Dodoma: Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe avamiwa, apigwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana

Dodoma: Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe avamiwa, apigwa na kujeruhiwa na watu wasiojulikana

denooJ

JF-Expert Member
Joined
Mar 31, 2020
Posts
18,509
Reaction score
68,228


EAA5D661-5A75-49D2-BDC1-3F4C9219B536.jpeg

2633C52F-FC62-46B5-BE09-4AB97CC7C6CA.png


Salaam,

Taarifa nilizozipata hivi punde toka chanzo changu kinanihabarisha kuwa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Freeman A. Mbowe amevamiwa na kikundi cha watu wasiojulikana akielekea nyumbani kwake usiku huu na kupigwa na wamemuumiza.

Tukio hili limetokea majira ya saa 6-7 usiku.

Mhe. Mbowe amekimbizwa Hospitali ya Ntyuka iliyopo jijini Dodoma.

Kamanda Muroto amesema wamepata taarifa kuwa kavunjwa mguu wa kulia na amelazwa Wodi namba 4 hospitalini hapo. Amesema taarifa zaidi zitafuata

UPDATES
FREEMAN MBOWE AHAMISHIWA DAR KUTOKEA DODOMA


Kiongozi huyo wa Kambi rasmi ya Upinzani, ametolewa katika hospitali ya DCMC jijini Dodoma na kusafirishwa kwenda jijini Dar kwa matibabu zaidi

Mnadhimu wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, Esther Bulaya amesema wataeleza baadaye ni hospitali gani anakwenda kutibiwa Mbowe, akifika jijini Dar

Daktari anayemtibu amesema hali ya Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai inaendela vizuri ila ni maumivu bado yupo nayo kutokana na kuvunjika kwa mfupa wa mguu wa kulia


MAONI YANGU:
Mhe. Mbowe kuvamiwa na kupigwa eneo la Area D, jijini Dodoma, Mtaa wa Sengia; linalotajwa kuwa na ulinzi wa kutosha, kama ilivyotokea kwa Lissu kunaacha maswali mengi, je, hili linaweza kuwa limechochewa na Lissu kutangaza nia ya kugombea Urais wa JMT October 2020? Ni hasira au kitu gani? No one knows.

Bado najiuliza; hivi kama Taifa kwa tabia hizi za kihuni tunaelekea wapi? Hawa wanaojichukulia sheria mikononi kila siku wanafanya hivyo kwa kutumwa na nani? Matendo haya yataendelea kwa viongozi wa upinzani mpaka lini?

We need to wake up, better late than never.

PIA SOMA
- Uelewa wangu juu ya kundi la watu wasiojulikana

~ Matukio ya Watu kupotea na wengine kudaiwa kutekwa, nini kinaendelea kuhusu usalama wa raia

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana
 
Nianze Kwanza kwa Kutoa Pole zangu za dhati kabisa kwa Mheshimiwa Freeman Mbowe, Familia yake, Wapiga Kura wake, Wanachama wake wa CHADEMA, Wanasiasa mbalimbali, Wabunge na Sisi Watanzania wa kawaida tusioegemea upande wowote ule (Mzukulu) nikiwemo kwa kilichotokea. Naamini Mwenyezi Mungu ataupigania Uhai wake ila kwa waliohusika Maulana / Mola atawajibu kwa Adhabu Kali kabisa.

Jana nilipoziona tu zile Nondo Kali na zenye Mashiko za Mheshimiwa Tundu Lissu nilihisi kabisa kuwa ili kuwapoteza Watu na Kuyahamisha Mawazo yao katika Kukijadili au Kuyajadili yale aliyoyaandika ambayo yote ni mazuri basi ni lazima tu Spinning ya Hatari ingefanyika. Kilichofanyika ni kutaka Kufunika alichokifanya Lissu jana kuanzia leo Watanzania wote tujikite zaidi katika Kuzungumzia hili lililomkuta Mheshimiwa Freeman Mbowe.

Na Kiutaalam zaidi ili kuonyesha kuwa hawa Wahuni wanaolelewa vibaya na walijipanga ni kwamba itakuwa walijipanga tokea pale Taarifa za Mheshimiwa Tundu Lissu aliposema kuwa atazungumza na Watanzania hivyo hata Wao walishajipanga na walipoona Jana Mheshimiwa Tundu Lissu katoa Nondo ile Kabambe basi na Wao wakaamua Kulitekeleza hilo walilolitekeleza.

Kuna Mmoja namuheshimu sana humu ila sasa nitaanza Kumdharau amesema kuwa Mheshimiwa Mbowe Kavamiwa na Majambazi akiwa na Kimada aliyemnunua. Ameshindwa kujua ya kwamba Siku zote Mbinu za Kijasusi huwa zinaratibiwa vyema na Kimkakati zaidi kwa kuwahusisha Magenge ya Wahuni ili hata likija Kufanikiwa basi hao Majasusi wasijulikane moja kwa moja kama ni Wao.

Kwa hali ilivyo na kwa uelewa wangu mdogo sana wa Masuala ya Usalama ( Ujasusi ) ila wale wanaojua zaidi yangu hapa JF watanisaidia ni kwamba kwa Nyakati tuliopo na kwa Hofu ya Wapinzani na Agenda zao, na kwa Uchungu wa Kulikosa Jimbo la Hai ambalo wanalitaka na kwa kutaka Kuleta Hofu na Vitisho nitakuwa wa mwisho Kuamini kama katika hili Tukio la Mbowe hayo Mapanga hayakuwa na Sumu za Kijasusi.

Namalizia tu kwa kusema kama Tanzania ya sasa imefikia hapa ambapo Wanasiasa wanafanyiwa mambo haya mabaya halafu nchi ina Kiongozi Mkuu na ina Idara yake ya Usalama na mambo (matukio) haya yanatokea kila Kukicha ila wanayanyamazia basi huenda kwa Mwaka huu Tanzania ikawa na Vifo vingi vya Wanasiasa (hasa wa Upinzani) na Wanaharakati kuliko wale ambao labda CORONA ingewauwa au imewauwa.

Nawaombea LAANA mbaya sana na Kali mno kwa Mwenyezi Mungu hawa Wote wanaoyafanya haya na hasa huyo Mkubwa wao anayewatuma.
 
Tanzania imefika huko? Ni matumaini yangu tukio hili litachunguzwa mara moja na Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma RPC Muroto na askari wake watahakikisha wahuni hao wanakamatwa mara moja.

Toka maktaba:
May 26, 2020
Kamanda aliapa Dodoma kuwa salama kwa viongozi wote waliohamia hapo jijini kuanzia rais na wakaazi wote wa mji huo Mkuu wa Tanzania

 
Wanachadema wakiongozwa na ngurumo wameanza kuvumisha taarifa za uongo kuwa amepigwa so sad,Waliokuwepo maisha club watasema ukweli,jinsi mbowe alivyosukumwa na kimada wake aliemnunua hapa [emoji117][emoji117][emoji117][emoji117]usitumie nguvu nyingi kupotosha ukweli

Jr[emoji769]
Unajua ana Mke na watoto, hivyo haiwezekani kimada au awe mchepuko, itakuwa ni "wahuni" hii kisiasa na kifamilia ndio inakaa vizuri zaidi.

Na zaidi ya hapo hakuwepo hapo Maisha club sababu ya lockdown ya nchi jirani maana sisi hatufuati who directives , watakuwa "wahuni" wamemleta hapo
 
Yeye ndo kaleta taarf mdaa huo huo Wana chadema ngoja tusubili kesho na iyo IT yako kama tudada twa snp
 
Back
Top Bottom