DR Congo yatishia kujiondoa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki

DR Congo yatishia kujiondoa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki

Umkonto

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2018
Posts
2,652
Reaction score
4,593
Je, DRC imeona ni bora kuwa na marafiki wachache wenye tija kuliko kuwa na marafiki wengi wasio na tija, au ipoje?

Habari kamili.

==========

Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imetishia kujiondoa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) iwapo jumuiya hiyo itashindwa kuiwajibisha Rwanda kwa madai ya unyanyasaji katika eneo la Mashariki lililokumbwa na ghasia.

Tishio hilo lilitolewa baada ya Mahakama ya Haki ya EAC kuripotiwa kukubali kuanza kesi dhidi ya Rwanda kuhusu kuhusika kwake na ghasia mashariki mwa DR Congo.

Naibu Waziri wa Sheria wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Samuel Mbemba aliutaja kuwa "ushindi wa mahakama kwa nchi yetu".

Mbemba pia aliitaka Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kuanzisha uchunguzi kuhusu madai ya ukatili wa Rwanda mashariki mwa DR Congo.

Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limekuwa likipambana na kundi la waasi la M23 - linalodaiwa kuungwa mkono na Rwanda.

Taifa la Rwanda limekuwa likipinga madai hayo ya DRC.

Chanzo: BBC Swahili
 
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imetishia kujiondoa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) iwapo jumuiya hiyo itashindwa kuiwajibisha Rwanda kwa madai ya unyanyasaji katika eneo la Mashariki lililokumbwa na ghasia.

Tishio hilo lilitolewa baada ya Mahakama ya Haki ya EAC kuripotiwa kukubali kuanza kesi dhidi ya Rwanda kuhusu kuhusika kwake na ghasia mashariki mwa DR Congo.
Kwani iliombwa au iliomba kujiunga
 
Hawa wa Congo wa jinga sana.mimi nikipewa nchi hio nitawale, na ina mali vile siku ya pili ningefika kwenye palace ya Kagame.

Kama wananchi wako wamezowea kukata viuno nenda uka recrute kwenye nchi zingine ambazo zimezowea vita kama Yemen, Sudan, Somal, Eritrea kule South America uone kama Rwanda atachezea tena Congo.
 
Hawa wa Congo wa jinga sana.mimi nikipewa nchi hio nitawale, na ina mali vile siku ya pili ningefika kwenye palace ya Kagame.

Kama wananchi wako wamezowea kukata viuno nenda uka recrute kwenye nchi zingine ambazo zimezowea vita kama Yemen, Sudan, Somal, Eritrea kule South America uone kama Rwanda atachezea tena Congo.
Congo DR ni moja ya nchi zenye wanajeshi waoga duniani..Nilishawahi kuona wakipambana na shambulizi moja the way walivyokua wanawakimbia maadui kwa uoga ilikua kichekesho sana kwangu..
 
Askari wa jeshi la Kongo wanazidiwa na Suma JKT ya bongo
 
Je, DRC imeona ni bora kuwa na marafiki wachache wenye tija kuliko kuwa na marafiki wengi wasio na tija, au ipoje?

Habari kamili.

==========

Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imetishia kujiondoa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) iwapo jumuiya hiyo itashindwa kuiwajibisha Rwanda kwa madai ya unyanyasaji katika eneo la Mashariki lililokumbwa na ghasia.

Tishio hilo lilitolewa baada ya Mahakama ya Haki ya EAC kuripotiwa kukubali kuanza kesi dhidi ya Rwanda kuhusu kuhusika kwake na ghasia mashariki mwa DR Congo.

Naibu Waziri wa Sheria wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Samuel Mbemba aliutaja kuwa "ushindi wa mahakama kwa nchi yetu".

Mbemba pia aliitaka Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kuanzisha uchunguzi kuhusu madai ya ukatili wa Rwanda mashariki mwa DR Congo.

Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limekuwa likipambana na kundi la waasi la M23 - linalodaiwa kuungwa mkono na Rwanda.

Taifa la Rwanda limekuwa likipinga madai hayo ya DRC.

Chanzo: BBC Swahili
Wabaki Africa ya kati, sijui hata waliingiaje EAC
 
Hawa wa Congo wa jinga sana.mimi nikipewa nchi hio nitawale, na ina mali vile siku ya pili ningefika kwenye palace ya Kagame.

Kama wananchi wako wamezowea kukata viuno nenda uka recrute kwenye nchi zingine ambazo zimezowea vita kama Yemen, Sudan, Somal, Eritrea kule South America uone kama Rwanda atachezea tena Congo.
una mawazo mazuri ila usidhanie viongoz wa drc hawapend kuwa hivyo ila kuna resistance ndani ya drc , ndani ya congo wapo viongoz na matajiri wanapenda hii situation iliyopo na ndio maana drc haitakuja kutulia hv karibuni , mpk hii generation iliyopo iondoke
 
Back
Top Bottom