#COVID19 Dotto Bulendu: Kwenye hili la chanjo, Rais Samia alikwama kimkakati

#COVID19 Dotto Bulendu: Kwenye hili la chanjo, Rais Samia alikwama kimkakati

Mashabiki vijana kwa wazee wanaingia uwanjani,nimeona jana kwenye super cup Dortmund vs Munich!

Hata data zinaonesha vifo vimepungua sana Ulaya baada ya chanjo!Kuna daktari mmoja bingwa wa mfumo wa upumuaji, ni mtanzania anayeishi USA alieleza namna chanjo inavyowasaidia watu kupambana na Corona na akaeleza kuwa waliochanjwa wengi hawawi Critical wanapopata maambukizi!

Tusiwe wabishi wa asili,tuangalie facts
MwanaJF mmoja kajibu hivi
Screenshot_20210818-090305.jpg
 
Ni kweli wamekuwa vigeugeu!Lakini turudi kwenye uhalisia, kipindi cha mwendazake waliendeshwa na wao wakakubali kuweka taaluma zao pembeni!

Si wakati wa kunyoosheana vidole kuwa wewe ulisema hiki juzi,ni walati wa kuangalia tunavukaje!
Je,chanjo inasaidia?


Siyo rahisi kiivyo!
Labda wawajibike/wawajibishwe zije sura mpya yamkini watakapokuja kutoa hamasa na elimu pengine wataweza kueleweka!

Lakini kwa watu walewale kuwa na ndimi mbili kiukweli inachanganya wananchi wengi!
 
Ilifika mahala hata kutamka neno ugonjwa wa Corona ilikuwa kama kufanya kosa !

Eti ikabidi isemwe changamoto zakupumua ! Imagine! [emoji15][emoji15]

Barakoa ikasemwa si salama ikibidi watu wavae za kushona na top officials walikuwa hawavai kabisa !

Gafla kimekuja kiswahili kingine tofauti kabisa, Je hapo wananchi washike lipi?! Lile u hili? Kwanini labda?!
 
Hiyo 3% ni kubwa mno wala haiwezi kufikiwa!! Tuko 60,000,000 kwa hiyo 3% ni watu 1,800,000!! Mpaka leo hizo dozi 1,000,000 za chanjo bado zimedoda!! Watu wameshachanganya akili za kuambiwa na za kwao halafu wanawacheki tu!! Nani wa kumsikiliza yule Dr gwaji mtaalamu wa mipasho na kudelemka?
Hakuna zababu za msingi za kuchanjwa hadi sasa. Ni porojo porojo tu za wanasiasa na wataalamu wetu wa afya ambao pia wanadai chanjo ni bora na salama kwa kuambiwa. WHO pia imetoa kibali cha dharura (EUA) cha matumizi ya baadhi ya hizo chanjo. Watengenezaji wa chanjo nao wanakiri kuwa bado wako kwenye maabara wakifuatilia matokeo ya chanjo zao.

Tanzania UVIKO-19 imekuwa ikitibika kwa dawa mbadala km nyungu. Dawa hizo pia zimetumika na kuendelea kutumika kama kinga ikiwa ni pamoja na kuzingatia kanuni za kujikinga dhidi ya maambukizi.

Pamoja na wimbi jipya (variants) la UVIKO-19, Watanzania wanaendelea na maisha yao kama kawa. Wanaosemekana wamekufa kutokana UVIKO-19 nchini (wengi wao wenye uwezo kifedha na madaraka), wataalamu hawathibitishi ukweli huo bali hisia za watu, kama wakati wa mwanzo wa UKIMWI.

Katika mazingira hayo hakuna shaka WaTz wengi hawatachanja. Ukweli tayari umejidhihirisha kwa chanjo ya awamu ya kwanza (1m) hadi sasa hajaisha. Hata watumishi wa huduma ya afya (madaktari na wauguzi wapatao zaidi ya milioni) wamesita kuchanjwa.
 
Kwenye hili la Chanjo, Rais Samia alikwama kimkakati.

Na Dotto Bulendu(MwanaPuge),nikiandika kutoka kijijini Puge.
:::::::::::::
Vita ya hoja juu ya Ugonjwa wa Corona nchini kati ya Ndugu wawili ,Dr Doroth Gwajima (MB) na Waziri wa Afya dhidi ya Shemeji yake Askofu Josephat Gwajima (Mb) zimevuka mipaka Sasa hakuna hoja ni vijembe ,kebehi ,kudhalilishana na kuvua a nguo.

