ishara ya kutambua mchango wa Rais Samia katika maendeleo ya sekta ya biashara ndogondogo nchini.
Kunaanza kunoga huko😂😂😂.
=====
Wamachinga wa Soko la Wazi la Machinga Complex, jijini Dodoma, wameandaa sherehe ya kipekee kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, itakayofanyika Januari 27, 2025.
Katika kusherehekea tukio hilo, wamachinga hao wametangaza punguzo la asilimia 30 kwa bidhaa zote sokoni hapo.
Mwenyekiti wa soko hilo, Nyamageni Kingamkono, amesema hatua hiyo ni njia ya kumshukuru Rais Samia kwa jitihada zake za kuboresha maisha ya wafanyabiashara wadogo.
Pia soma: Wafanyabiashara Dodoma Wamshukuru Rais Samia kwa Ujenzi wa Machinga Complex
Sherehe hiyo itapambwa na burudani za kipekee kutoka kwa wasanii wa soko hilo, ambapo mfanyabiashara Shehani Edwards amesema kuwa itakuwa ni siku ya pekee kwa taifa.
Wafanyabiashara hao wamesisitiza kuwa hatua hiyo ni ishara ya kutambua mchango wa Rais Samia katika maendeleo ya sekta ya biashara ndogondogo nchini.