blance86
JF-Expert Member
- Aug 31, 2016
- 2,138
- 5,632
Kwenye hili la Chanjo, Rais Samia alikwama kimkakati.
Na Dotto Bulendu(MwanaPuge),nikiandika kutoka kijijini Puge.
:::::::::::::
Vita ya hoja juu ya Ugonjwa wa Corona nchini kati ya Ndugu wawili ,Dr Doroth Gwajima (MB) na Waziri wa Afya dhidi ya Shemeji yake Askofu Josephat Gwajima (Mb) zimevuka mipaka Sasa hakuna hoja ni vijembe ,kebehi ,kudhalilishana na kuvua a nguo.
Askofu Dr Josephat Gwajima ana hoja zake za msingi ambazo Serikali ilitakiwa izitolee ufafanuzi Ili kuondoa hofu kubwa ambayo imetengenezwa Na Serikali Yeye.
Leo ukienda mtaani watanzania wapo njia panda kuhusu uwepo ama kutokuwepo Kwa Ugonjwa wa UVIKO-19,na Kama Chanjo dhidi ya UVIKO-19 ni Salama ama si Salama.
Watanzania wamekuwa njia panda Maana ni Serikali hii hii,Viongozi hawahawa Mwaka huu walizunguka kila kona ya nchi hii,wakasambaa Kwenye kila aina ya chombo cha Habari Na kuuambia umma Kuwa Tanzania hakuna Corona,hata watu walipoanza kufariki wao walisema hakuna Corona,watu walipougua walisema hakuna Corona bali kuna Changamoto ya kupumua.
Dunia ilipoleta Chanjo,Viongozi hawahawa,Mwaka Huu Huu waliwaambia wananchi kataeni Chanjo Maana imepandikizwa Vitu vibaya vyenye madhara Kwa wananchi Na hasa Waafrika.
Watanzania hawahawa ambao wamechanjwa Ndui,Homa ya manjano,Pepopunda ,Polio,Tetanasi Na zote zimetoka huko Ulaya,Marekani Na Asia wakalielewa vizuri somo kuhusu Chanjo Na wakasusia kila kitu kuhusu Chanjo.
Watanzania hawahawa ambao wakipata maambukizi ya Virusi vya UKIMWI wanameza ARV za msaada kutoka Marekani,wadada wakipata Ujauzito wanameza P2 za Mabeberu wakalielewa somo la wivu wa watu wa Magharibi Kuwa wamepandikiza Sumu Kwenye Chanjo za Corona Na Sasa wamezikataa.
Toka UVIKO ufumuke Mpaka mwezi wa Tatu Mwaka huu,ni viongozi hawahawa waliwaambia wananchi hakuna Corona,Chanjo ni Sumu,leo wamegeuka Na kuwaambia wananchi Corona ipo,Chanjo ni Salama tena wanawaambia kawaida.
Kampeni dhidi ya Chanjo Na Corona awamu ya kwanza chini ya Rais Magufuli ilipigwa Na Serikali nzima chini ya Raisi Magufuli mwenyewe lakini kampeni ya Sasa ya kukiri Corona ipo Na Chanjo itumike inapigwa na Waziri Gwajima pekee yake ,hii ni ishara Kuwa Samia Yupo peke yake katika hili wakati mtangulizi wake alikuwa Na watu nyuma wa kumsaidia kufanya kampeni za kusema hakuna Corona.
Rais Samia hatafanikiwa kubadili fikra za watanzania hata Kama atawakamata wote wanaopingana Na msimamo wa Serikali yake Kwani Serikali yake imeshawavuruga wananchi.
Doroth Na Mollel ndiyo walikuwa Vinara wa nyungu,Na kusema hakuna Corona leo wageuke kusema Corona ipo Na Chanjo ni Salama,hakuna wa kumuelewa Maana Watanzania siyo miti,ni watu wenye akili zao timamu.
Askofu Gwajima Kwa kifupi ana hoja nzito,na Bahati nzuri hoja zake zote za kisayansi zimejibiwa Na wanasayansi labda Kama nae Askofu Gwajima hataki kusikiliza hao wanasayansi.
Binafsi nimesikia Hoja za Askofu Gwajima zikijibiwa vizuri Na Dr Mwele Malecela kuhusu muda wa utafiti wa Chanjo,hoja ya damu kuganda ilijibiwa vizuri Na Prof Janabi,hoja ya watu kuchanjwa Na kupata maambukizi imejibiwa vizuri na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza pamoja Na Dr Derick wa Tanzanite Hospital kupitia Vyombo vya Habari .
Tatizo kubwa naloliona walewale walioendesha propaganda za Kuwa Hakuna Corona leo wanaongoza propaganda za Kuwa kuna Corona Na Chanjo ni salama .
