DPP: Ushahidi Kagoda unakaribishwa

Miaka si mingi iliyopita tulikuwa tunashangaa na wengine kuwacheka babu zetu jinsi walivyoendeshwa na wakoloni. Sasa leo hii sii na midigrii yote hiyo, vyombo vya habari, exposure etc. Kwa utaratibu huu Historia itakuja kutuhukumu bila huruma na tutachekwa kupita mno and this is just within the coming ten years!
 

Wakoloni walikuwa na vibaraka na mbwa wao wa kuwalinda, vivyo hivyo siku hizi mafisadi wana vibaraka na mbwa wao!
Vibaraka na mbwa hao ni hatari kuliko hata mafisadi wenyewe kwa mafisadi wanawategemea hao.
Kwa bahati mbaya sana, mara nyingi wananchi wanategemea vibraka na mbwa wa mafisadi kuwasaidia katika vita dhidi ya ufisadi.
Ili kushinda vita dhidi ya ufisadi, mapambano yanatakiwa yaelekezwe kwanza kwa vibaraka na mbwa wa mafisadi ambao ndio wanaowalinda mafisadi na baada ya kuwamaliza itakuwa rahisi kuwashughlikia mafisadi.
 
yani MH. RAIS ROSTAM AZIZ kajipanga wee and dealt with all trails that implicate him for those 4 years and then he was like ''DPP, now let the CIRCUS begin''
 
Enough said

Pelekeni ushahidi acheni kulalamika kama wenzenu walivyobumbulua mambo ya watergate.
 
Kwa mwendo huu wa fenesi et al., wengi tutamalizwa kwa shinikizo la damu na ugonjwa wa moyo
 
Tukuletee ushahidi,huo mshahara wako tutagawana?..ninyi leteni ujanjaujanja,ila yana mwisho haya,.wapi Mubaraka,Mobutu n.k
 
Ni bora kukaa kimya watu wakakudhania kuwa u mpumbav kuliko kuongea watu wakathibitisha kuwa u mpumbavu, DPP ni taasisi ya mashtaka nt investigatory organ, nlikuwa napita tu anyway.

Mbuki Feleshi, umeisema vizuri na katika hili Eleizer Feleshi kwa kufungua mdomo wake amethibitisha 'upumbavu' wake. Bora angekaa kimya.



Mwanyika, Mwema na Hosea walivyotayarisha report yao na kumkabidhi Rais, walitumia ushahidi gani? Na Rais alivyowapongeza kwa kazi nzuri waliyofanya na kuweza kuwabana wezi wa EPA wakarudisha Shs 53 Bilioni (kati ya Shs 133 Bilioni zilizoibiwa), walitumia ushahidi gani?

Na Quality Group (Manji) alivyofungua kesi ya madai dhidi ya Kagoda (Rostam), alitumia ushahidi gani?

Sasa kwa nini huyu Feleshi leo aseme "leteni" ushahidi, au anataka ushahidi gani? Makoye matale!!!!!
 
Hapa ndipo maneno ya zamani kama "Tumenyanyaswa kiasi cha kutosha, tumedhalilishwa kiasi cha kutosha, tumeonewa kiasi cha kutosha, tumedharauliwa kiasi cha kutosha" yanapokuwa na maana sana.

Haikubaliki DPP kusema anataka taarifa kutoka kwa watu wasio na uwezo kwa kupata taarifa hizo kisheria. Benki Kuu na CRDB zina wafanyakazi na sheria zinazitaka ziwe na kumbukumbu ya financial transactions ZOTE!!! Ananiomba mtu kama mimi anategemea naweza kupata kumbukumbu hizo kutoka vyombo hivyo vya fedha???

Namuuliza DPP, je amefungua kesi yoyote kuishitaki KAGODA??? Au anaizungumzia tu?? Nadhani akifungua kesi kuna uwezekano wa kupata taarifa kwa watu watakaojitoa muhanga na kuanika mambo haya. Ingekuwa busara kukaa kimya kuliko kuleta jambo hili katika hadhara ya watu wenye ufahamu mkubwa.

Disappointed!!!
 

Inakatisha tamaa lakini 'time will tell' tena hatuta tafuta mwenye kagoda bali wote walioilinda kwamaana kwamba muda ukifika viongozi wote waliochangia kutumaliza watalipa kwa kuwajibishwa na umma
 
Huu sasa ni uhuni - DPP acha ujinga na ubabaishaji. Kwa taarifa yako huko mahakamani kuna kesi iliwahi kufunguliwa na mtu anayejiita Yusufu Manji akidai ni yeye aliidhamini Kagoda kuchota hela Benki Kuu, je ulifuatilia ? Katika kukusaidia hebu soma hapa;


Lakini kubwa zaidi ni hii inayofuatia;
Na katika kuongezea chumvi kwenye kidonda;

Jamaa wote waliotajwa hapo juu hakuna hata moja aliyewajibishwa hadi leo. Feleshi, ni kama unatutukana Watanzania unapodai mwenye ushahidi kuhusu Kagoda akuletee, ili uufanyie nini ? Unataka kuuchakachua huo ushahidi kwa kuwasafisha mabosi wako waliokuteua ambao hawawezi kusafishika hata kama watavua magamba hadi damu ziwatoke ? Ningekuwa wewe, ningejinyamazia kuliko kuonyesha huu ubumbumbu na ukilaza huu wa kutisha, pambafu.

