Dr.Kitila Mkumbo asema ‘Rasimu imechemka umri wa urais’

Dr.Kitila Mkumbo asema ‘Rasimu imechemka umri wa urais’

JERRY

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2009
Posts
630
Reaction score
502
‘Rasimu imechemka umri wa urais’


na Edson Kamukara




MHADHIRI wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu (DUCE), Dk. Kitila Mkumbo, amesema kuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, imechemka kwa kutoafiki maoni ya kutaka umri wa mgombea urais kupunguzwa.

Dk. Mkumbo ambaye pia ni Mkuu wa Kitivo cha Elimu cha chuo hicho, alitoa kauli hiyo jana mjini hapa wakati akitoa mada katika kongamano la hali ya elimu na mustakabali wa taifa, lililoandaliwa na Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha).

Alisema kuwa matokeo ya sensa na utafiti yameonesha kuwa asilimia 45 ya Watanzania ni watoto chini ya miaka 15 na asilimia 16 ni vijana wenye umri kati ya miaka 15 hadi 24.

“Kwa hiyo utaona kuwa asilimia 61 ya Watanzania ni watoto wa umri chini ya miaka 25. Hii ni nchi ya watoto. Kwa kweli kama kuna kitu rasimu hii ya katiba imechemka ni kutokubali wazo la kupunguza umri wa mgombea urais.

“Hakuna sababu ya msingi kwa nchi kutotawaliwa na mtu wa miaka 30. Huyu kama amepata elimu bora yenye kumwezesha kuchanganua mambo anafaa kabisa kuwa rais,” alisema.

Hata hivyo, wakati wa uzinduzi wa Rasimu ya Katiba, Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba alisema katika kipengele hicho waliamua kuwa umri wa mgombea urais uendelee kubakia ule ule wa kuanzia miaka 40.

Kuhusu mfumo wa elimu nchini, Dk. Mkumbo ambaye pia ni mshauri wa masuala ya kiufundi wa CHADEMA, alisema kuwa nchi zote zinazopanga mipango mizuri, fedha zake nyingi huelekezwa kwenye elimu ili kuwekeza kwa vijana.

“Leo nchi haina wataalam, ina vijana wenye elimu isiyowawezesha hata kuajiriwa au kujiajiri, lakini watawala wanazungumza kuchimba gesi. Hiyo gesi bila elimu itawalipukia. Tatizo letu tumechagua wenye akili ndogo kuwatawala wenye akili kubwa,” alisema.

Mkumbo alifafanua kuwa jamii iliyoelimika vizuri inapenda na kuheshimu kazi na haiamini kwenye ujanja ujanja, inapenda maadili na kuchukia rushwa, inapenda demokrasia.

“Elimu yetu imekaa kimitihani, wanafunzi wanasomea kufaulu mitihani wala si kuelewa. CHADEMA tunataka kutengeneza mfumo wa watu kujifunza, ambao utaunganisha elimu ya msingi na ufundi ili kuzalisha watu wanaofikiri na kujiajiri badala ya kuangalia vyeti na vyeo,” alisema.

Msomi huyo alifafanua kuwa taifa hili limekaa zaidi kwenye kuombaomba badala ya kujitegemea kama muasisi wake Mwalimu Nyerere alivyoweka misingi hiyo.

“CHADEMA inataka kutengeneza taifa la kujitegemea ndiyo maana tumeweka nguvu zote kwenye elimu. Tunapaswa kusema hapana kuwa ombaomba. Kulijenga taifa si kuimba tu ‘People’s Power’, hiyo ni hamasa, lazima tufikirie mbali na kufanya kazi kwa bidii,” alisema.

Alisema ili kuitathimini elimu yetu tunapaswa kupima ni watu wangapi wanapata elimu, ni elimu ya namna gani inatolewa kama wanaweza kufikiri, kuajirika na kuajiri wengine na anayehitimu anaaminika kwa kiwango gani katika jamii.

“Katika kupata suluhu ya hili, CHADEMA tunaona cha kufanya ni kuandaa sera mpya ya mfumo wa elimu yetu ambayo tutaitoa kwa wananchi kabla ya uchaguzi ili waisome na kutafakari nini tunataka kufanya,” alisema.