Askofu Dr Josephat Gwajima ana hoja zake za msingi ambazo Serikali ilitakiwa izitolee ufafanuzi Ili kuondoa hofu kubwa ambayo imetengenezwa Na Serikali Yeye.

Leo ukienda mtaani watanzania wapo njia panda kuhusu uwepo ama kutokuwepo Kwa Ugonjwa wa UVIKO-19,na Kama Chanjo dhidi ya UVIKO-19 ni Salama ama si Salama.

Watanzania wamekuwa njia panda Maana ni Serikali hii hii,Viongozi hawahawa Mwaka huu walizunguka kila kona ya nchi hii,wakasambaa Kwenye kila aina ya chombo cha Habari Na kuuambia umma Kuwa Tanzania hakuna Corona,hata watu walipoanza kufariki wao walisema hakuna Corona,watu walipougua walisema hakuna Corona bali kuna Changamoto ya kupumua.

Dunia ilipoleta Chanjo,Viongozi hawahawa,Mwaka Huu Huu waliwaambia wananchi kataeni Chanjo Maana imepandikizwa Vitu vibaya vyenye madhara Kwa wananchi Na hasa Waafrika.

Watanzania hawahawa ambao wamechanjwa Ndui,Homa ya manjano,Pepopunda ,Polio,Tetanasi Na zote zimetoka huko Ulaya,Marekani Na Asia wakalielewa vizuri somo kuhusu Chanjo Na wakasusia kila kitu kuhusu Chanjo.

Watanzania hawahawa ambao wakipata maambukizi ya Virusi vya UKIMWI wanameza ARV za msaada kutoka Marekani,wadada wakipata Ujauzito wanameza P2 za Mabeberu wakalielewa somo la wivu wa watu wa Magharibi Kuwa wamepandikiza Sumu Kwenye Chanjo za Corona Na Sasa wamezikataa.

Toka UVIKO ufumuke Mpaka mwezi wa Tatu Mwaka huu,ni viongozi hawahawa waliwaambia wananchi hakuna Corona,Chanjo ni Sumu,leo wamegeuka Na kuwaambia wananchi Corona ipo,Chanjo ni Salama tena wanawaambia kawaida.

Kampeni dhidi ya Chanjo Na Corona awamu ya kwanza chini ya Rais Magufuli ilipigwa Na Serikali nzima chini ya Raisi Magufuli mwenyewe lakini kampeni ya Sasa ya kukiri Corona ipo Na Chanjo itumike inapigwa na Waziri Gwajima pekee yake ,hii ni ishara Kuwa Samia Yupo peke yake katika hili wakati mtangulizi wake alikuwa Na watu nyuma wa kumsaidia kufanya kampeni za kusema hakuna Corona.

Rais Samia hatafanikiwa kubadili fikra za watanzania hata Kama atawakamata wote wanaopingana Na msimamo wa Serikali yake Kwani Serikali yake imeshawavuruga wananchi.

Doroth Na Mollel ndiyo walikuwa Vinara wa nyungu,Na kusema hakuna Corona leo wageuke kusema Corona ipo Na Chanjo ni Salama,hakuna wa kumuelewa Maana Watanzania siyo miti,ni watu wenye akili zao timamu.

Askofu Gwajima Kwa kifupi ana hoja nzito,na Bahati nzuri hoja zake zote za kisayansi zimejibiwa Na wanasayansi labda Kama nae Askofu Gwajima hataki kusikiliza hao wanasayansi.

Binafsi nimesikia Hoja za Askofu Gwajima zikijibiwa vizuri Na Dr Mwele Malecela kuhusu muda wa utafiti wa Chanjo,hoja ya damu kuganda ilijibiwa vizuri Na Prof Janabi,hoja ya watu kuchanjwa Na kupata maambukizi imejibiwa vizuri na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza pamoja Na Dr Derick wa Tanzanite Hospital kupitia Vyombo vya Habari .

Tatizo kubwa naloliona walewale walioendesha propaganda za Kuwa Hakuna Corona leo wanaongoza propaganda za Kuwa kuna Corona Na Chanjo ni salama .

