Mezeni nyembe mnaomchukia Dr Mwakyembe H, hatuna cha kuwasaidia ....anajua anachokifanya heko Harrison! Mafisadi na mapandikizi wao nafasi yao inazidi kuwa finyu kila mtego wao utawanasa wao wenyewe.
Masanilo aka Ze Comedy,
Wewe beba tu mabox ya Wazungu huko Majuu; unashangaa hilo mbona hushangai mtu kuchukua posho mbili na bado akajiona hajakosea?
Wewe lipwa mara mbili kwenye hizo boksi zako tuone kama hutatupwa mpaka huko kwenu Mwanza.
Hii inatuonyesha dhahiri kwamba sio kila kinachopitiwa na editor in material. Wakatimwingine kuna agenda zao au hata ulevi tu wa kifisadi. Kuna siku nilisoma kuhusu tikio ambalo mimi nilikuwepo. Kilicho ripotiwa baadae klikuwa tofauti kwa kila reporter. Ukisoma katikati ta mstari utaona kuwa wanaunganisha "values" zao na habari. Kama vile tunavyoweza kucheza na data.....ukitata number ziseme JF ni mbaya unaweza tena bila shidaKuna tatizo kubwa kwenye hili gazeti na tayari limeshapoteza mwelekeo kwa sababu ya uswahiba wa wahariri na mafisadi. Hivi vichwa vya habari huwa wanaelekezwa kutoka MONDULI au IGUNGA. Si mnajua agenda ya hawa mafisadi! BURIANI Tanzania Daima! Tuliwapenda, lakini mafisadi waliwapenda zaidi...
Hii ya Ujerumani nasikia ni kweli,Mwakyembe alichukua pesa na wala hakusafiri kwenda uko Ujerumani,yeye ukimwuliza anasema watanifanya nini,kwani kati yenu nani anajua sheria kunizidi mimi....
Umesema sawa kabisaaa! Mawaziri na viongozi wengine kupokea mshiko mara mbili wala si la ajabu! Lakini cha kushangaza ni timing ya Takukuru! Na jinsi walivyotilia "UMUHIMU" kumbe hata wao waliwapa huo mshko huku wakijua kuwa ni kinyume cha sheria?? Mbona contradiction??
HIYO HELA ALIYOLIPA INALINGANA NA KAGODA, RICHMOND AU EPA? Tukifatilia vi kashfa mnavyotoa hakuna serikalini atakayepona.
HAPA TUNAJADILI ZAIDI MAHELA MAKUBWA.
Na haya yote yanakuja leo why?
Hivi wabunge wangine wote waliojiwa au kuna ambao walikataa kuojiwa kamwa mwakyembe?
Kuna tatizo kubwa kwenye hili gazeti na tayari limeshapoteza mwelekeo kwa sababu ya uswahiba wa wahariri na mafisadi. Hivi vichwa vya habari huwa wanaelekezwa kutoka MONDULI au IGUNGA. Si mnajua agenda ya hawa mafisadi! BURIANI Tanzania Daima! Tuliwapenda, lakini mafisadi waliwapenda zaidi...
Mwakyembe knows what is doing.....! safi sana
ukitaka kujua ilikua mchezo wa mafisadi dhidi ya Dr Harrison Mwakyembe angalia tu habari ilivyopokelewa na machapisho ya pale Kijiweni, Sinza. walijuaje hizo habari kama si Hosea kuwajulisha kua Dr Mwakyembe aligoma kuhojiwa na TAKUKURU.
Katuika ujumla wake TAKUKURU ilipaswa kuanza na Mawaziri, maana hakuna hata mmoja ambae hajawahi kupokea posho mbilimbili, wala haiitaji uchunguzi.
Serikali kuu inawalipa Per diem, kisha wanalipwa posho za kuishi huko bungeni Dodoma, aende Mawizarani akaulize kama kuna waziri hajalipwa posho yakujikimu akiwa Dodoma, kisha akamuulize Muhasibu wa Bunge kama hawajalipa posho nyingine kwa mawaziri hao wakiwa DODOMA.
Ambao hammjui Mwakyembe mtapata shida sana, jamaa ni mpambanaji kwa mambo anayopingana nayo lakini yeye mwenyewe ni fisadi mkubwa kwenye mambo mengine ambayo anafaidika nayo.
Kuna kashfa nyingine inakuja ambayo kwa msaada wa spika Sitta kalipwa mamilioni ya pesa kwa kusingizia kwamba alienda kutibiwa nje (Ujerumani) wakati ule baada ya ajali wakati alikuwa amejifungia nyumbani kwake Kunduchi.
Nchi hii inaliwa na hao hao wanaojifanya wanailinda.
Hivi habari hii ni kweli. Hebu toa details zaidi ili Takukuru, CAG na Cheyo wafuatalie. Unajua pengine hawa jamaa huwa hawasomi JF. Inabidi wapewe hizo details through other means.
Kwa hali ilivyo mimi sioni ajabu kwa hili maana wote Sitta na Mwakyembe kwa vipimo vyote ni mafisadi.