Dondoo za hatua za kupata hati ya umiliki wa ardhi hapa Tanzania kwa mwaka 2022

Kuna hasara gani kufatilia hati miliki ukiwa peke ako
Changamoto kubwa kufuatilia Hati mwenyewe ni kupoteza muda mwingi coz ili mchakato wa Hati ukamilike ni lazima
• Eneo Liwe limepimwa
•Eneo liwekwe beacons
•Town plan (ramani ya mipango mji) kutoka wizarani
•Mkataba wa mauziano
•Uhakiki wa mipaka na majirani

Sasa haya yote lazima ufanye kwa ushrikiano wa karibu na aliyekuuzia na majirani wa eneo ulilonunua,
Gharama za kulipia serikalini kwa kufanikisha mchakato wa Hati ni ndogo sana na inapanda au kupungua kutokana na ukubwa wa eneo lako au eneo kiwanja chako kilipo

•Note Usikubali kununua kiwanja kama hakija pimwa na hujaona Ramani ya mipango miji coz Kila eneo kwa Kila halimashauri Lina matumizi yake.
Jiridhishe eneo unalotaka kulinunua linendana na matumizi ya eneo husika ili kuepusha usumbufu hapo baadaye

Mfano Mimi kuna sehemu nashughulikia hati kwenye kiwanja changu nlilipa 71380 tuu, Lakini hiyo ni nje ya ile nliolipa kampuni ambayo iliniuzia kiwanja ili kunirahisishia mchakato mzima
 
Mleta mada naomba nipate namna ya kuwasiliana nawe
 
Asante kwa maelezo yako mazuri juu ya hili swala. Nina swali, kama utaweza kunisaidia, au mtu yeyote mwenye uelewa juu ya haya mambo. Je, utaratibu upoje kwenye kubadilisha majina ya mmiliki wa kiwanja kwenye hati?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…