Hoja za Askofu Gwajima ndiyo Hoja za wananchi huku nje,zijibiwe kisayansi na Mara Kwa Mara!maana Hoja za Kuwa Corona haipo,Chanjo siyo Salama haiwezi kujibiwa Siku Moja kupitia TBC ikafuta imani iliyopandikizwa kichwani mwa wananchi Kwa muda wa Mwaka mmoja Na Serikali hii hii na watu hawahawa.

Samia Kama anataka kuaminika Kwenye hili,Yeye binafsi awe kinara wa kutoa elimu,wasaidizi wake wawe Vinara Maana Sasa kaachwa Doroth Gwajima pekee tofauti Na wakati wa Magufuli.

Kitu cha mwisho,CCM kaeni Na Askofu Gwajima zungumzeni nae,tuhuma anazozitoa Kuwa Serikali imehongwa Ili ipokee chanjo ni tuhuma nzito.

Askofu Gwajima anataka kumaanisha Rais Samia kahongwa Ili kuwauwa Watanzania?kwamba Samia kahongwa ili 2025 watanzania wote wawe wamekufa?hizi ni tuhuma nzito.

Tuhuma hizi pekee ni hoja binafsi Bungeni kuwa Mbunge ka mtuhumu Rais kuhongwa Ili aangamize watu wake.

Tuhuma za Serikali(Rais)kuhongwa ni tuhuma nzito kuliko tuhuma ya aina yeyote,kumtuhumu Rais kuhongwa tena Ili watu wafe ni tuhuma mbaya Na nzito.

Naamini kikao kijacho cha Bunge,wabunge waihoji serikali kuhusu tuhuma hizi nzito zilizotolewa Na Mbunge Kuwa Serikali imehongwa.

Hizi ni tuhuma nzito kuliko tuhuma yeyote Kwa Serikali na Chama Tawala.

Kwa sasa dhana ya Uwajibikaji wa pamoja ambayo ilikuwepo wakati wa Serikali ya Rais Magufuli ilikuwepo wakati wa janga la Corona,Ila Kwa Sasa hakuna dhana ya uwajibikaji wa Pamoja!Katika Corona!CCM Na Serikali hawapo pamoja kila mtu Na msimamo wake.

Gharama za Kuwa sehemu ya taasisi ni kuwajibika pamoja,Kama huwezi kuiishi dhana ya uwajibikaji wa pamoja unanshauriwa usiwe sehemu ya Serikali.
Hili mambo yaende sawa, sirikali ikawabananishe Maaskofu wa Katoriki pamoja na Mashehe wa Bakwata, waandike waraka kwa waumini wao kuwa hawataruhusiwa kuingia kanisani au msikitini kama haujachanjwa. Hii itawafanya wananchi wachanje fasta. Ndani ya wiki tuu hizo dawa zote zitakuwa chache. Maana huu mziki unaonekana kama ni one woman show.
 
Tatizo liko wapi? Waliochanjwa wako salama, kwa nini wanataka kuwalazimisha wasio chanjwa? Waliochanjwa waendelee kula kuku kwa mrija wafaidi matunda ya ulimwengu kwa miongo kadhaa waachane na wasiochanjwa.
 
Hata mm nawaona Samia, waziri wa afya na naibu wake kama kituko. Hasa wanapo ongelea kuhusu chanjo ya korona.

Walisema korona haipo nchini lkn Sasa wanasema ipo. Hili linasameheka, maana yawezekana korona imeingia hivi karibuni.

Lkn walisema chanjo ni njama ya mabeberu kuangamiza waafrika. Sasa wanasema tuchanjwe. Kwa hili kamwe hawasameheki na ndiyo kikwazo kikubwa cha ubishani na mgomo wa watanzania kuchanjwa.
Madai ya Askofu Gwajima ni kuwa chanjo ni njia ya kumdhibiti (control) aliyechanjwa. Kujichanganya kwa Waziri wa Afya na Naibu wake kila siku yawezekana ni kutokana na kuchanjwa (dalili za awali). Yajayo kwa waliochanjwa watajiju
 
Siyo rahisi kiivyo!
Labda wawajibike/wawajibishwe zije sura mpya yamkini watakapokuja kutoa hamasa na elimu pengine wataweza kueleweka!

