Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Haki gani mkuu mbona hii thread ya 2013?Pumzika kwa amani kiongozi hatimae Haki yako imepatikanaa...!!
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Si ndio mkuu japo imecheleweshwaaa..!!Haki gani mkuu mbona hii thread ya 2013?
Waliohusika wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa.Haki gani mkuu mbona hii thread ya 2013?
Okay!Waliohusika wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa.
Ulikuwa mdogo au ulikuwa huijui JF au leo ni matanga😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭
Ulikuwa mdogo au ulikuwa huijui JF au leo ni matanga😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭
Nilikuwa na miaka 10 etiUlikuwa mdogo au ulikuwa huijui JF au leo ni matanga
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliyekuwa akipatiwa matibabu nchini Afrika Kusini amefariki dunia.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Bw. Assaa Rashid leo jioni (Jumanne, Novemba 12, 2013), Dkt. Sendongo Mvungi majira ya saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini akiwa katika Hospitali ya Milpark.
"Kwa masikitiko makubwa, Tume inawafahamisha wananchi kuwa Mjumbe wake, Dkt. Sengondo Mvungi aliyekuwa akipata matibabu katika Hospital ya Milpark iliyopo jijini Johannesburg-nchini Afrika Kusini amefariki dunia leo (Jumanne, Novemba 12, 2013) saa 8:30 mchana kwa saa za Afrika ya Kusini," amesema Bw. Rashid katika taarifa yake fupi ya awali.
"Taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka nchini Afrika Kusini kuja nchini kwa mazishi zinaendelea na taarifa zaidi zitatolewa kesho (Jumatano, Novemba 13, 2013)," ameongeza.
Marehemu Dkt. Mvungi alisafirishwa siku ya Alhamisi, Novemba 7, 2013 kwenda nchini Afrika Kusini kwa uchunguzi na matibabu zaidi akitokea Kitengo cha Mifupa Muhimbili (MOI) aliokuwa amelazwa baada ya kuvamiwa nyumbani kwake Kibamba, wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na watu waliomjeruhi vibaya kichwani usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, Novemba 3, 2013.
Katika taarifa yake, Tume pia imewaomba watanzania wote kuungana na familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Dkt. Mvungi katika kuomboleza msiba huo.
CHADEMA WATOA RAMBIRAMBI
Katiba nzuri yenye kubeba maoni, fikra, na mitizamo ya Wananchi walio wengi zaidi katika nchi Kamwe haijawahi kupatikana hivi hivi tu kwa urahisi, kuna gharama kubwa sana ya kulipa ya machozi, jasho na damu.Ni huzuni kwa Taifa kwani masahibu yaliyopelekea umauti yanatokana na kazi ya kuhuisha roho ya Taifa (Katiba ya Nchi). Mungu ailaze roho yake mahala pema.