Donald Trump arejea na mtandao wake

Donald Trump arejea na mtandao wake

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1645531761321.png

Picha: Chapisho la kwanza la Trump kwenye mtandao wake

Jukwaa la mtandao wa kijamii la Donald Trump, Truth Social limezinduliwa,kwa kiasi kidogo kwenye Apple App store nchini Marekani.

Wachambuzi wamebaini kuwa programu hiyo inafanana na Twitter. Bw Trump alipigwa marufuku kutoka Twitter, Facebook na YouTube mwaka jana.

Na watumiaji wengine wa mapema walikuwa na shida kusajili akaunti.

Kiongozi wa mradi na mbunge wa zamani Devin Nunes alisema unatarajiwa kufanya kazi kikamilifu mwishoni mwa Machi.

Baadhi ya wale wanaojaribu kujiandikisha walikuwa wameambiwa: "Kwa sababu ya mahitaji makubwa, tumekuweka kwenye orodha yetu ya wanaosubiri," shirika la habari la Reuters liliripoti.

Imeundwa na kampuni ya Trump Media & Technology Group (TMTG), Truth Social hapo awali ilitolewa kwa watumiaji wapatao 500 wanaojaribu beta.

Wiki iliyopita, Donald Trump Jr aliweka mtandaoni picha ya skrini ya "ukweli" wa kwanza wa baba yake kwenye mtandao wa kijamii: "Jitayarishe. Rais wako unayempenda atakuona hivi karibuni." Aliandika .
 
View attachment 2127362
Picha: Chapisho la kwanza la Trump kwenye mtandao wake

Jukwaa la mtandao wa kijamii la Donald Trump, Truth Social limezinduliwa,kwa kiasi kidogo kwenye Apple App store nchini Marekani.

Wachambuzi wamebaini kuwa programu hiyo inafanana na Twitter. Bw Trump alipigwa marufuku kutoka Twitter, Facebook na YouTube mwaka jana.

Na watumiaji wengine wa mapema walikuwa na shida kusajili akaunti.

Kiongozi wa mradi na mbunge wa zamani Devin Nunes alisema unatarajiwa kufanya kazi kikamilifu mwishoni mwa Machi.

Baadhi ya wale wanaojaribu kujiandikisha walikuwa wameambiwa: "Kwa sababu ya mahitaji makubwa, tumekuweka kwenye orodha yetu ya wanaosubiri," shirika la habari la Reuters liliripoti.

Imeundwa na kampuni ya Trump Media & Technology Group (TMTG), Truth Social hapo awali ilitolewa kwa watumiaji wapatao 500 wanaojaribu beta.

Wiki iliyopita, Donald Trump Jr aliweka mtandaoni picha ya skrini ya "ukweli" wa kwanza wa baba yake kwenye mtandao wa kijamii: "Jitayarishe. Rais wako unayempenda atakuona hivi karibuni." Aliandika .
Kugombana na tajiri mkubwa ndiyo matokeo yake haya.Unamtishia kitu ambacho yeye ana uwezo nacho,unatarajia nini?
 
Back
Top Bottom