Lakini kwa watu walewale kuwa na ndimi mbili kiukweli inachanganya wananchi wengi!
Mimi binafsi sikuwaunga mkono walati wanahimiza nyungu na kukandia chanjo,nilijua walikuwa wanaangalia boss wao anaenda kwa gia ipi!
Binafsi naiamini WHO na ndio maana nimechanja tayari!
Ambao watataka waje wabembelezwe sawa wasubiri,ningeliwa mimi wala hata nisingehamasisha!
Ningesema tu serikali imejiridhisha kuwa chanjo inaongeza kinga,anayetaka kuchanja ajiandikishe,asiyetaka aache!Maisha yaendelee!
 
Hili mambo yaende sawa, sirikali ikawabananishe Maaskofu wa Katoriki pamoja na Mashehe wa Bakwata, waandike waraka kwa waumini wao kuwa hawataruhusiwa kuingia kanisani au msikitini kama haujachanjwa. Hii itawafanya wananchi wachanje fasta. Ndani ya wiki tuu hizo dawa zote zitakuwa chache. Maana huu mziki unaonekana kama ni one woman show.


Kwanini mnapenda ku-force mambo ?
Kwanini mnapenda ubabe?

Kwanini njia ya hamasa na elimu isitumike kuliko vitisho?

Je wakiamua kutokwenda kusali huko makanisani na misikitini ? Wakaamua kusali majumbani?!

Tena siku hizi kuna global church services hata kwenye simu ya kiganjani kunaweza kufuatilia Ibada mubashara
 
Kabla ya kuanza na mkakati mpya, ili kutoa sintofahamu zilizotangulia ilibidi viongozi wote walioshiriki kwenye (kampeni) mikakati ya Nyungu & anti chanjo, maombi ya kitaifa - wote angewapiga chini ili sasa aanze na watu wapya kutangaza upya Chanjo, maombi hayaondoi ungonjwa sababu ugonjwa ni sayansi na si wa kiroho, Nyungu haijawahi kuua virus..

sasa hapa ndipo kwenye tatizo, wale wale waliotuambia Nyunguuu pigeni nyunguuu wale wale, chanjo si nzuri, maombi maombi ndiyo hawa hawa leo wanatuambia na kutuambia opposite side of it.
 
Watanzania hawa hawa waliokuwa wanampinga Magufuli kwa kuamini Corona itaondolewa na maombi, ndio hawa hawa wanaopinga chanjo ya Corona sasa hivi.
Very confusing
 
Kwenye hili la Chanjo, Rais Samia alikwama kimkakati.

Na Dotto Bulendu(MwanaPuge),nikiandika kutoka kijijini Puge.
:::::::::::::
Vita ya hoja juu ya Ugonjwa wa Corona nchini kati ya Ndugu wawili ,Dr Doroth Gwajima (MB) na Waziri wa Afya dhidi ya Shemeji yake Askofu Josephat Gwajima (Mb) zimevuka mipaka Sasa hakuna hoja ni vijembe ,kebehi ,kudhalilishana na kuvua a nguo.

Askofu Dr Josephat Gwajima ana hoja zake za msingi ambazo Serikali ilitakiwa izitolee ufafanuzi Ili kuondoa hofu kubwa ambayo imetengenezwa Na Serikali Yeye.

Leo ukienda mtaani watanzania wapo njia panda kuhusu uwepo ama kutokuwepo Kwa Ugonjwa wa UVIKO-19,na Kama Chanjo dhidi ya UVIKO-19 ni Salama ama si Salama.

Watanzania wamekuwa njia panda Maana ni Serikali hii hii,Viongozi hawahawa Mwaka huu walizunguka kila kona ya nchi hii,wakasambaa Kwenye kila aina ya chombo cha Habari Na kuuambia umma Kuwa Tanzania hakuna Corona,hata watu walipoanza kufariki wao walisema hakuna Corona,watu walipougua walisema hakuna Corona bali kuna Changamoto ya kupumua.

Dunia ilipoleta Chanjo,Viongozi hawahawa,Mwaka Huu Huu waliwaambia wananchi kataeni Chanjo Maana imepandikizwa Vitu vibaya vyenye madhara Kwa wananchi Na hasa Waafrika.

Watanzania hawahawa ambao wamechanjwa Ndui,Homa ya manjano,Pepopunda ,Polio,Tetanasi Na zote zimetoka huko Ulaya,Marekani Na Asia wakalielewa vizuri somo kuhusu Chanjo Na wakasusia kila kitu kuhusu Chanjo.