Mkumbo aliongeza kuwa kumekuwa na mfumo mbovu wa kubadilisha hovyo mitaala na kuwepo kwa mifumo mingi ya elimu ndani ya nchi moja ambayo imeharibu mfumo wa shule za umma na kukumbatia za binafsi.

Alisema CHADEMA haitafuta mfumo wa shule binafsi bali itaugawa katika makundi mawili ambapo moja litakuwa la huduma ambalo litasimamiwa na serikali ili kudhibiti kupandisha ada kiholela.

“Kundi la pili utakuwa mfumo wa biashara ambao utawaacha wapandishe ada watakavyo, lakini tutawatoza kodi kubwa,” alisema.

Aliongeza kuwa CHADEMA itatengeneza mfumo utakaowavutia watu wenye vipaji kujiunga na ualimu tofauti na sasa katika utawala wa CCM ambapo sifa moja ya kujiunga na ualimu ni lazima uwe umefeli.

Alisema kuwa hao wenye vipaji na wito watakapojiunga na ualimu watalipwa mishahara na maslahi yanayolingana na taaluma nyingine, kwamba CHADEMA inataka mishahara ya watumishi wa umma ifanane.

“Posho ya kufundishia lazima irudishwe kama ilivyokuwa zamani ili kumfanya mwalimu atulie aache kuhangaika kutafuta njia zingine za kuuza maandazi kujikimu kipato,” alisema.

Mwisho
 
Ninamuheshimu sana Dr.Katilia, lakini sikubari kabisa na wazo la miaka 30. Atuambie ni wapi kwenye demokrasia rais wake ana umri wa miaka 30? Almost Kila nchi, watoto na vijana huchukua % kubwa kutokana na ratio of 2:4 (two adults with 4 children) Kama wanafikiria kubadilisha umri wa mgombea, tutegemee kubadilishwa kwa umri wa ukomo wa mgombea
 
Kitila some time namshangaa sana, yaani kisa nchi ina watoto wengi basi nchi itawaliwe na watoto? hii argument mfu kabisa? bora angesema kingine!
 
Ningeshangaa kama asingelizingumzia hili swala la umri wa mgombea Urais nchini kutokana na historia yake na makundi yaliyopo ndani ya CDM.

Hata katika vita vya kisiasa, retreating is not only a sign of being defeated. it can be for tactical reason.
 
Miaka 30 hapana. Wanaosoma uwalimu na wale waliofeli? Labda huko Duce.
 
kwa sababu rais hatachaguliwa kwa kigezo cha umri pekee, bado sioni kwanini tunaweka kikwazo cha Umri. Kwa maana pamoja na umri wake kuwa mdogo, ni sifa zake zilizotukuka mbele ya umma wa watanzania ndizo zitakzomfanya afikiriwe na kukubalika na watanzania kuwa anafaa kuwa Rais katika umri wake huo mdogo.

Wazee kama ndio kusema eti wanakuwa wamejengeka kibusara na weredi mbona ndio hao wanatuangusha??? tatizo labda hapa ni gharama kubwa ambazo zitatumika kumtunza Rais mstaafu ambaye anaweza kuwa bado ana nguvu na akaishi labda hata miaka 50 baada ya kung'atuka urais.
 
Ninamuheshimu sana Dr.Katilia, lakini sikubari kabisa na wazo la miaka 30. Atuambie ni wapi kwenye demokrasia rais wake ana umri wa miaka 30? Almost Kila nchi, watoto na vijana huchukua % kubwa kutokana na ratio of 2:4 (two adults with 4 children) Kama wanafikiria kubadilisha umri wa mgombea, tutegemee kubadilishwa kwa umri wa ukomo wa mgombea
Tusiweke vizingiti visivyo vya lazima. kwangu mimi umri ni kizingiti kisicvho na msingi. Mtu ana uwezo wa kuchagua kwa nini asiwe na uwezo wa kuchagiliwa?
 
Naye huyu profesor?? Tz imeisha. Bora pr. Maji marefu. Nenda Duce.
 
Wakati mwingine wasomi wetu wanatufanya tujiulize maswali mengi bure kuhusu exposure zao.Hivi kweli dr. anamjua sawasawa mtu wa umri wa miaka 30 au ni kwa sababu wasomi wa chuo kikuu wahisi lolote wanalosema waweza kulisimamia??? kwa hili mtu huhitaji kwenda darasa.maana miaka 30 atakuwa amepata wapi uzoefu wa mambo ya ndani ya nchi kabla hata hujasema ya nje.
Tunahitaji tupate rais atakayeingia ikulu na kuanza kazi za maamuzi mara moja siyo rais wa kufika na kuanza kuuliza hili linafanyikaje!!!! mtawapa shida watanzania.

