Dr Joyce Ndalichako ateuliwa kuwa Rais wa umoja wa mabaraza ya mitihani Afrika

Dr Joyce Ndalichako ateuliwa kuwa Rais wa umoja wa mabaraza ya mitihani Afrika

DR JOYCE NDALICHAKO ATEULIWA KUWA RAIS WA UMOJA WA MABARAZA YA MITIHANI AFRIKA



Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania ( Necta), Dk Joyce Ndalichako, ameteuliwa kuwa Rais wa Umoja wa Mabaraza ya Mitihani Afrika (AEAA), nafasi ambayo awali ilikuwa ikishikiliwa na Serara Moahi wa Botswana.



Akizungumza baada ya kutangazwa kuteuliwa kwake, Dk Ndalichako alisema atatumia fursa hiyo kuendeleza ajenda mbalimbali zitakazosaidia kuinua elimu Bara la Afrika.

"Hii ni heshima ya pekee kwa Baraza la Mitihani Tanzania, kipindi cha mwaka mmoja nikiwa Rais wa AEAA nitaendeleza yaliyoanzishwa na mtangulizi wangu, pia kutekeleza ajenda mbalimbali zitakazoleta manufaa kwa nchi yetu," alisema Dk Ndalichako. Pia, alisema atajitahidi kuwa mbunifu na kupanua ushirikiano na nchi nyingine.

, kuhakikisha anawajengea uwezo zaidi wafanyakazi wa mabaraza ya mitihani kwa nchi wanachama.

"Kwa mfano kwetu naona changamoto kubwa ni suala la standardisation (kusanifisha alama za mitihani), nitajitahidi kuhakikisha watu wetu wanajengewa uwezo kwenye nyanja hii," alisema.

Alitumia fursa hiyo kushauri nchi za Afrika kuhakikisha zinatilia mkazo zaidi kuongeza walimu wa kutosha, walio bora na vifaa vya kujifunzia. Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Selestine Gesimba, alisema kupata cheo hicho ni heshima kwa nchi.



MY TAKE:
WATAKAOKASIRIKA WATAFUTE NCHI YAO WAKAJIFICHE HUKO
Asante sana mkuu kwa kutuletea habari hii nyeti na muhimu sana. Huyu mama ana sifa zote za kuwa kiongozi. Amejitahidi kuondoa uozo wote pale NECTA na kwa kuwa watu walishazoea kuiba mitihani na kufaulu visivyo basi mama amefunga mianya na ndiyo maana wengi wanampiga vita. Watu wafaulu kwa sifa ili na vyuo vyetu viwe na wanafunzi bora na si bora wanafunzi. Keep it up mama.
 
Teh teh teh! Hivi yule jamaa wa redio(angalia ubao wa matangazo) Geradi Hando bado yupo? hajatoa maoni? nadhani atakuwa wa kwanza kuhamia burundi kuukimbia ukweli huu, Maana alisema Ndalichako hafai, kazi yake ni kuonesha mazombi, LOH! SIKU HIZI MUNGU ANAWAUMBUA WANAFIKI MAPEMA SANA, HONGERA SANA DR. NDALICHAKO.
 
Haiwezekani bana hata huu uteuzi hatuna imani nao, lazima ango'ke tu, lazima aachie ngazi hata hiki cheo kipya alichopata ni lazima ang'oke, la sivyo kiwango cha elimu kitashuka.
 
[h=3]DR JOYCE NDALICHAKO ATEULIWA KUWA RAIS WA UMOJA WA MABARAZA YA MITIHANI AFRIKA[/h]

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania ( Necta), Dk Joyce Ndalichako, ameteuliwa kuwa Rais wa Umoja wa Mabaraza ya Mitihani Afrika (AEAA), nafasi ambayo awali ilikuwa ikishikiliwa na Serara Moahi wa Botswana.



Akizungumza baada ya kutangazwa kuteuliwa kwake, Dk Ndalichako alisema atatumia fursa hiyo kuendeleza ajenda mbalimbali zitakazosaidia kuinua elimu Bara la Afrika.

“Hii ni heshima ya pekee kwa Baraza la Mitihani Tanzania, kipindi cha mwaka mmoja nikiwa Rais wa AEAA nitaendeleza yaliyoanzishwa na mtangulizi wangu, pia kutekeleza ajenda mbalimbali zitakazoleta manufaa kwa nchi yetu,” alisema Dk Ndalichako. Pia, alisema atajitahidi kuwa mbunifu na kupanua ushirikiano na nchi nyingine.

, kuhakikisha anawajengea uwezo zaidi wafanyakazi wa mabaraza ya mitihani kwa nchi wanachama.

“Kwa mfano kwetu naona changamoto kubwa ni suala la standardisation (kusanifisha alama za mitihani), nitajitahidi kuhakikisha watu wetu wanajengewa uwezo kwenye nyanja hii,” alisema.

Alitumia fursa hiyo kushauri nchi za Afrika kuhakikisha zinatilia mkazo zaidi kuongeza walimu wa kutosha, walio bora na vifaa vya kujifunzia. Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Selestine Gesimba, alisema kupata cheo hicho ni heshima kwa nchi.



MY TAKE:
WATAKAOKASIRIKA WATAFUTE NCHI YAO WAKAJIFICHE HUKO

nani akajifiche wewe!hii nchi inaendaga hivyo hivyo tu,mwanzoni umeanza vizuri ila umemaliza kwa kuonesha utaahira wako na inaonesha uwezo wako kifikra ni duni
 
yaap bigup zako mama,yani n full kupunguza ma2ndu ya nyavu na kuvua papa adi vijidagaa vcvyojielewa!
 
Sideeq
Ni mafanikio gani aliyoyapata nchini katika kazi yake?

Kufutilia mbali wizi wa mitihani. Wezi wa mitihani hawana hamu naye. Komesha yao! Ni kiboko yao! Bravo Ndalichako, taji ni hapa hapa duniani!
 
Ni mafanikio gani aliyoyapata nchini katika kazi yake?

kama hujui lolote ni bora kunyamaza.....ifupi ni no,1 kw kufichua uuozo kwenye elimu!ni ni muwazi na zaidi ana ni msomi! na AN AKILI SANA!
 
kama hujui lolote ni bora kunyamaza.....ifupi ni no,1 kw kufichua uuozo kwenye elimu!ni ni muwazi na zaidi ana ni msomi! na AN AKILI SANA!
Nimekuuliza mafanikio aliyoyapata katika kufanyakazi nchini wewe unaniambia ni muwazi, Msomi, ana akili sana..

Hao ndio wasomi wetu.
 
Hiyo sasa itapelekea elimu ya Tanzania iludi kama ilivyokuwa zaman,kama kwenu zipo unafaulu,kama wewe ni mwenzangu na mimi,umeumia.duuuuuuuu!hatari..........sana.DR.Joyce alikuwa mtu mwenye msimamo sana,anafuata sana taratibu zilizopo.lakini may be tunaweza pata mbadala wake.:kev:
 
.............n rais wa balaza la mitian kwa nchi zinazoendelea afrika hukitoa s.afrika.......🙂

Sasa wewe hata kuandika kiswahili tu unapata shida na sasa kweli hata ukipata division zero kuna ubaya?
 
Back
Top Bottom