Dr.Kitila Mkumbo asema ‘Rasimu imechemka umri wa urais’

Dr.Kitila Mkumbo asema ‘Rasimu imechemka umri wa urais’

wewe utakuwa unaugua ule ugonjwa wetu wa siku zote wa kulinganisha visivyolingana, hata ktk hizo nchi ulizozitaja kila Nchi imeweka Umri ambao inafikiri unafaa kutokana na utamaduni wake, sasa kwa nini sisi iwe tofauti?

Mila na desturi zetu hazikubaliani na hilo swala, kwetuu sisi mtu wa miaka 30 bado sana kwanza hata hajakomaa, wengi wetu bado tunakimbizana na videmu, ktk jamii nyingine kijana wa miaka 25 tayari anajua majukumu yake ktk jamii inayomzunguka kwa sababu jamii yake imeshamuandaa, wenzetu Ulaya, kijana wa miaka 18 anahama nyumbani anajitegemea analipa bili zake mwenyewe n.k na anajua nafasi yake, sisi kwetu miaka 25 bado ni mtoto tu na sia ajabu ktk maisha yake hajawahi hata kujilipia kitu chochote, hivyo hajakomaa!

Hata hizo ulizozitja usikute hizo sheria ni mpya, baada ya kuona labda sasa wameshafikia mahali ambapo vijana wao wameshakomaa kuweza kuwa viongozi, sisi kwetu bado, hivyo usilinganishe visivyolingana, kijana wa Miaka 30 Tz sio kijana wa miaka 30 Ulaya!

Na ushahidi upo, nenda Dodoma ukaone Wabunge wamjaa Disko wanacheza mduara na kushika shika malaya Disko, Wabunge wa Ulaya hawafanyi hivyo!

Jamani katika mjadala huu wa umri, Tusisahau kuwa hadi huyu kijana achaguliwe katika umri wa say miaka 30, ina maana amepita katika mikono salama na jopo la watu wamemkubali ndio maana anapitishwa kugombea. Tusichukulie kama vile miaka 30 basi ni given kuwa rais. Kuna sifa zingine za kumwezesha kuwania urais hata kabla ya hio ya umri.

Kwangu mimi miaka 30 ni sawa tu. huyu mtu atafikaje hadi kufikia kuwania urais bila kuwa amepata exposure na kukomaa kiumri na kisiasa bila ya kuonekana na watu. Watu watamuona na kuridhika KUWA katika umri wake huo, tayari anafaa. Mbona DHAIFU aliambiwa na mding kuwa bado hajakuwa, na miaka kumi baadae si mmeona mambo yake au mtasema alikuwa bado tena.

Miaka 30 ni sawa.
 
Hivi Kwa nini Nyerere hakukutana na vikwazo vya umri wakati anapata fursa ya kuwa rais wa kwanza wa nchi hii?
 
Jamani katika mjadala huu wa umri, Tusisahau kuwa hadi huyu kijana achaguliwe katika umri wa say miaka 30, ina maana amepita katika mikono salama na jopo la watu wamemkubali ndio maana anapitishwa kugombea. Tusichukulie kama vile miaka 30 basi ni given kuwa rais. Kuna sifa zingine za kumwezesha kuwania urais hata kabla ya hio ya umri.

Kwangu mimi miaka 30 ni sawa tu. huyu mtu atafikaje hadi kufikia kuwania urais bila kuwa amepata exposure na kukomaa kiumri na kisiasa bila ya kuonekana na watu. Watu watamuona na kuridhika KUWA katika umri wake huo, tayari anafaa. Mbona DHAIFU aliambiwa na mding kuwa bado hajakuwa, na miaka kumi baadae si mmeona mambo yake au mtasema alikuwa bado tena.

Miaka 30 ni sawa.

Wewe umenishawishi, kuanzia sasa ninaunga mkono hoja, umri wa kugombe ushushwe mpaka miaka kumi na nane, ama sivyo ni uvunjaji wa haki za binaadamu kumpa mtu haki ya kupigia kura watu wengine na hapo hapo unamnyanganya haki ya yeye kupigiwa kura? now i see the nonesense of the 40 Years syndrome.
 
Tusitumie uongo kunogesha hoja zetu.Kama hoja ni ya muhimu wala haihitaji uongo ili isimame.Inasimama yenyewe!

Nadhani Dr.Kitila hujamtendea haki Warioba kwa kumnukuu vibaya kuwa alidanganya kusema hakuna nchi yenye utaratibu huo wa kuwa na rais under 40.Alichosema ni kuwa hakuna raisi aliyewahi kuchaguliwa popote duniani akiwa chini ya miaka 40.Kama huo ni uongo na tuanzie hapo,tusipotoshe kauli yake.


Thirty-year-old Kabila became president of the DRC (formerly Zaire) in 2001, when his father Laurent-Desire Kabila, who also served as president of the republic, was killed. In October 2006 he became the first democratically elected president under 40. (The world)

 
Tume kwa kutaka mgombea binafsi na kuacha umri wa kugombea urais kuwa miaka 40 imejicontradict.

Kimsingi, mwenye haki ya kumpigia kura rais awe na haki ya kupigiwa kura kuwa rais.Kama hana potential ya kuwa rais tumewezaje kumpa haki ya kuchagua rais? Anyang'anywe na hiyo basi tuseme walio na haki ya kumpigia kura rais ni wenye miaka 40 na zaidi tu.

Umri wa kuweza kuwa rais uwe miaka 18.

Which does not mean ni lazima tuwe na rais wa miaka 18.Practically ni vigumu sana kumpata kijana mwenye miaka 18 mwenye experience ya kuwa rais. Lakini hili waachiwe wananchi kuamua, ndiyo maana ya demokrasia.

Katiba inapoanza kuweka wigo wa demokrasia arbitrary inawapora wananchi haki zingine inazotoa. Inatoa haki kwa mkono wa kulia na kuichukua kwa wa kushoto.Why 40 and not 39, 36, 35 or 30 for example? At least 18 is the age of majority.

Kuruhusu vijana zaidi kugombea urais haimaanishi ni lazima wawe marais. Only hatumnyimi haki yake ya kikatiba raia anayefaa.
 
Tusitumie uongo kunogesha hoja zetu.Kama hoja ni ya muhimu wala haihitaji uongo ili isimame.Inasimama yenyewe!

Nadhani Dr.Kitila hujamtendea haki Warioba kwa kumnukuu vibaya kuwa alidanganya kusema hakuna nchi yenye utaratibu huo wa kuwa na rais under 40.Alichosema ni kuwa hakuna raisi aliyewahi kuchaguliwa popote duniani akiwa chini ya miaka 40.Kama huo ni uongo na tuanzie hapo,tusipotoshe kauli yake.

Nafikiri kuna shida katika kusoma maandishi. Nilichosema mie ni Warioba hakusema kweli kwamba hakuna nchi alipochaguliwa rais chini ya miaka 40. Sasa sijui hiyo ingine umeitoa wapi.
 
Back
Top Bottom