Watanzania hawahawa ambao wakipata maambukizi ya Virusi vya UKIMWI wanameza ARV za msaada kutoka Marekani,wadada wakipata Ujauzito wanameza P2 za Mabeberu wakalielewa somo la wivu wa watu wa Magharibi Kuwa wamepandikiza Sumu Kwenye Chanjo za Corona Na Sasa wamezikataa.

Toka UVIKO ufumuke Mpaka mwezi wa Tatu Mwaka huu,ni viongozi hawahawa waliwaambia wananchi hakuna Corona,Chanjo ni Sumu,leo wamegeuka Na kuwaambia wananchi Corona ipo,Chanjo ni Salama tena wanawaambia kawaida.

Kampeni dhidi ya Chanjo Na Corona awamu ya kwanza chini ya Rais Magufuli ilipigwa Na Serikali nzima chini ya Raisi Magufuli mwenyewe lakini kampeni ya Sasa ya kukiri Corona ipo Na Chanjo itumike inapigwa na Waziri Gwajima pekee yake ,hii ni ishara Kuwa Samia Yupo peke yake katika hili wakati mtangulizi wake alikuwa Na watu nyuma wa kumsaidia kufanya kampeni za kusema hakuna Corona.

Rais Samia hatafanikiwa kubadili fikra za watanzania hata Kama atawakamata wote wanaopingana Na msimamo wa Serikali yake Kwani Serikali yake imeshawavuruga wananchi.

Doroth Na Mollel ndiyo walikuwa Vinara wa nyungu,Na kusema hakuna Corona leo wageuke kusema Corona ipo Na Chanjo ni Salama,hakuna wa kumuelewa Maana Watanzania siyo miti,ni watu wenye akili zao timamu.

Askofu Gwajima Kwa kifupi ana hoja nzito,na Bahati nzuri hoja zake zote za kisayansi zimejibiwa Na wanasayansi labda Kama nae Askofu Gwajima hataki kusikiliza hao wanasayansi.

Binafsi nimesikia Hoja za Askofu Gwajima zikijibiwa vizuri Na Dr Mwele Malecela kuhusu muda wa utafiti wa Chanjo,hoja ya damu kuganda ilijibiwa vizuri Na Prof Janabi,hoja ya watu kuchanjwa Na kupata maambukizi imejibiwa vizuri na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza pamoja Na Dr Derick wa Tanzanite Hospital kupitia Vyombo vya Habari .

Tatizo kubwa naloliona walewale walioendesha propaganda za Kuwa Hakuna Corona leo wanaongoza propaganda za Kuwa kuna Corona Na Chanjo ni salama .

Hoja za Askofu Gwajima ndiyo Hoja za wananchi huku nje,zijibiwe kisayansi na Mara Kwa Mara!maana Hoja za Kuwa Corona haipo,Chanjo siyo Salama haiwezi kujibiwa Siku Moja kupitia TBC ikafuta imani iliyopandikizwa kichwani mwa wananchi Kwa muda wa Mwaka mmoja Na Serikali hii hii na watu hawahawa.

Samia Kama anataka kuaminika Kwenye hili,Yeye binafsi awe kinara wa kutoa elimu,wasaidizi wake wawe Vinara Maana Sasa kaachwa Doroth Gwajima pekee tofauti Na wakati wa Magufuli.

Kitu cha mwisho,CCM kaeni Na Askofu Gwajima zungumzeni nae,tuhuma anazozitoa Kuwa Serikali imehongwa Ili ipokee chanjo ni tuhuma nzito.

Askofu Gwajima anataka kumaanisha Rais Samia kahongwa Ili kuwauwa Watanzania?kwamba Samia kahongwa ili 2025 watanzania wote wawe wamekufa?hizi ni tuhuma nzito.

Tuhuma hizi pekee ni hoja binafsi Bungeni kuwa Mbunge ka mtuhumu Rais kuhongwa Ili aangamize watu wake.

Tuhuma za Serikali(Rais)kuhongwa ni tuhuma nzito kuliko tuhuma ya aina yeyote,kumtuhumu Rais kuhongwa tena Ili watu wafe ni tuhuma mbaya Na nzito.

Naamini kikao kijacho cha Bunge,wabunge waihoji serikali kuhusu tuhuma hizi nzito zilizotolewa Na Mbunge Kuwa Serikali imehongwa.