Kwa mfano kuna watu wanataka urais lakini ktk maisha yao hawajawahi hata office attendant anafanya kazi gani za kila siku.Hawa ni wale ndugu zetu walioanzia kazi mjengoni baada ya kutoka chuo hawajawahi kufanya kazi za ofisini.Leo umpe urais khaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Tuambie utafiti upi na sensa ya mwaka gani then nitatoa comment zaidi?
 
Tusiweke vizingiti visivyo vya lazima. kwangu mimi umri ni kizingiti kisicvho na msingi. Mtu ana uwezo wa kuchagua kwa nini asiwe na uwezo wa kuchagiliwa?
Katiba inakuruhusu kumiliki mawazo yako, siwezi kuingilia uhuru wa mawazo yako. It doesn't mean you're right
 
Hapa nadhani Kitila anampigia chapuo Zitto. Mtu kama Zitto sina mashaka juu ya uwezo wake wa kuongoza tatizo linakuja pale ambapo tutakapompa rungu kijana wa miaka 30 ambaye bado ana hulka ya kisharobaro.si atawapa ulaji madem wake?
 
Katika mchakato huu wa kujadili rasimu tujitahidi kujenga hoja kwa utulivu bila kutukunana. Makamu wa Rais wakati anazindua rasimu alitusihi tujitahidi 'kujenga hoja na sio kupiga kelele' akinukuu maneno yasemayo: Argue, Don't Shout!

Hoja yangu ilikuwa, na bado, ni kwamba Tume haijatupa sababu za msingi kwa nini mgombea urais lazima awe na miaka arobaini na kuendelea zaidi ya kusema kwamba katika uchambuzi wao hawakukuta nchi ambapo mtu alichaguliwa akiwa chini ya miaka 40, ambayo kwanza sio kweli, na pili sio sababu ya msingi.

Nikaeleza kwamba kisayansi hakuna tofauti za msingi za kiuwezo kiakili, kifikra na kimantiki baina ya umri wa miaka 40 na miaka mingine ya utu uzima kuanzia miaka 18. Ndivyo saikolojia ya makuzi inavyosema. Tofauti pekee ni za kijamii, ambapo vijana waliopo kati ya miaka 18 hadi pengine around 25-30 wanatarajiwa kuwa wapo katika ngazi mbalimbali za elimu ya juu na wengine bado wanatafuta kazi na wengine bado wana-settle katika kazi zao. Hivyo nchi kadhaa duniani zimeshusha umri wa kuania madaraka makubwa hadi miaka kati ya miaka 18-35 kwa kutambua ubaya wa ubaguzi wa kiumri. Nitatoa mifano michache hapa chini.

Nchini Uingereza umri wa kugombea nafasi ya ubunge ambayo inakufanya pia u-qualify kuwa waziri mkuu ulikuwa miaka 21 hadi mwaka 2005. Baraza la Vijana la nchi hiyo (British Youth Council) walipambana kwa miaka kadhaa hadi kufikia mwaka 2006 serikali ikasalimu amri na kushusha umri hadi miaka 18.

Katika nchi zifuatazo unaruhusiwa kugombea nafasi yeyote ukiwa na umri kuanzia miaka 18: Netherlands, Australia, Denmark.

Nchini Turkey, Rais lazima uwe na miaka 40 lakini waziri mkuu, ambaye ndiyo mkuu wa serikali, umri wa kugombea uwaziri mkuu ni sawa na umri wa kugombea ubunge ambao ni miaka 18.

Nchi zifuatazo zimweka umri wa miaka 35: Mexico, Brazil, Chile, Cyprus, Indonesia, USA.

Nchini Afrika Kusini wamekwepa kuweka umri maalumu isipokuwa wanatamka kwamba mtu yeyote mwenye sifa ya kuchagua ana sifa pia ya kuchaguliwa. Sifa ya kuchagua Afrika Kusini ni miaka 18.

