DR Congo: Watoto wawili waokolewa ziwani baada ya kutokea mafuriko

DR Congo: Watoto wawili waokolewa ziwani baada ya kutokea mafuriko

Boran Jakutay

Senior Member
Joined
Apr 8, 2023
Posts
110
Reaction score
259

WATOTO wawili wameokolewa wakielea karibu na ufukwe wa ziwa Kivu huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo siku chache baada ya mafuriko yaliyoua zaidi ya watu 400.

Haijabainika jinsi watoto hao wachanga walivyonusurika kwa siku tatu katika ziwa hilo, lakini mashuhuda wanasema walionekana wakiwa wanaelea.

Vijiji viwili viliathiriwa zaidi na mafuriko yaliyotokea wiki iliyopita na maiti zaidi zilipatikana kwenye tope siku ya Jumatano, na kufanya idadi ya waliofariki kufikia 411. ambapo kati ya marehemu hao, 317 tayari wamezikwa.
 
Mabadiliko ya tabia ya nchi. Ni hatari sana, tahadhali zaidi inabidi zichukuliwe hasa kuepuka kujenga mabondeni na kwny njia za maji.
 
Back
Top Bottom