Dodoma: Wanne mbaroni kwa kumuua ndugu yao na kumkata viungo

Dodoma: Wanne mbaroni kwa kumuua ndugu yao na kumkata viungo

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
JESHI la Polisi mkoa wa Dodoma limewakamata ndugu wanne wa familia moja wanaotuhumiwa kumuua ndugu yao na kisha kumkata miguu yote miwili chini ya magoti na kuufunika mwili kwa mahindi yaliyopukuchuliwa na kuuchoma moto.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Onesmo Lyanga alisema jana kuwa, watuhumiwa hao ni wakazi wa kijiji cha Daki, tarafa ya Mondo, wilaya ya Chemba, mkoani Dodoma.

Alimtaja aliyeuawa kuwa ni Rashid Nduata (40) na kwamba iligundulika aliuawa ndani ya nyumba yake.

Kwa mujibu wa Kamanda Lyanga, Nduata aliuawa kwa kunyongwa shingo, kuchomwa na kitu chenye ncha kali shavu la kulia, kupigwa na kitu kizito kwenye taya la juu na chini na kisha kukatwa miguu sehemu ya chini ya magoti.

“Mwili wake ulifunikwa na mahindi yaliyopukuchuliwa na kuchomwa moto,” alisema.

Alisema wanafunzi kijijini hapo walikuwa wakipita kando ya nyumba hiyo na kuona moshi ukitoka ndani na ndipo walitoa taarifa.

Kamanda Lyanga alisema chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa ardhi kati ya marehemu na ndugu zake. “Watu wanne wamekamatwa kwa mahojiano kuhusiana na tukio hilo,” alisema

HabariLeo
 
Kwa mujibu wa Kamanda Lyanga, Nduata aliuawa kwa kunyongwa shingo, kuchomwa na kitu chenye ncha kali shavu la kulia, kupigwa na kitu kizito kwenye taya la juu na chini na kisha kukatwa miguu sehemu ya chini ya magoti.
emoji848.png
emoji848.png
emoji848.png
emoji2827.png
emoji2827.png
emoji2827.png
emoji31.png
emoji31.png
emoji31.png
 
Duuh. Aisee ikiwa ninkweli aisee sheria ya kunyongwa inawahusu hawa wauaji maana sio kwa unyama kama huo
Simnasemaga kinyume na haki za binadamu kunyongwa?

nambie boss mashetani Kama hao usiwanyonge kwanini??
ndiomaana katika Taurat imeandikwa anaeua nae auwawe, na mwizi akatwe mkono,

Cha ajabu leo anaeua kinyama anaonewa huruma kuliko unyama aliofanya!!
 
Ahsante kwa taarifa.
Kutokana na habari za moto unazotupatia kila siku mkuu, hii profile name yako ilifaa kabisa uitwe digitali malenga na siyo analogia malenga.
 
Simnasemaga kinyume na haki za binadamu kunyongwa?

nambie boss mashetani Kama hao usiwanyonge kwanini??
ndiomaana katika Taurat imeandikwa anaeua nae auwawe, na mwizi akatwe mkono,

Cha ajabu leo anaeua kinyama anaonewa huruma kuliko unyama aliofanya!!
Wanasema hao co.mimi umeona nilichosema hapa?
 
Mali za urithi zina shida sana. Ona sasa!! Hiyo ardhi yenyewe, wote wanaiacha!! Ujinga mtupu.
 
Back
Top Bottom