Hoja za Askofu Gwajima ndiyo Hoja za wananchi huku nje,zijibiwe kisayansi na Mara Kwa Mara!maana Hoja za Kuwa Corona haipo,Chanjo siyo Salama haiwezi kujibiwa Siku Moja kupitia TBC ikafuta imani iliyopandikizwa kichwani mwa wananchi Kwa muda wa Mwaka mmoja Na Serikali hii hii na watu hawahawa.
Samia Kama anataka kuaminika Kwenye hili,Yeye binafsi awe kinara wa kutoa elimu,wasaidizi wake wawe Vinara Maana Sasa kaachwa Doroth Gwajima pekee tofauti Na wakati wa Magufuli.
Kitu cha mwisho,CCM kaeni Na Askofu Gwajima zungumzeni nae,tuhuma anazozitoa Kuwa Serikali imehongwa Ili ipokee chanjo ni tuhuma nzito.
Askofu Gwajima anataka kumaanisha Rais Samia kahongwa Ili kuwauwa Watanzania?kwamba Samia kahongwa ili 2025 watanzania wote wawe wamekufa?hizi ni tuhuma nzito.
Tuhuma hizi pekee ni hoja binafsi Bungeni kuwa Mbunge ka mtuhumu Rais kuhongwa Ili aangamize watu wake.
Tuhuma za Serikali(Rais)kuhongwa ni tuhuma nzito kuliko tuhuma ya aina yeyote,kumtuhumu Rais kuhongwa tena Ili watu wafe ni tuhuma mbaya Na nzito.
Naamini kikao kijacho cha Bunge,wabunge waihoji serikali kuhusu tuhuma hizi nzito zilizotolewa Na Mbunge Kuwa Serikali imehongwa.
Hizi ni tuhuma nzito kuliko tuhuma yeyote Kwa Serikali na Chama Tawala.
Kwa sasa dhana ya Uwajibikaji wa pamoja ambayo ilikuwepo wakati wa Serikali ya Rais Magufuli ilikuwepo wakati wa janga la Corona,Ila Kwa Sasa hakuna dhana ya uwajibikaji wa Pamoja!Katika Corona!CCM Na Serikali hawapo pamoja kila mtu Na msimamo wake.
Gharama za Kuwa sehemu ya taasisi ni kuwajibika pamoja,Kama huwezi kuiishi dhana ya uwajibikaji wa pamoja unanshauriwa usiwe sehemu ya Serikali.
Na Dotto Bulendu(MwanaPuge),nikiandika kutoka kijijini Puge.
:::::::::::::
Vita ya hoja juu ya Ugonjwa wa Corona nchini kati ya Ndugu wawili ,Dr Doroth Gwajima (MB) na Waziri wa Afya dhidi ya Shemeji yake Askofu Josephat Gwajima (Mb) zimevuka mipaka Sasa hakuna hoja ni vijembe ,kebehi ,kudhalilishana na kuvua a nguo.
Askofu Dr Josephat Gwajima ana hoja zake za msingi ambazo Serikali ilitakiwa izitolee ufafanuzi Ili kuondoa hofu kubwa ambayo imetengenezwa Na Serikali Yeye.
Leo ukienda mtaani watanzania wapo njia panda kuhusu uwepo ama kutokuwepo Kwa Ugonjwa wa UVIKO-19,na Kama Chanjo dhidi ya UVIKO-19 ni Salama ama si Salama.
Watanzania wamekuwa njia panda Maana ni Serikali hii hii,Viongozi hawahawa Mwaka huu walizunguka kila kona ya nchi hii,wakasambaa Kwenye kila aina ya chombo cha Habari Na kuuambia umma Kuwa Tanzania hakuna Corona,hata watu walipoanza kufariki wao walisema hakuna Corona,watu walipougua walisema hakuna Corona bali kuna Changamoto ya kupumua.
Dunia ilipoleta Chanjo,Viongozi hawahawa,Mwaka Huu Huu waliwaambia wananchi kataeni Chanjo Maana imepandikizwa Vitu vibaya vyenye madhara Kwa wananchi Na hasa Waafrika.
Watanzania hawahawa ambao wamechanjwa Ndui,Homa ya manjano,Pepopunda ,Polio,Tetanasi Na zote zimetoka huko Ulaya,Marekani Na Asia wakalielewa vizuri somo kuhusu Chanjo Na wakasusia kila kitu kuhusu Chanjo.
Watanzania hawahawa ambao wakipata maambukizi ya Virusi vya UKIMWI wanameza ARV za msaada kutoka Marekani,wadada wakipata Ujauzito wanameza P2 za Mabeberu wakalielewa somo la wivu wa watu wa Magharibi Kuwa wamepandikiza Sumu Kwenye Chanjo za Corona Na Sasa wamezikataa.
