DR Congo: Wanafunzi walivamia Bunge wakitaka Walimu wao waongezewe mshahara

DR Congo: Wanafunzi walivamia Bunge wakitaka Walimu wao waongezewe mshahara

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Mamia ya wanafunzi wamelivamia bunge nchini DRC wakitaka walimu wao waongezewe mshahara.

Wanafunzi hao walikuwa wanapeperusha matawi na kuimba "tunataka kusoma" na "ikiwa hatutasoma, tutatumia dawa za kulevya".

Maandamano ya aina hiyohiyo yalitokea katika mji wa Beni kaskazini mwa Kivu ,kwa mujibu wa radio inayomilikiwa na Umoja Mataifa- Radio Okapi.

Walimu wamekuwa katika mgomo tangu Oktoba 4, mwanzoni mwa masomo mwaka huu wakitaka waongezewe mshahara na kupunguza umri wa kustaafu pamoja na masuala mengine.

Serikali imewashutumu viongozi wa dini ambao wanasimamia shule nyingi za msingi , kwa kudai kuwa wanahusika na mgomo huo ingawa viongozi hao wamekanusha madai dhidi yao.

Makamu wa rais wa Jamuhuri ya demokrasia ya Kongo Jean-Marc Kabunda, amewataka wanafunzi kurudi nyumbani maana haya sio mapambano yao.

"Nyinyi sio watu wa mtaani, mnapaswa kuwa shuleni na kama hampo shule mnapaswa kuwa nyumbani," alisema.
 
Sasa anapo sema ayo sio mapambano yao anamaanisha nn!? Kwan walimu wanapogoma anaeathirika ni nan kama sio wanafunzu?

Sasa waathirika wa mgomo wameamua waingilie kati hapo ni serikali itumie akili kutatua hilo tatizo sio kutumia kauli za hvyo
 
Back
Top Bottom