Hess
JF-Expert Member
- Feb 27, 2012
- 593
- 675
Wana jamvi,
Kumekuwa na mtazamo hasi na dhaifu wa utendaji wa Dr. Ndalichako na Baraza la Mtihani Tanzania NECTA hasa kutoka kwa watu wanaojiita WACHAMBUZI na wengine hujiita Wasomi. Wengi wao wanatoa uchambuzi wao kulaumu (NECTA) bila hata kujua nini NECTA wanashughulikia.
Gazeti la leo la MAWIO, na 0056, gazeti nisilolikosa kila wiki, gazeti linalopendwa na wazalendo na kuchukiwa na watawala limeingia katika mtego huu kwa kutoa maoni yao kuhusu Dr. Ndalichako:
1. MAWIO wanamlaumu Dr. Ndalichako na NECTA kwa ujumla wake kwa makosa ya mtihani wa MOCK kwa wilaya 40 ambapo maswali yakiluwa hayajibiki. Huu ni udhaifu wa wahariri wa MAWIO kutojua nani anahusika na mitihani wa MOCK. Kwa taarifa tu, mitihani ya utimilifu (MOCK) si mitihani ya NECTA bali huandaliwa na TAHOSSA, Tanzania Heads of Secondary Schools Association. Hawa ndo wanawajibika na MOCK si NECTA. Tusiwahukumu kwa wasilohusika nalo. TAHOSSA kila kanda hufanya mitihani hii na bajeti yao ni pesa ya wazazi.
2. MAWIO na hata baadhi ya wasomi wetu wasiojua ABCs za NECTA, wanalilaumu baraza kwa kufeli wanafunzi wengi kidato cha nne. NECTA na Ndalichako wanaingiaje hapa? NECTA ni Measurement and Evaluation organ, wanatumia sylabus iliyoandaliwa na Taasis ya ukuzaji mitaala kwa sera na miongozo ya Wizara ya Elimu. Wanatunga mitihani bila kujali mwanafunzi kasoma au hajasoma, katoka St. Kayumba au St. George, kamaliza sylabus au la, shule ina walimu au la. Wanatunga mtihani kwa kufuata sylabus na kuusahihisha then hutoa matokeo. Si kazi yao kujibu kwa nini wanafunzi wamefeli.
Kwa kilicotoke mwaka jana, serikali yetu iliamua kuwaburuza kwa kuficha aibu. Wakabadili formula, kama kuna mwanafunzi alifeli au kufaulu baada ya kurudia kumark si kazi yao maana marking quide yao ndo mwongozo wa marking.
3. MAWIO na wengi wa aina mtazamo huu wanalaumu eti elimu haitapanda kama hakuna upatikanaji wa vifaaa vya kufunzia na kujifunzia. Baraza linaingiaje hapa. Tuwe wasomi na wachambuzi wa kweli si kubeza kitu bila kukijua.
4. MAWIO wanalaumu kuwa kuna walimu wamefaulu hawana sifa. Si walimu wote wanahitimu ualimu toka mikononi mwa NECTA. Kuna wengi wamepita vizuri kwenye mitihani ya NECTA na walikuwa wazuri. Wamekuwa vilaza vyuoni maana elimu ya chuo kikuu haina uhusiano na NECTA. Mhadhiri ndo NECTA na ndio humtoa mwalimu.
5. MAWIO wanasema baraza limeshindwa kudhibiti viwango wakati nchi nzima wanalia ufaulu umeshuka, nani ameonyesha kuwa ufaulu umeshuka? NECTA ndo wametuonyesha hakuna kitu katika mashule yetu so TUWAPONGEZE.
6. Kuna dini moja wanataka Ndalichako ajiuzuru eti ANAKAMATA wanafuzi wa dini hiyo. Mawazo dhaifu. ni lini na wapi kuna majina wakati wa kusahihisha mitihani ya NECTA? Hivi hakuna wafanyakazi wa dini hiyo pale baraza? Mbona wapo wengi tu. Uwezo mdogo wa wanafunzi wetu na udhaifu wa shule zetu isibadilishwe kuwa lawama kwa Dr. Ndalichako.
