LGE2024 Dodoma: Wananchi wamkataa mgombea wa CCM wadai wamechoka kuonewa

LGE2024 Dodoma: Wananchi wamkataa mgombea wa CCM wadai wamechoka kuonewa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Wakazi wa Mtaa wa Chinyoya, Kata ya Kilimani, Wilaya ya Dodoma Mjini, jijini Dodoma, wamepinga uteuzi wa mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) anayewania nafasi ya uenyekiti, wakidai kuwa mgombea huyo ameonesha tabia za kujifanyia maamuzi kwa matakwa yake binafsi na kutumia ubabe katika uongozi.

Wakiwa na waandishi wa habari mtaani hapo, wakazi hao wameeleza kuwa mwenyekiti huyo mteule amekuwa akiendeleza migogoro ya ardhi na kuchochea malalamiko kwa kutumia nafasi yake. Wameeleza kuwa hatua ya CCM kuteua mgombea huyo imewaumiza wananchi, na wanaona ni kama chama hakijazingatia maslahi ya wananchi wake.

Katika siku za karibuni, kumekuwepo na malalamiko mengine mkoani Dodoma kuhusu uteuzi wa wagombea wa serikali za mitaa kwa chama hicho, ambapo baadhi ya watia nia waliopendekezwa na wajumbe hawakurudishwa, na majina mapya yasiyochaguliwa yakipewa kipaumbele. Malalamiko haya yametokea pia katika wilaya za Mpwapwa na Chemba.

 
Ha
Wakazi wa Mtaa wa Chinyoya, Kata ya Kilimani, Wilaya ya Dodoma Mjini, jijini Dodoma, wamepinga uteuzi wa mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) anayewania nafasi ya uenyekiti, wakidai kuwa mgombea huyo ameonesha tabia za kujifanyia maamuzi kwa matakwa yake binafsi na kutumia ubabe katika uongozi.
Hawa wanachama wa CCM mimi siwaelewi. Kwani kura za maoni ndio uchaguzi? Wana uhakika gani kuwa huyo wanayempenda atashinda uchaguzi? Hawa wamezoea kupita bila kupingwa. Safari hii hakuna mbeleko lazima wapambane kwenye kura.
 
Wakazi wa Mtaa wa Chinyoya, Kata ya Kilimani, Wilaya ya Dodoma Mjini, jijini Dodoma, wamepinga uteuzi wa mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) anayewania nafasi ya uenyekiti, wakidai kuwa mgombea huyo ameonesha tabia za kujifanyia maamuzi kwa matakwa yake binafsi na kutumia ubabe katika uongozi.

Wakiwa na waandishi wa habari mtaani hapo, wakazi hao wameeleza kuwa mwenyekiti huyo mteule amekuwa akiendeleza migogoro ya ardhi na kuchochea malalamiko kwa kutumia nafasi yake. Wameeleza kuwa hatua ya CCM kuteua mgombea huyo imewaumiza wananchi, na wanaona ni kama chama hakijazingatia maslahi ya wananchi wake.

Katika siku za karibuni, kumekuwepo na malalamiko mengine mkoani Dodoma kuhusu uteuzi wa wagombea wa serikali za mitaa kwa chama hicho, ambapo baadhi ya watia nia waliopendekezwa na wajumbe hawakurudishwa, na majina mapya yasiyochaguliwa yakipewa kipaumbele. Malalamiko haya yametokea pia katika wilaya za Mpwapwa na Chemba.

Achane na mambo ya mama tusaidie! Kwani mmefungiwa huko ccm. Chagueni chama mbadala,acheni kuwa kama Chonya of Chilonwa!
 
Achane na mambo ya mama tusaidie! Kwani mmefungiwa huko ccm. Chagueni chama mbadala,acheni kuwa kama Chonya of Chilonwa!
Da chonya of chilonwa umenikumbusha kitabu cha SHIDA kili
choandikwa na NDYANAO BALISIDYA.
 
Back
Top Bottom