Dotto Biteko, kwa nini suala la mgao wa umeme halifiki kikomo?

Dotto Biteko, kwa nini suala la mgao wa umeme halifiki kikomo?

Watumishi wengi wa umma ni wazembe wazembe na wezi wezi, bila usimamizi na uongozi wa kitemi na kibabe na baadaye kuweka mfumo wa kibabe utakaowasimamia tunakwama sana.

Tanesco pamoja na yote tunayoyaongelea sijui ukosefu wa umeme wa kutosha sijui miundo mbinu na blah blah nyingine LAKINI TATIZO KUUBWA KABISA NI WATUMISHI WENYE UWEZO MDOGO, AJIRA ZA KUJUANA JUANA, WATUMISHI WAZEMBEWAZEMBE NA WEZI WEZI.
Suluhu ni uongozi wa kibabe ambao hautacheka na kima zaidi ya ubabe ubabe wa watumishi wajingawajinga.
 
KIZIMKAZI YY ndio hajui chochote.YY ndio chanzo cha haya yote
 
Hii wizara ya nishati inatakiwa apewe uwaziri mtu aliyesomea mambo ya enginneer wa umeme na aliyefauru vizuri lakini kwa hawa wengine tutasulubika sana mfano
Mimi mashine zangu tatu zimesimama kisa umeme na mashine mbili ndo natumia generator
 
Yaani nashangaa umeme bado ni kero kubwa sana kwetu sisi wananchi wa Tanzania.
Tuliaminishwa kwamba kijana huyu mheshimiwa Waziri Biteko akiingia mgawo wa umeme utakuwa historia lakini mpaka muda huu bado ni bila bila.

Umeme kukatika hovyo hovyo Tanzania imekuwa ni kero isiyopata suluhisho la kudumu.
Wananchi tunaunguza vifaa vya umeme, biashara za watu zinazoitaji umeme wa uhakika zinaharibika pasipo fidia yoyote kutoka TANESCO.

Lakini jambo la kujiuliza ilikuwaje Waziri Kalemani akaweza hii wizara ya Nishati mpaka suala la mgao wa umeme kutokuwepo likadhibitiwa huku umeme vijijini ulikuwa ukipelekwa kwa spidi kubwa na kwa bei ndogo tu ya shs 27,000? Kwa hapa Mh. Kelemani chini ya uongozi wa hayati JPM tutawapa heshima yenu siku zote.

Turudi kwenye mada,
Inakuwaje Dotto Biteko pamoja na cheo kingine kikubwa cha Naibu waziri mkuu mbona kama vile hivyo vyeo havina mtu.
Umeme bado ni jambo linalotutesa sana sisi wananchi wa taifa hili.
CCM ni chama tawala Tanzania chenye miaka zaidi ya 60 ya kutawala Tanzania (CCM ni TANU kilichobadili jina tu) inakuwaje hampo serious katika kuwezesha suala la upatikanaji wa umeme Tanzania?

Katika comment yangu nikichangia katika uzi wa Ipi siri ya nchi ndogo ya Korea Kusini kuzalisha umeme mwingi wa Gigawatts 143?
Nili comment kwamba Hakuna nchi inaweza kuendelea pasipo uhakika wa upatikanaji wa umeme. Ukuaji wa nchi unategemea ukuaji wa viwanda, ukuaji wa viwanda unategemea umeme wa uhakika.
Hiyo comment ilileta likes zaidi ya 20 hii ni kuonesha namna gani watanzania walivyo aware na masuala ya umeme na wanjua umuhimu wa umeme wa uhakika katika kuchochea uanzishwaji na uzalishaji mkubwa viwandani na hivyo uchumi wa nchi kwa ujumla kukua kwa sababu tu ya umeme wa uhakika.

Kuna tetesi kwamba katika mabwawa yetu ya umeme kuna kipindi waziri kipara aliwahi kuamuru maji ya mto yasielekezwe bwawani ili maji yasijae bwawani lakini pia jambo la kushangaza pamoja na mvua nyingi hivi bado kuna uhaba wa maji katika mabwawa yetu ya umeme. Nini kipo nyuma ya mgawo mkubwa huu wa umeme chini Tanzania?
Lakini pia huu si ni uhujumu uchumi wa nchi?
Kwa nini Dotto Biteko usitoke nje ya hadhara useme nini kipo nyuma na hujuma zilizoko huko TANESCO zinazofanya umeme kuwa wa mgao husioisha nchini Tanzania?
Kwa nini Dotto Biteko usiangushe mbuyu chini? kama makambas na maharagwe waliacha mifumo na mikataba mibovu huko TANESCO kwa ajili ya kujinufaisha wao na familia zao kwa nini usilipue hiyo mifumo ili kulinda nafasi zako huko mbeleni?

Viongozi kutojituma kutatua kero za wananchi na kutumia nafasi mlizozipata kula rushwa na kuuza nchi kifisadi ndo maana sisi wananchi tunawaombea mabaya yawapate ninyi na familia zenu. Mtafanikiwa kuiba mali za watanzania lakini kamwe furaha na amani haitakuwa sehemu za maisha yenu.
Moto wa Kalemani wanaujua madereva wake.
Kwake ilikuwa kazi kazi, muda wa kula kiyoyozi ofisini alikuwa hana.
Na alikuwa na maamuzi ya kutekelezeka.
Hawa wengine ni mawaziri wa media.
 
Moto wa Kalemani wanaujua madereva wake.
Kwake ilikuwa kazi kazi, muda wa kula kiyoyozi ofisini alikuwa hana.
Na alikuwa na maamuzi ya kutekelezeka.
Hawa wengine ni mawaziri wa media.
Kwa kweli ukiwa mtumishi mchapa kazi legency yako haifutiki
 
Back
Top Bottom