Donald Ngoma arudi South Afrika kutibiwa

Donald Ngoma arudi South Afrika kutibiwa

Mpachika mabao wa Yanga aliyeongezewa mkataba hivi juzi kati,Donald Ngoma amerejea Afrika Kusini anako tibiwa!

Ngoma ambaye karibia msimu wote uliopita hakuwa fiti,amerejea tena kupata matibabu kutokana na afya yake kutokuwa fiti
Tairi kipara, pancha kwenda mbele!
 
Atibiwe apone haraka ashiriki ngao ya hisani pengine anaweza kufanya matokeo yakawa Simba 5 Yanga 1
Hizi ni ndoto za mchana.

Zile tano za kipindi kile tulikuwa na mgogoro wa kumuondoa Nchunga kwenye nafasi yake. Sasa hivi hatuna mgogoro wa jinsi hiyo maana hata Mwenyekiti ameachia ngazi mwenyewe. Ni Lazima tuwakandamize na usajili wenu wa majina.

Ajibu mtamuomba radhi asiendelee kuwasulubu maana huyo ndiye ataongoza maangamizi huku jamaa yenu Tambwe akikamilisha kikapu cha magoli.

Jiandaeni kisaikolojia, tuna hamu na nyie tuwaoneshe kuwa soka la sasa siyo kusajili kwa majina yaliyovuma huko siku za nyuma. Soka la sasa ni la vipaji hivyo ni lazima kuzingatia status quo ya mchezaji na siyo historia yake.
 
Back
Top Bottom