Sasa wandugu katika kipindi hiki kigumu sana katika nchi yetu cha kulisuka taifa letu upya tujifunze kujenga hoja bila kutukanana. Hii kwamba wahadhiri siku hizi vipi, vilaza n.k., kisa mtu katoa hoja ambayo haifanani na ya kwako sio sawa.

Bila shaka naelewa kwamba wengi wetu tumekulia katika mfumo hodhi wa kimawazo na tumezoeshwa kufikiri kwa mtindo mmoja kwa muda mrefu sana na tumezoeshwa kuwashangaa na kuwazomea watu wanaotoa mawazo tusiyoyapenda na ambayo hayafanani na sisi tunavyofikiri. Lakini nafikiri ni muhimu tuanze kujifunza kuvumiliana na kustahimili hoja kinzani maadamu tumekwisha kukubali kuingia katika mfumo usio hodhi katika kila nyanja, ikiwemo uhuru wa kufikiri na wa kutoa mawazo. Hii ni muhimu sana hasa katika kipindi hiki cha kuandika katiba yetu upya.

Mjadala mwema.
 
Katika mchakato huu wa kujadili rasimu tujitahidi kujenga hoja kwa utulivu bila kutukunana. Makamu wa Rais wakati anazindua rasimu alitusihi tujitahidi 'kujenga hoja na sio kupiga kelele' akinukuu maneno yasemayo: Argue, Don't Shout!

Hoja yangu ilikuwa, na bado, ni kwamba Tume haijatupa sababu za msingi kwa nini mgombea urais lazima awe na miaka arobaini na kuendelea zaidi ya kusema kwamba katika uchambuzi wao hawakukuta nchi ambapo mtu alichaguliwa akiwa chini ya miaka 40, ambayo kwanza sio kweli, na pili sio sababu ya msingi.

Nikaeleza kwamba kisayansi hakuna tofauti za msingi za kiuwezo kiakili, kifikra na kimantiki baina ya umri wa miaka 40 na miaka mingine ya utu uzima kuanzia miaka 18. Ndivyo saikolojia ya makuzi inavyosema. Tofauti pekee ni za kijamii, ambapo vijana waliopo kati ya miaka 18 hadi pengine around 25-30 wanatarajiwa kuwa wapo katika ngazi mbalimbali za elimu ya juu na wengine bado wanatafuta kazi na wengine bado wana-settle katika kazi zao. Hivyo nchi kadhaa duniani zimeshusha umri wa kuania madaraka makubwa hadi miaka kati ya miaka 18-35 kwa kutambua ubaya wa ubaguzi wa kiumri. Nitatoa mifano michache hapa chini.

Nchini Uingereza umri wa kugombea nafasi ya ubunge ambayo inakufanya pia u-qualify kuwa waziri mkuu ulikuwa miaka 21 hadi mwaka 2005. Baraza la Vijana la nchi hiyo (British Youth Council) walipambana kwa miaka kadhaa hadi kufikia mwaka 2006 serikali ikasalimu amri na kushusha umri hadi miaka 18.

Katika nchi zifuatazo unaruhusiwa kugombea nafasi yeyote ukiwa na umri kuanzia miaka 18: Netherlands, Australia, Denmark.

Nchini Turkey, Rais lazima uwe na miaka 40 lakini waziri mkuu, ambaye ndiyo mkuu wa serikali, umri wa kugombea uwaziri mkuu ni sawa na umri wa kugombea ubunge ambao ni miaka 18.

Nchi zifuatazo zimweka umri wa miaka 35: Mexico, Brazil, Chile, Cyprus, Indonesia, USA.

Nchini Afrika Kusini wamekwepa kuweka umri maalumu isipokuwa wanatamka kwamba mtu yeyote mwenye sifa ya kuchagua ana sifa pia ya kuchaguliwa. Sifa ya kuchagua Afrika Kusini ni miaka 18.

Sasa wandugu katika kipindi hiki kigumu sana katika nchi yetu cha kulisuka taifa letu upya tujifunze kujenga hoja bila kutukanana. Hii kwamba wahadhiri siku hizi vipi, vilaza n.k., kisa mtu katoa hoja ambayo haifanani na ya kwako sio sawa.

