Dr. NDODI: Kuvaa suruali kuna madhara kwa wanawake

Dr. NDODI: Kuvaa suruali kuna madhara kwa wanawake

Duh inabidi tuchambua kwa kina hoja zake labda kuna ukweli.

Kwenye swala la vitambi kuhusiana na nguo zinazobana kwa wanawake sidhani kama kweli.Wako wakina dada wengi sana ambao hawana vitambi, wanavaa suruali zinazobana kila siku na hawajapata vitambi.Swala la kitambi hapa linatoka na ukosefu wa mazoezi na kula bila mpangilio kwa pande zote za jinsia.


Kwenye swala la kujaa maji kwa wanawake tuna msubiri Michelle alete jibu lol.Nadhani dokta kachukulia kwa juu juu kwamba mtu akivaa soksi zinazo mbana miguu uvimba basi kaona labda na mwanamke akivaa suruali inayobana ikulu inajaa maji (maoni yangu).


Sasa labda anavielezo zaidi na kafanya utafiti hai.Atuambie aliwachukua wanawake wangapi ambao hawana vitambi na kuwavalisha suruali zinazo bana kwa mda gani mpaka akaja na maamuzi haya.
mbona hakusema kufuri na kawaida ya kufuli sikuzote inabana!!!
 
hilo taspeli limewashika sana watu, hamna kitu pale jamaa anafanya kazi ya shehe yahya tu
 
Jamani kama mtu una chuki binafsi usiziweke humu, kama mtu haujafanya utafiti wa kisayansi ya vyakula usilete siasa hapa, eti aya ipi inasema usile nguruwe hata kama ipo inaonekana hautafuata maana sio wote tunafuata mafundisho ya kidini, tusiwaite wengine waongo au wazandiki bila kuwa na justfication. Kama vipi nenda kinyume na ulaji anofundisha uugue kisukari ndio uende kwake akupe dawa na masharti ya mpangilio wa chakula uufuate alafu mwisho usipopona ndiyo hapo umkosoe.

Mafundisho ya ndodi kuhusu lishe na dawa ni sahihi kabisa. Kuhusu kuvaa suruali ndodi hajasema wanawake wasivae suruali bali wasivae suruali za kubana mtu anasema wazungu na wachina wanvaa suruali lakini hujaweka wazi ni za aina gani wachina wanavaa cotton na si za kubana wazungu asilimia kubwa wanavaa kaptula au suruali nzito wakati wa baridi. Hebu angalia wale black Americans wanaovaa tight trousers walivyo na vitambi na maumbo mabaya. Mwingine anadiriki kusema tangu ameanza kuvaa suruali za kubana mpaka sasa ingekua ni bwawa nakushauri uwe unasikiliza vizuri siyo kwamba maji yanatoka wakati wote bali wakati mahsusi pale unapopata mguso au unapokua faraga sasa endelea siku usipoachwa kwa kumfanya samaki mzee wakati anaingia ikulu.

Nawashauri ndugu zangu kama mtu unataka kupinga kitu kilichofanywa kiutafiti fanya utafiti wa aina ile ili uone matokeo ni yaleyale au tofauti? Tuache blabla watanzania, hasa pale maslahi yetu yanapoguswa vibaya. wachina wanaleta dawa zao, wazungu wanaleta wala hatuongei kitu ingawa zina kemikali zenye madhara mwilini sasa mwenzetu kaja na dawa isiyokuwa na side effect mnamtukana. Jamani ingia google search omega wash


kaka umesema sawa kabisa ndo sisi humu tunamukumu ndod af tunawaacha wanawake/wanamme zetu kwa kuwa wana shape mbaya automatcaly mwanaume mafuta yanakaa kweny ktambi na mwanamke kwenye hips na makalio sasa sayansi isiyo hitaji hata phd
kwenye kiuno dada kabana jins yake na mkanda ukiiangalia kwa nyuma utafikiri ana makalio manne sasa mafuta yatapita wapi kwenda kwenye hps na makalio??
Wakati huo huo machps,pza,baga nk vinaingia tu toilet week, akienda ka mbuz mtaan anadundika tu p@@@vu!!

Mf: wale wadada wanaokuwa na vtambi
wanavaaga mabelt kwenye tumbo ya nini?
 
Mi nataka kujua biological relationship ya kuvaa suruali na kujaa maji ikulu. na vipi wale mamodo mbona huvaa suruali muda mwingi na hawana vitambi? tunasahau kuwa vitambi vingi nyakati hizi vinaletwa na vyakula na njia za uzazi wa mpango inakuwaje kwa wale ambao hawavai suruali lakini wana vitambi?
 
Siku za mwisho watajitokeza manabii wa uongo wengi sana,u can see hawana hata haya kujiita manabii pamoja na wake zao,make up you mind.
 
mh! anaongomba sana huyu mtu si kweli na nakataa, mimi ni mtu wa vibana makalio mwanzo mwisho lakini ikulu kahuna water wala maji mpaka nshomile wangu anachanganyikiwa, atafute kingine cha kutuambia
 
Mbona huku uswazi tunavaa madera full time na hatubanwi hata kidogo, ila vitambi utadhani mimba ya kujifungua?
 
Mbona mtaan kuna kina dada wamefungasha inye balaa na wanavaa suluari, vitambi wanawake hawafanyi mazoezi.
 
labda kweli....
wanawake wengi wanaopenda kuvaa suruali za kubana...
wanakuwa hwana wowowo....na wanakuwa na kitambi....
could be
Me nilikuwa sivai ila nimeanza mh itabidi niache mapema , maana tayari nimepigwa pasi ya uhakika. lol The Boss
 
Last edited by a moderator:
Inashangaza jinsi watu wanavyoweza kudanganywa na kudanganyika kirahisi namna hii. Au ndio matunda ya shule za yeboyebo? Huyo anayejiita Dr Ndodi ni muongo na tapeli mkubwa, hana hata chembe ya elimu ya tiba. Kinachomwezesha kuwafikishieni uongo wake ni uwezo wake wa kulipia vipindi vya TV ambao anaupata kutoka kwa wadanganyika. Biashara huria. Na wataalamu tuliowasomesha kwa kodi zetu wapo, wanakaa kimya huku tukiangamizwa na matangazo ya tiba feki. Nguvu ya pesa. Ni uleule ufisadi unaendelea kutuguguna. Wizi mtupu.

Wajinga ndio waliwao
 
Basi jana nikamsikiliza Dr. Ndodi, mwenye hospitali yake Itumbi Hoteli, kupitia Channel 5. Akafundisha mengi na kumalizia na yafuatayo:

1. Kwa kawaida protein/wanga ya/wa ziada husababisha vitambi kwa kina baba na maumbo makubwa(hasa makalio na mapaja) kwa kina mama. Kwa kuwa wanawake wakivaa suruali wanabana makalio na mapaja, hivyo protini/wanga ya/wa ziada hutaifadhiwa matumboni na hivyo kusababisha wanawake kuwa na vitambi.

2. Mbali na vitambi, kuvaa suruali husababisha ongezeko la maji "ikulu".

Mie nimelileta ili nipate kujuzwa kama kuna ukweli wowote juu ya madai haya.

Hiyo point ya kwanza,imenimaliza mbavu,hahhhahhaaaahha
 
Back
Top Bottom