Wizi wa Kagoda - Chama tawala iliwala Watanzania !
1. Msimamizi Mkuu - Benjamin Mkapa, Raisi na Mwenyekiti wa CCM.
2. Mnufaikaji Mkuu - Jakaya Kikwete, mgombea Uraisi kutoka CCM.
3. Mnufaikaji Mkuu Msaidizi - Rostamu Azizi, Mweka Hazina wa CCM.
4. Mnufaikaji Msaidizi - Yusufu Manji, mfadhili wa CCM.
5. Mtekelezaji Mkuu - Zakia Meghji, Waziri wa Fedha.
6. Mtekelezaji Mkuu Msaidizi - Daudi Balali, Gavana Benki Kuu
Listi itaendelea .......................................
 
Huyu jamaa anaongea akiwa nyuma ya kivuli cha mtu mwenye nguvu sana, hasa mwajiri wake. Hawezikani kwa mtu kama yeye kusema upuuzi huu halafu eti mwajiri wake asimchukulie hautua za kinidhamu. Ni lazima mwajiri huyo awe ndiye aliyemtuma jamaa kumwaga upupu huo kwenye mikrofoni.
 
Mwenzenu anaelekezwa jamani,hatumii taaluma yake,yeye na kina Hosea wamefyata mkia kwa sab wanaelekezwa cha kufanya,ndio maana hosea kalalamika kupitia weki leaks
Cha kufanya ni kuweka ofisi,taasisi hizi huru kupitia ktb mpya,wakuu wake wasitokane na rais,vinginevyo hawawezi kufanya kitu kwa sababu wanahofia usalama wao,ni sawa na kumtoa mbwa meno na makucha yote halafu utegemee kutenda kazi,haitawezekana!
 
This mo<^&*$@%)@|\}r is a%@&#*le. Yaani huyu anamwakilisha huyo aliyemteua katika kazi zake. Jamaa pamoja na mamlaka hayo yote aliyonayo anashindwa kwenda pale CRDB na BoT kujua upupu uliofanywa na marafiki wa huyo aliyemteua?!!:A S cry:

Mkiona namna gani vipi, mfungulie Dr. Slaa na CHADEMA kesi kuwa wanaeneza chuki kwa kutoa habari za uongo kuhusu Kagoda. Hapo ndipo utapata ushahidi BUT ndani ya MAHAKAMA. Msitake kuwahadaa watanzania, they know better than that crap.
 
Hivi hawaoni hata aibu mbona sanaa hizi . ............. nisije kupigwa ban

Ndio maana

  • chenge na vijisenti vya jrsey mambo yameisha. "wanachi" hatuna ushaudi

kwani serikali iliyopo madarakani si ya wananchi. feleshi anataka kuseme ameshindwa kuorganise resources alizonazo ukupata ushaidi.


Disgusting
 
Mimi nautafsiri huu wito kama ni mwendelezo wa hila inayofanywa na uongozi mpya wa chama cha magamba wa kutaka kuionyesha jamii kwamba sasa wapo serious wanataka kupambana na ufisadi kumbe ni usanii mtupu! Watanzania lazima tupuuze wito wa kipumbavu namna hii na tuendelea na mapambano yetu kwa namna nyingine. Nawasihi sana viongozi wa chadema waendelee kuhamasisha wananchi kukichukia chama hiki cha magamba ili ifikapo 2015 tukifutilie mbali na uso wa dunia kupitia kwenye masanduku ya kura. Namshangaa sana DPP kwa kukubali kuendesha ofisi kwa maelekezo ya chama. Aibu gani hii isiyo na kifani!!
 
Feleshi, watu wakishindwa kazi tunawafukuzwa. Ondoka ofisini bila kupoteza muda wowote ule. Msitufanye sisi ni wajinga kama nyie. Nani Tanzania anauwezo wa kukusanya ushahidi zaidi ya wewe na vyombo vya usalama? Tanzania inavyombo vingapi vya ulinzi na upelelezi, mnafundishwa nini vyuoni nyie? Hizi njia zakutaka kuwaachia mafisadi nchini kwa kutumia hizi tactics ndizo zitawaweka clean sio? Fanya kazi na kama huwezi muondoke na kumwacha Dr Slaa apendekeze wanaoweza na kufanya kazi za wananchi. I am tired of you guys and real I hope ushetani wenu uwarudi. Ushahidi upo nenda wizara ya madini, treasure, BOT na ofisi ya raisi, wote wanajua wanayoyaficha au muulize makamba alipata wapi pesa ya kumpa mtoto wake January kuweza kufanya kampeni.

Vichwa bure kabisa na iko siku yenu nyie...Hamwangalii international news.
 


That is ezactly, how i also see it......and is no different but the usual pres. RA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…