Bila shaka naelewa kwamba wengi wetu tumekulia katika mfumo hodhi wa kimawazo na tumezoeshwa kufikiri kwa mtindo mmoja kwa muda mrefu sana na tumezoeshwa kuwashangaa na kuwazomea watu wanaotoa mawazo tusiyoyapenda na ambayo hayafanani na sisi tunavyofikiri. Lakini nafikiri ni muhimu tuanze kujifunza kuvumiliana na kustahimili hoja kinzani maadamu tumekwisha kukubali kuingia katika mfumo usio hodhi katika kila nyanja, ikiwemo uhuru wa kufikiri na wa kutoa mawazo. Hii ni muhimu sana hasa katika kipindi hiki cha kuandika katiba yetu upya.

Mjadala mwema.

Jana usiku wakati jaji warioba akiongea ktk kipindi cha ITV alizungumza kuhusu nafasi ya spika alijaribu kutetea kupata spika nje ya wabunge alisema'' mataifa mengi ya common wealth yanatumia mtindo wa spika kuwa mbunge toka chama tawala, lakini kwa tanzania tumeshuhudia mapungufu mengi na kugundua ni bora tuanze na huu utaratibu ili kuweka heshima kwa bunge kwa kuwa na spika asiyetokana na vyama''.Kuhusu vijana dr. napingana na wewe sababu, kwanza Tanzania hatujawa na utaratibu wa kuandaa vijana kushika uongozi, si serikali au familia moja moja.Leo wewe dr.unaweza kutuletea mifano ya familia zilizoweza kuandaa vijana ambao ukitoa mfano hapa tutaridhika kama wako tayri ??? Tunahitaji kuwa na sera ya kuendeleza vijana na kuwapa nafasi ya kushika madaraka ya uongozi baadae.
Tatizo hili kaligundua hata rAIS OBAMA na ndiyo moja ya mission yake atakapotembelea afrika, amegundua mapungufu kuwa vijana hawaandaliwi.Marekani wamepitisha hilo kwa sasa wanaandaa wanasayansi vijana kwa miaka ijayo.Tulizungumze kwanza hili na vijana walielewe kwamba tunaawaaandaa kushika hatamu na kweli tuonekane kuwaaandaa na wao waonekane wanaandaliwa.
Lakini leo tunashuhudia wanasiasa vijana wanapopewa madaraka wanaanza misuguano na viongozi wao, yote hiyo ni proof kwamba vijana wapo tayari ila HAWAJAAANDALIWA kuwapa nafasi ni janga kwa taifa.poleni vijana lakini dunia imegundua sasa mapungufu hayo.
 
Katika mchakato huu wa kujadili rasimu tujitahidi kujenga hoja kwa utulivu bila kutukunana. Makamu wa Rais wakati anazindua rasimu alitusihi tujitahidi 'kujenga hoja na sio kupiga kelele' akinukuu maneno yasemayo: Argue, Don't Shout!

Hoja yangu ilikuwa, na bado, ni kwamba Tume haijatupa sababu za msingi kwa nini mgombea urais lazima awe na miaka arobaini na kuendelea zaidi ya kusema kwamba katika uchambuzi wao hawakukuta nchi ambapo mtu alichaguliwa akiwa chini ya miaka 40, ambayo kwanza sio kweli, na pili sio sababu ya msingi.

Nikaeleza kwamba kisayansi hakuna tofauti za msingi za kiuwezo kiakili, kifikra na kimantiki baina ya umri wa miaka 40 na miaka mingine ya utu uzima kuanzia miaka 18. Ndivyo saikolojia ya makuzi inavyosema. Tofauti pekee ni za kijamii, ambapo vijana waliopo kati ya miaka 18 hadi pengine around 25-30 wanatarajiwa kuwa wapo katika ngazi mbalimbali za elimu ya juu na wengine bado wanatafuta kazi na wengine bado wana-settle katika kazi zao. Hivyo nchi kadhaa duniani zimeshusha umri wa kuania madaraka makubwa hadi miaka kati ya miaka 18-35 kwa kutambua ubaya wa ubaguzi wa kiumri. Nitatoa mifano michache hapa chini.

Nchini Uingereza umri wa kugombea nafasi ya ubunge ambayo inakufanya pia u-qualify kuwa waziri mkuu ulikuwa miaka 21 hadi mwaka 2005. Baraza la Vijana la nchi hiyo (British Youth Council) walipambana kwa miaka kadhaa hadi kufikia mwaka 2006 serikali ikasalimu amri na kushusha umri hadi miaka 18.

