Doto Magari atembelea mradi wake wa kufuga nguruwe wa million sabini Dodoma. Na kila nguruwe chakula kwa siku laki 3.

Doto Magari atembelea mradi wake wa kufuga nguruwe wa million sabini Dodoma. Na kila nguruwe chakula kwa siku laki 3.

Ila hawa wa piga kelele hawa! Mmmmh,
Cha ajabu huwezi kuwasikia watu kama Fernandez boss wa Nala, au, lady Jay d, au, boss wa jamii forum, au bakheresa wakijitapa kwa, ukwasi, wao,
Wanaojitqpa, ni hawa, hawa, Mara utasikia natumia 40 milioni kwa siku!
Kuna watu wana hela wanaogopa wake zao, ndugu zao hadi watoto wao wakijua.
 
Ingekuwa fresh kama angedadavua mchanganuo kidogo wa uwekezaji wake...

Maana huelewi hiyo Mil 70 kama imejumuisha gharama zote hadi ununuzi wa ardhi na mishahara ya wafanyakazi...
 
Ukija siku moja twende maili sita kwa mama mmoja anaitwa mama cam anao hao nguruwe nilisomaga kwake tukiwa tunaenda mashambani tunaenda kuwaona na hayo manguruwe yake
Sawa Mjukuu ila hakuna Nguruwe anakula chakula cha laki na 80 seuse laki 3 ya Dotto Magali

Kufanya Mradi wa gharama hiyo ni hasara

Chukulia huyo Nguruwe unamfuga hadi kumuuza akiwa na miezi 6

Miezi 6 ni sawa na Siku 180

Chukulia huyo Nguruwe wenu anakula chakula cha shilingi 180,000

Ina maana kujua atatumia kiasi gani cha Fedha hadi kumuuza itakuwa;
180x180,000 = 32,400,000

Iwapo utamuuza huyo Nguruwe wako shilingi milioni 5.

Utabaki na Faida ya HASI (32,400,000-5,000,000) ambayo ni shilingi 27,400,000

Je wewe kama mfanyabiashara utaendelea na hiyo biashara Mjukuu???
 
Hizo gharama amezitaja ili kuwatoa kwenye mjadala wa kufuga nguruwe huku akiwa ustadhi
Nguruwe mimi napakana nao na hata muda huu ninatype huku nasikia wakikoroma. Gharama za kumlisha mmoja sidhani hata sh. 2,000/= kwa siku jamaa huwa anatumia
 
Back
Top Bottom