DPW Special Thread: Uzi maalumu kuhusu kampuni ya DP World

Uchizi kamili.
Unajiachia wazi na kuonyesha hali yako halisi.

Usifikiri unaweza kunivuta kwenye kujadili ukichaa wako. Sina muda wa kupoteza na watu wa aina yako.
Rostam kaomba radhi huko, umesikia?
 
Mkataba ulisainiwa na Wazanzibari wawili kwa niaba ya watu milioni 60 wa nchi ya Tanganyika! Tena inawezekana ni baada ya kurubuniwa na hapo DP World!

Sasa unaposema "nyie", "kuweni", nk! Huoni kama hututendei haki! Tunahusika vipi na huo mkataba?
 
Baada ya DP World kuburuzwa mahakamani na nchi 10s, sasa wana boresha mikataba yao ili wasiweze kufikishwa mahakamani. Tanzania ni nchi ya kwanza kuifanyia majaribio na kuna viongozi nyuma yake wamehusishwa kuwahadaa wananchi na wameliingilia hadi bunge kwa njia ya kaki na madaraka
 
Mkataba ulisainiwa na Wazanzibari wawili kwa niaba ya watu milioni 60 wa nchi ya Tanganyika! Tena inawezekana ni baada ya kurubuniwa na hapo DP World!

Sasa unaposema "nyie", "kuweni", nk! Huoni kama hututendei haki! Tunahusika vipi na huo mkataba?
Hao wazanzibari sio watanzania?. Ubaguzi unaanzia kwenye mada kama hii.
 
Sasa hicho kifungu si ukilete hapa au unapenda kuongea bila ushahidi?
Utakapouona mkataba mahali soma kifungu hicho. Hawa wazee kina Shivji na Warioba wameamua kwa makusudi kusimamia vifungu wanavyojua wakiviweka wazi hadharani wataendelea kulinda heshima yao.

Sijui wanapoitwa ikulu au kuwa karibu na Rais Samia wanamtazama vipi usoni. Very unfair.
 
Sasa hicho kifungu si ukilete hapa au unapenda kuongea bila ushahidi?
Mkataba upo na kifungu kipo, mimi sina mkataba hapa lakini najua kuwa kifungu namba 14 sehemu namba 2 kumeelezewa juu ya utaifishaji.

Tunayo hulka ya kuchagua baadhi ya vifungu ambavyo tunadhani vinatupa hoja za kuupinga uwekezaji mzima wa DPW kumbe vipo vingine vyenye kuelezea tunatoka vipi kwenye matatizo hayo hayo.

Inasikitisha kuona wazee wa hadhi ya Shivji na Warioba wakinasa kwenye mitego hii hii inayowanasa watanzania wengi wa mitandaoni.
 
Mkuu nimekuomba ulete vifungu bado unabisha? Hebu nukuu hivyo vifungu unavyoona vina manufaa uviweke hapa. Na pia hivyo vifungu wanavyotumia Warioba na Shivji kama unaona havina maana yoyote vilete hapa tuvichambue. Kama huna hoja ukae kimya.
 
Una uhakika raia wa huko wanajitambulisha kama Watanzania?
Zanzibar ni NCHI. Wananchi kutoka Zanzibar ni wazanzibar sio watanganyika wala sio watanzania. Kama kuna mtu anabisha alete hoja, nimekaa pale!
 
Your browser is not able to display this video.
 
Inasikitisha leo mahakimu wa CCM wameamua kuwapa waarabu bandari kwa maslahi finyu ya mafisadi wachache. Inauma sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…