Katika nchi zifuatazo unaruhusiwa kugombea nafasi yeyote ukiwa na umri kuanzia miaka 18: Netherlands, Australia, Denmark.

Nchini Turkey, Rais lazima uwe na miaka 40 lakini waziri mkuu, ambaye ndiyo mkuu wa serikali, umri wa kugombea uwaziri mkuu ni sawa na umri wa kugombea ubunge ambao ni miaka 18.

Nchi zifuatazo zimweka umri wa miaka 35: Mexico, Brazil, Chile, Cyprus, Indonesia, USA.

Nchini Afrika Kusini wamekwepa kuweka umri maalumu isipokuwa wanatamka kwamba mtu yeyote mwenye sifa ya kuchagua ana sifa pia ya kuchaguliwa. Sifa ya kuchagua Afrika Kusini ni miaka 18.

Sasa wandugu katika kipindi hiki kigumu sana katika nchi yetu cha kulisuka taifa letu upya tujifunze kujenga hoja bila kutukanana. Hii kwamba wahadhiri siku hizi vipi, vilaza n.k., kisa mtu katoa hoja ambayo haifanani na ya kwako sio sawa.

Bila shaka naelewa kwamba wengi wetu tumekulia katika mfumo hodhi wa kimawazo na tumezoeshwa kufikiri kwa mtindo mmoja kwa muda mrefu sana na tumezoeshwa kuwashangaa na kuwazomea watu wanaotoa mawazo tusiyoyapenda na ambayo hayafanani na sisi tunavyofikiri. Lakini nafikiri ni muhimu tuanze kujifunza kuvumiliana na kustahimili hoja kinzani maadamu tumekwisha kukubali kuingia katika mfumo usio hodhi katika kila nyanja, ikiwemo uhuru wa kufikiri na wa kutoa mawazo. Hii ni muhimu sana hasa katika kipindi hiki cha kuandika katiba yetu upya.

Mjadala mwema.

wewe utakuwa unaugua ule ugonjwa wetu wa siku zote wa kulinganisha visivyolingana, hata ktk hizo nchi ulizozitaja kila Nchi imeweka Umri ambao inafikiri unafaa kutokana na utamaduni wake, sasa kwa nini sisi iwe tofauti?

Mila na desturi zetu hazikubaliani na hilo swala, kwetuu sisi mtu wa miaka 30 bado sana kwanza hata hajakomaa, wengi wetu bado tunakimbizana na videmu, ktk jamii nyingine kijana wa miaka 25 tayari anajua majukumu yake ktk jamii inayomzunguka kwa sababu jamii yake imeshamuandaa, wenzetu Ulaya, kijana wa miaka 18 anahama nyumbani anajitegemea analipa bili zake mwenyewe n.k na anajua nafasi yake, sisi kwetu miaka 25 bado ni mtoto tu na sia ajabu ktk maisha yake hajawahi hata kujilipia kitu chochote, hivyo hajakomaa!

Hata hizo ulizozitja usikute hizo sheria ni mpya, baada ya kuona labda sasa wameshafikia mahali ambapo vijana wao wameshakomaa kuweza kuwa viongozi, sisi kwetu bado, hivyo usilinganishe visivyolingana, kijana wa Miaka 30 Tz sio kijana wa miaka 30 Ulaya!

Na ushahidi upo, nenda Dodoma ukaone Wabunge wamjaa Disko wanacheza mduara na kushika shika malaya Disko, Wabunge wa Ulaya hawafanyi hivyo!
 
Dr Kitila, what you have said is accurate, what we need is dynamic tolerance our status in the global scale isn't unique except for the deplorable state of leadership at the helm. Wisdom isn't a matter of age and experience alone, it is borne of knowing one's limits in life and providing room for other opinions.
We don't always have to agree on everything and call ourselves united.
The New Constitution need a redress on the age issue for sure, as Kijana si taifa la kesho as was always said.
 