Hizi ni tuhuma nzito kuliko tuhuma yeyote Kwa Serikali na Chama Tawala.

Kwa sasa dhana ya Uwajibikaji wa pamoja ambayo ilikuwepo wakati wa Serikali ya Rais Magufuli ilikuwepo wakati wa janga la Corona,Ila Kwa Sasa hakuna dhana ya uwajibikaji wa Pamoja!Katika Corona!CCM Na Serikali hawapo pamoja kila mtu Na msimamo wake.

Gharama za Kuwa sehemu ya taasisi ni kuwajibika pamoja,Kama huwezi kuiishi dhana ya uwajibikaji wa pamoja unanshauriwa usiwe sehemu ya Serikali.
Mkuu mwambie Dotto Bulendu kuwa serikali ya Tanzania haijawahi kusema hakuna corona, wala haitaki kuchukua hatua za kupambana na corona, na wala kukataa chanjo ya corona- MENGINE yote sina shida nayo maana ni hulka za kiana harakati.
Kwa faida ya wengi na nukuu maneno haya

“You can be wrong if you’re dealing with information that is evolving.” The data about covid-19 and the vaccines seems to change nearly every day; for those of us with potentially confounding conditions, we carefully monitor that changing and updating data" (Anthony S. Fauci, infectious-disease expert)
 
Josephat Gwajima yuko na hoja lakini kwanini anafanya kama mashindano yani kila siku akilala akiamka anaanza kuipondea hiyo chanjo serikali ilishasema kuchanja sio lazima yeye alishasema hatachanja lakini kwanini amekua mtu wa kurudiarudia hili kila siku mpaka mtu unaitukana serikali kweli?Nauona mwisho mbaya sana kwa huyu jamaa hata time will tell huwezi shindana na serikali .....Upande wa Gwajima Waziri hakupaswa kuendelea kuwa waziri ingekua vyema angejiuzulu hauwezi kuwa kigeugeu watu hawawezi kukuelewa hata kidogo ulituambia ni tisa saivi unasema sita ...yote kwa yote elimu bado inahitajika sana kwa watu
 
Tatizo kubwa sio serikali wala Gwajimas. Tatizo kubwa ni ujinga wa baadhi ya waTanzania walio wengi tena wakiwemo walioenda shule. Ni wajinga nasisitiza.
Serikali imeleta chanjo. Anayetaka achanje, bure! Asiyetaka aache, pia kuacha ni bure! Sasa makelele ya nini? Au ni kukosa kazi za kufanya?
Mtu asiyetaka chanjo anaidai nini Serikali? Ni vitu vya ajabu kila siku kuwe na ubishani kuhusu chanjo, kama mtu anaona haifai siaiache tu?? Narudia, shida sio Serikali wala Gwajimas, shida ni ujinga wa baadhi ya miTanzania.
 
Tatizo kubwa sio serikali wala Gwajimas. Tatizo kubwa ni ujinga wa baadhi ya waTanzania walio wengi tena wakiwemo walioenda shule. Ni wajinga nasisitiza.
Serikali imeleta chanjo. Anayetaka achanje, bure! Asiyetaka aache, pia kuacha ni bure! Sasa makelele ya nini? Au ni kukosa kazi za kufanya?
Mtu asiyetaka chanjo anaidai nini Serikali? Ni vitu vya ajabu kila siku kuwe na ubishani kuhusu chanjo, kama mtu anaona haifai siaiache tu?? Narudia, shida sio Serikali wala Gwajimas, shida ni ujinga wa baadhi ya miTanzania.
Kwa mawazo yako unaisi kila mtz, hanautashi wa kutosha juu ya chanjo zote.
Wewe mwenyewe tukikuuliza juu ya chanjo gani ni salama?? utabaki kimya.
But sipo kwa ya kumtetea huyu Askof Rashidi . The problems is government
Kwa nini wasitoe elimu ya kutosha juu ya chanjo. Kwa hiyo wananchi wengi wanabaki dailema hawajui ipi ni kipi , sasa wanatokea watu wapuuuzi kama Askof, hanaongea vitu alivyo viota usiku, nakuongea as if hana scientific research juu hiyo .
Wakati ni layman tuu, Hanaye itaji msada wa ki- psychology
 
Back
Top Bottom