Dodoma: Sitta apita;asubiri kupitishwa

Dodoma: Sitta apita;asubiri kupitishwa

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Lile vuguvugu lililoanzishwa na Wajumbe Huru (WAHU) la kutaka Samwel John Sitta kuwa Mwenyekiti wa Kudumu wa Bunge la Katiba limefikia pazuri.Sasa,karibu kila Mjumbe anamtaja Sitta kwa hili au lile ilimradi tu kumuunga mkono. Mmoja wa viongozi wa WAHU amenidokeza kuwa tayari Sitta ameshapita mbele ya Wajumbe na wanachosubiri sasa ni chama chake cha CCM kuleta jina lake Bungeni kwa nafasi hiyo.

'Hapa tayari.Tunaisubiri CCM ituletee jina lake hapa kama mgombea.Unajua...mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi kama hizi huwa ni wa ki-chama zaidi. Wakituangusha katika hili,tutawaangusha katika mambo mbalimbali ya kichama' alisema kiongozi huyo wa WAHU bila ya kusema wataiangusha CCM katika mambo gani.

Kwa hali ilivyo hapa katika viunga vya Bunge la Katiba Dodoma, Sitta hana mpinzani. Kwa siasa za Tanzania lakini chochote chaweza kutokea. Na Wajumbe watalazimika kusimamia wanachokiamini. Vile watakavyoona inafaa. Yetu macho na masikio!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
 
recycling bin....

then badae tunalalamika kama bata mzinga
 
Tehe tehe tehe.! Sidhani, lakini afadhali ya huyu kuliko Meembe (kikwete 2.0).!

Bora na wewe huwa unamwona huyu jamaa, yaani unakuta watu wanamwaza kuwa rais, itakuwa tu toleo la pili la lililopo tena yaweza kuwa mbaya zaidi.

Hapa kwa mzee Six hata mimi naamini atapunguza ujinga huko bunge la katiba, tena naenda kupata nafasi ya kuonyesha kama ni wa wanainchi au wa kwao
 
Sipati picha output ikiwa negative na matarajio ya wengi chini ya mh. Sitta
 
Kama mtu mmoja anazungumzwa na kila mtu kwamba bila yeye mambo yataenda kombo basi ujue tatizo kubwa lipo!

Kuiachia CCM pekee jukumu la kumtoa Mwenyekiti wa Kudumu Bunge la Katiba ni udhaifu na ulegelege wa vyama vingine vya siasa!

Kila mtu kwa sasa eti anamzungumza Mhe. Sita kwa mazuri ilhali wengi walimuona hafai kuongoza Bunge la JMT!

Mimi nasubiri tu kusikia vilio vya watanzania mambo yatakapokuwa kinyume na matarajio.

Wazungu wanasema 'what goes around comes around'!
 
Over my dead body!.
Pasco

You are saying that bcoz you know hatapitishwa na ccm? Otherwise, sidhani una ubavu wa kumzuia kama akipitishwa. That kind of statement is only given by people who have power/ authority to stop something from happening - Do you have it?
 
Lile vuguvugu lililoanzishwa na Wajumbe Huru (WAHU) la kutaka Samwel John Sitta kuwa Mwenyekiti wa Kudumu wa Bunge la Katiba limefikia pazuri.Sasa,karibu kila Mjumbe anamtaja Sitta kwa hili au lile ilimradi tu kumuunga mkono. Mmoja wa viongozi wa WAHU amenidokeza kuwa tayari Sitta ameshapita mbele ya Wajumbe na wanachosubiri sasa ni chama chake cha CCM kuleta jina lake Bungeni kwa nafasi hiyo.

'Hapa tayari.Tunaisubiri CCM ituletee jina lake hapa kama mgombea.Unajua...mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi kama hizi huwa ni wa ki-chama zaidi. Wakituangusha katika hili,tutawaangusha katika mambo mbalimbali ya kichama' alisema kiongozi huyo wa WAHU bila ya kusema wataiangusha CCM katika mambo gani.

Kwa hali ilivyo hapa katika viunga vya Bunge la Katiba Dodoma, Sitta hana mpinzani. Kwa siasa za Tanzania lakini chochote chaweza kutokea. Na Wajumbe watalazimika kusimamia wanachokiamini. Vile watakavyoona inafaa. Yetu macho na masikio!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
Mzee VUTA-NKUVUTE safari hii sifa ya kugombea sharti kuwa mwanamke iliondolewa.
Ni kipengere kilimshinda uspika safari ileeeee!
 
Last edited by a moderator:
Anafaa kuwa Spika sio Presidaa.....6 hana Qualities za kuwa Presidaa wa Tz
 
Back
Top Bottom