Jana usiku wakati jaji warioba akiongea ktk kipindi cha ITV alizungumza kuhusu nafasi ya spika alijaribu kutetea kupata spika nje ya wabunge alisema'' mataifa mengi ya common wealth yanatumia mtindo wa spika kuwa mbunge toka chama tawala, lakini kwa tanzania tumeshuhudia mapungufu mengi na kugundua ni bora tuanze na huu utaratibu ili kuweka heshima kwa bunge kwa kuwa na spika asiyetokana na vyama''.Kuhusu vijana dr. napingana na wewe sababu, kwanza Tanzania hatujawa na utaratibu wa kuandaa vijana kushika uongozi, si serikali au familia moja moja.Leo wewe dr.unaweza kutuletea mifano ya familia zilizoweza kuandaa vijana ambao ukitoa mfano hapa tutaridhika kama wako tayri ??? Tunahitaji kuwa na sera ya kuendeleza vijana na kuwapa nafasi ya kushika madaraka ya uongozi baadae.
Tatizo hili kaligundua hata rAIS OBAMA na ndiyo moja ya mission yake atakapotembelea afrika, amegundua mapungufu kuwa vijana hawaandaliwi.Marekani wamepitisha hilo kwa sasa wanaandaa wanasayansi vijana kwa miaka ijayo.Tulizungumze kwanza hili na vijana walielewe kwamba tunaawaaandaa kushika hatamu na kweli tuonekane kuwaaandaa na wao waonekane wanaandaliwa.
Lakini leo tunashuhudia wanasiasa vijana wanapopewa madaraka wanaanza misuguano na viongozi wao, yote hiyo ni proof kwamba vijana wapo tayari ila HAWAJAAANDALIWA kuwapa nafasi ni janga kwa taifa.poleni vijana lakini dunia imegundua sasa mapungufu hayo.

Hao wazee wanaotuongoza leo na watakaotuongoza huko tuendako waliandaliwa wapi?
 



Na ushahidi upo, nenda Dodoma ukaone Wabunge wamjaa Disko wanacheza mduara na kushika shika malaya Disko, Wabunge wa Ulaya hawafanyi hivyo!

Hao wazee ndio wamejaa zaidi kabisa kwenye hizo kumbi za disco. Hakuna hata uhusiano. Kwenye mambo ya maana hamtaki tujilinganishe na nchi zingine lakini kwenye mambo mengi ya ovyo mnataka tuige huko ulaya na kwingineko. Tuache ubaguzi wa umri na mwingine wowote.
 
Tusitumie uongo kunogesha hoja zetu.Kama hoja ni ya muhimu wala haihitaji uongo ili isimame.Inasimama yenyewe!

Nadhani Dr.Kitila hujamtendea haki Warioba kwa kumnukuu vibaya kuwa alidanganya kusema hakuna nchi yenye utaratibu huo wa kuwa na rais under 40.Alichosema ni kuwa hakuna raisi aliyewahi kuchaguliwa popote duniani akiwa chini ya miaka 40.Kama huo ni uongo na tuanzie hapo,tusipotoshe kauli yake.
 
Hao wazee ndio wamejaa zaidi kabisa kwenye hizo kumbi za disco. Hakuna hata uhusiano. Kwenye mambo ya maana hamtaki tujilinganishe na nchi zingine lakini kwenye mambo mengi ya ovyo mnataka tuige huko ulaya na kwingineko. Tuache ubaguzi wa umri na mwingine wowote.

Unavyosema kwanza ni kinyume chake, hilo la Umri ndio jambo lisilo na maana kuiga, na mambo ya maana hamtaki kuiga Ulaya kama kwa mfano nchi zote za Ulaya zinatumia Lugha zao kufundishia kuanzia chekechea mpaka Chuo Kikuu,mbona hamuigi hilo?

Badala yake mnaona Kiswahili ndio adui wa maendeleo wakati tafiti zimefanywa Dunia nzima na kuonyesha kwamba mtoto anaelewa zaidi na anakuwa na mafanikio zaidi kielimu anapofundishwa kwa lugha ambayo anaiongea Nyumbani au akiwa na wenzake!

Lkn ninyi mnataka kufuta Kiswahili na kukiweka daraja la pili au la tatu, sasa mimi kwangu hakuna jambo la maana kama hilo, na kama kuiga ya maana tungeiga hapo kwani hizo nchi zote ulizozitolea mfano zinatumia Lugha yake kufundishia kuanzia Cheke chea mpaka Elimu ya juu, hakuna jambo la maana kuiga zaidi ya hilo!
 
Back
Top Bottom