Dr. Ndalichako anafanya kazi kubwa sana. Nani aseme leakage ya mitihani ya NECTA leo ikoje ukilinganisha na miaka ya nyuma? Tuseme ukweli, bila Dr. Ndalichako kusimama na kufanya kazi, kwa serikali yetu hii ya mbwembwe shule za kata zingekuwa zinatoa flying colour kuficha udhaifu. Big up Dr, usikate tamaa kwa uchambuzi dhaifu.
Kuna mwandishi mmoja wa radio moja (Soma kituo cha matangazo) anaitwa Gerald Hando, kwa ufinyu wa kufikiri na kutoelewa mambo ya elimu na mgawanyo wa kazi, alimlaumu mama Ndalichako eti kwa kuonyesha picha za Zombi. Hando anasema huyu mama hafai alitakiwa aje na mikakati ya kudhibiti hili si kuonyesha zombi. Nilijiuliza kama Hando ana uelewa wa kazi za NECTA na nani anatakiwa azuie MAZOMBI. Ndalichako was right kuumbua wale waliotakiwa kuzuia Zombi.
WANDISHI wengi wa Tanzania wameingia kwenye fani kuuza sura tu au kuganga njaa. Wengi hawana uelewa wa mambo mengi na wakitumia kalamu zao kupotosha umma. Kama hujui unachokichambua kwa kina UTAPOSHA. Kwa hili MAWIO mmechemka.
Kwa taarifa tu kuna WIZARA YA ELIMU, TAMISEMI, TIE, NECTA, EMAC, TAHOSSA, na wadau wengine kila mtu kwa nafasi yake wanatakiwa wafanye kazi. NECTA is all about Measurement and Evaluation. Mliosoma ualimu mnajua nasema nini, mtakuwa mnamkumbuka Prof. Omary.
Tumtendee haki Dr. Ndalichako na NECTA in general na tumhukumu anapoboronga kwenye sehemu yake, japo si msemaji wake nalazimika kuwaambia wasiojua wakae kimya. TOA HOJA
Kumekuwa na mtazamo hasi na dhaifu wa utendaji wa Dr. Ndalichako na Baraza la Mtihani Tanzania NECTA hasa kutoka kwa watu wanaojiita WACHAMBUZI na wengine hujiita Wasomi. Wengi wao wanatoa uchambuzi wao kulaumu (NECTA) bila hata kujua nini NECTA wanashughulikia.
Gazeti la leo la MAWIO, na 0056, gazeti nisilolikosa kila wiki, gazeti linalopendwa na wazalendo na kuchukiwa na watawala limeingia katika mtego huu kwa kutoa maoni yao kuhusu Dr. Ndalichako:
1. MAWIO wanamlaumu Dr. Ndalichako na NECTA kwa ujumla wake kwa makosa ya mtihani wa MOCK kwa wilaya 40 ambapo maswali yakiluwa hayajibiki. Huu ni udhaifu wa wahariri wa MAWIO kutojua nani anahusika na mitihani wa MOCK. Kwa taarifa tu, mitihani ya utimilifu (MOCK) si mitihani ya NECTA bali huandaliwa na TAHOSSA, Tanzania Heads of Secondary Schools Association. Hawa ndo wanawajibika na MOCK si NECTA. Tusiwahukumu kwa wasilohusika nalo. TAHOSSA kila kanda hufanya mitihani hii na bajeti yao ni pesa ya wazazi.
2. MAWIO na hata baadhi ya wasomi wetu wasiojua ABCs za NECTA, wanalilaumu baraza kwa kufeli wanafunzi wengi kidato cha nne. NECTA na Ndalichako wanaingiaje hapa? NECTA ni Measurement and Evaluation organ, wanatumia sylabus iliyoandaliwa na Taasis ya ukuzaji mitaala kwa sera na miongozo ya Wizara ya Elimu. Wanatunga mitihani bila kujali mwanafunzi kasoma au hajasoma, katoka St. Kayumba au St. George, kamaliza sylabus au la, shule ina walimu au la. Wanatunga mtihani kwa kufuata sylabus na kuusahihisha then hutoa matokeo. Si kazi yao kujibu kwa nini wanafunzi wamefeli.
