Dr. Cheni akanusha mfungwa Lulu kuonekana Uganda akila bata sikukuu ya Pasaka

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mlezi wa hiyari wa msanii Elizabeth Michael aka Lulu amekanusha binti yake kuonekana katika viunga vya Kampala Uganda akila bata wakati wa Pasaka.

Dr. Cheni amewataka waandishi kumtembelea Lulu gerezani ambako watamkuta amejaa tele akiendelea kutumikia adhabu yake ya miaka miwili gerezani.

Chanzo: Eatv!
 
Samahani mkuu, adhabu anayotumikia ni ya miaka miwili!
 
Unajua watu ambao hawajawahi kukaa gerezani huwa wanadanganyana sana tena sana. Yani hakuna askari wasio aminiana kama wa magereza na hakuna askari magereza anae mwamini mfungwa hata uwe mpole na mstarabu kiasi gani gerezani mfungwa anatoka na askari nje dakika tatu nyingi ukirudi lazima usachiwe leo ndo wamuache lulu akasherekee sikukuu uganda wakina ruge wako pale basi wangekuwa wanalala hotel kama ingekuwa ni rahisi jamani asiwadanganye mtu hata uwe na pesa kiasi gani ukishangia gerezani umeingia sana sana utapewa magodoro mazuri kama matatu ya kuungamisha kulalia.
 
Labda mbona nasikiaga eti "penye udhia penyeza Rupia"? Au hii haifanyi kazi gerezani?
 
Jamani, mtulia eti kichaa, faruu ndugai anapikia gesi, na lulu tena eti kaonekana Uganda jamani, mbona wale walioenda kumuona mbowe walimkuta dada wa watu amejikalia tu segerea
 

Hivi ulitegemea akubali? Nani hajui kwamba michezo hii huwa ipo?
 
kuna jamaa wa jj comunications huko moshi alihukumiwa kuozea jela alimchoma moto dereva fulani alihamishiwa maweni Tanga lakini akaonekana uarabuni huko na wala hayupo jela hii inawezekana kule moshi kuna wale wamiliki wa matours ambao wengi ni majambazi yakiyokubuhu wanalalaga makwao asubuhiwanarudi behind bars . enzi za kina msahita na wenzie
 
Jamani, mtulia eti kichaa, faruu ndugai anapikia gesi,, na lulu tena eti kaonekana Uganda jamani,,, mbona wale walioenda kumuona mbowe walimkuta dada wa watu amejikalia tu segerea
Kwahiyo walikuwa selo moja!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…