Toka UVIKO ufumuke Mpaka mwezi wa Tatu Mwaka huu,ni viongozi hawahawa waliwaambia wananchi hakuna Corona,Chanjo ni Sumu,leo wamegeuka Na kuwaambia wananchi Corona ipo,Chanjo ni Salama tena wanawaambia kawaida.
Kampeni dhidi ya Chanjo Na Corona awamu ya kwanza chini ya Rais Magufuli ilipigwa Na Serikali nzima chini ya Raisi Magufuli mwenyewe lakini kampeni ya Sasa ya kukiri Corona ipo Na Chanjo itumike inapigwa na Waziri Gwajima pekee yake ,hii ni ishara Kuwa Samia Yupo peke yake katika hili wakati mtangulizi wake alikuwa Na watu nyuma wa kumsaidia kufanya kampeni za kusema hakuna Corona.
Rais Samia hatafanikiwa kubadili fikra za watanzania hata Kama atawakamata wote wanaopingana Na msimamo wa Serikali yake Kwani Serikali yake imeshawavuruga wananchi.
Doroth Na Mollel ndiyo walikuwa Vinara wa nyungu,Na kusema hakuna Corona leo wageuke kusema Corona ipo Na Chanjo ni Salama,hakuna wa kumuelewa Maana Watanzania siyo miti,ni watu wenye akili zao timamu.
Askofu Gwajima Kwa kifupi ana hoja nzito,na Bahati nzuri hoja zake zote za kisayansi zimejibiwa Na wanasayansi labda Kama nae Askofu Gwajima hataki kusikiliza hao wanasayansi.
Binafsi nimesikia Hoja za Askofu Gwajima zikijibiwa vizuri Na Dr Mwele Malecela kuhusu muda wa utafiti wa Chanjo,hoja ya damu kuganda ilijibiwa vizuri Na Prof Janabi,hoja ya watu kuchanjwa Na kupata maambukizi imejibiwa vizuri na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza pamoja Na Dr Derick wa Tanzanite Hospital kupitia Vyombo vya Habari .
Tatizo kubwa naloliona walewale walioendesha propaganda za Kuwa Hakuna Corona leo wanaongoza propaganda za Kuwa kuna Corona Na Chanjo ni salama .
Hoja za Askofu Gwajima ndiyo Hoja za wananchi huku nje,zijibiwe kisayansi na Mara Kwa Mara!maana Hoja za Kuwa Corona haipo,Chanjo siyo Salama haiwezi kujibiwa Siku Moja kupitia TBC ikafuta imani iliyopandikizwa kichwani mwa wananchi Kwa muda wa Mwaka mmoja Na Serikali hii hii na watu hawahawa.
Samia Kama anataka kuaminika Kwenye hili,Yeye binafsi awe kinara wa kutoa elimu,wasaidizi wake wawe Vinara Maana Sasa kaachwa Doroth Gwajima pekee tofauti Na wakati wa Magufuli.
Kitu cha mwisho,CCM kaeni Na Askofu Gwajima zungumzeni nae,tuhuma anazozitoa Kuwa Serikali imehongwa Ili ipokee chanjo ni tuhuma nzito.
Askofu Gwajima anataka kumaanisha Rais Samia kahongwa Ili kuwauwa Watanzania?kwamba Samia kahongwa ili 2025 watanzania wote wawe wamekufa?hizi ni tuhuma nzito.
Tuhuma hizi pekee ni hoja binafsi Bungeni kuwa Mbunge ka mtuhumu Rais kuhongwa Ili aangamize watu wake.
Tuhuma za Serikali(Rais)kuhongwa ni tuhuma nzito kuliko tuhuma ya aina yeyote,kumtuhumu Rais kuhongwa tena Ili watu wafe ni tuhuma mbaya Na nzito.
Naamini kikao kijacho cha Bunge,wabunge waihoji serikali kuhusu tuhuma hizi nzito zilizotolewa Na Mbunge Kuwa Serikali imehongwa.
Hizi ni tuhuma nzito kuliko tuhuma yeyote Kwa Serikali na Chama Tawala.
Kwa sasa dhana ya Uwajibikaji wa pamoja ambayo ilikuwepo wakati wa Serikali ya Rais Magufuli ilikuwepo wakati wa janga la Corona,Ila Kwa Sasa hakuna dhana ya uwajibikaji wa Pamoja!Katika Corona!CCM Na Serikali hawapo pamoja kila mtu Na msimamo wake.
Gharama za Kuwa sehemu ya taasisi ni kuwajibika pamoja,Kama huwezi kuiishi dhana ya uwajibikaji wa pamoja unanshauriwa usiwe sehemu ya Serikali.