Kwa kilicotoke mwaka jana, serikali yetu iliamua kuwaburuza kwa kuficha aibu. Wakabadili formula, kama kuna mwanafunzi alifeli au kufaulu baada ya kurudia kumark si kazi yao maana marking quide yao ndo mwongozo wa marking.
3. MAWIO na wengi wa aina mtazamo huu wanalaumu eti elimu haitapanda kama hakuna upatikanaji wa vifaaa vya kufunzia na kujifunzia. Baraza linaingiaje hapa. Tuwe wasomi na wachambuzi wa kweli si kubeza kitu bila kukijua.
4. MAWIO wanalaumu kuwa kuna walimu wamefaulu hawana sifa. Si walimu wote wanahitimu ualimu toka mikononi mwa NECTA. Kuna wengi wamepita vizuri kwenye mitihani ya NECTA na walikuwa wazuri. Wamekuwa vilaza vyuoni maana elimu ya chuo kikuu haina uhusiano na NECTA. Mhadhiri ndo NECTA na ndio humtoa mwalimu.
5. MAWIO wanasema baraza limeshindwa kudhibiti viwango wakati nchi nzima wanalia ufaulu umeshuka, nani ameonyesha kuwa ufaulu umeshuka? NECTA ndo wametuonyesha hakuna kitu katika mashule yetu so TUWAPONGEZE.
6. Kuna dini moja wanataka Ndalichako ajiuzuru eti ANAKAMATA wanafuzi wa dini hiyo. Mawazo dhaifu. ni lini na wapi kuna majina wakati wa kusahihisha mitihani ya NECTA? Hivi hakuna wafanyakazi wa dini hiyo pale baraza? Mbona wapo wengi tu. Uwezo mdogo wa wanafunzi wetu na udhaifu wa shule zetu isibadilishwe kuwa lawama kwa Dr. Ndalichako.
Dr. Ndalichako anafanya kazi kubwa sana. Nani aseme leakage ya mitihani ya NECTA leo ikoje ukilinganisha na miaka ya nyuma? Tuseme ukweli, bila Dr. Ndalichako kusimama na kufanya kazi, kwa serikali yetu hii ya mbwembwe shule za kata zingekuwa zinatoa flying colour kuficha udhaifu. Big up Dr, usikate tamaa kwa uchambuzi dhaifu.
Kuna mwandishi mmoja wa radio moja (Soma kituo cha matangazo) anaitwa Gerald Hando, kwa ufinyu wa kufikiri na kutoelewa mambo ya elimu na mgawanyo wa kazi, alimlaumu mama Ndalichako eti kwa kuonyesha picha za Zombi. Hando anasema huyu mama hafai alitakiwa aje na mikakati ya kudhibiti hili si kuonyesha zombi. Nilijiuliza kama Hando ana uelewa wa kazi za NECTA na nani anatakiwa azuie MAZOMBI. Ndalichako was right kuumbua wale waliotakiwa kuzuia Zombi.
WANDISHI wengi wa Tanzania wameingia kwenye fani kuuza sura tu au kuganga njaa. Wengi hawana uelewa wa mambo mengi na wakitumia kalamu zao kupotosha umma. Kama hujui unachokichambua kwa kina UTAPOSHA. Kwa hili MAWIO mmechemka.
Kwa taarifa tu kuna WIZARA YA ELIMU, TAMISEMI, TIE, NECTA, EMAC, TAHOSSA, na wadau wengine kila mtu kwa nafasi yake wanatakiwa wafanye kazi. NECTA is all about Measurement and Evaluation. Mliosoma ualimu mnajua nasema nini, mtakuwa mnamkumbuka Prof. Omary.
Tumtendee haki Dr. Ndalichako na NECTA in general na tumhukumu anapoboronga kwenye sehemu yake, japo si msemaji wake nalazimika kuwaambia wasiojua wakae kimya. TOA HOJA