Dr Shein: Anabaguliwa?

I think his talents are wasted on the political arena with a CV like that.
 

Dr Shein kama Dr Shein hana tatizo lolote. Tatizo lipo kwenye nafasi yenyewe ya Umakamu wa Rais. Kama mnakumbuka CCM wenyewe walichukua muda mrefu kuweka sawa namna Makamu wa Rais atakavyopatikana. Alikuwa ni Mwalimu ndiye aliwachimba 'mkwara' mzito ndipo wakaamua haraka haraka namna ya kumpata Makamu wa Rais. Mpaka leo Wazanzibari wengi hawaridhiki na namna Makamu wa Rais anavyopatikana. Wao walitaka Makamu wa Rais awe ni Rais wa Zanzibar.

CCM waliogopa hilo la Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Rais ukichukulia na upinzani mkali iliouonyesha CAF kabla ya uchaguzi wa 95. Kama Seif angeshinda Urais wa Zanzibar na kuwa Rais ni wazi angekuwa Makamu wa Rais (kama wazanzibari watakavyo) hivyo basi angekuwa ni Makamu wa Rais (kutoka upinzani) akiongozwa na Rais kutoka CCM. Hilo liliwaogopesha sana CCM na mwalimu alipokuja juu ndipo 'wakarukia' kuweka Makamu wa Rais kama mgombea mwenza bila kuainisha vizuri kazi zake! Anachokifanya Shein ni kile kile alichokuwa akikifanya Marehemu Omar Juma!

Shein kama Shein ni mchapa kazi. Kwenye serikali kama hii JK inayoongiozwa na 'mazomozi' unategemea Shein afanye nini zaidi ya kukaa kimya na kusubiri mshahara wake! Hata mimi ningekuwa yeye ningefanya hivyo hivyo. Huyu Shein ndiye Waziri pekee aliyeingia kwenye serikali ya Karume kutoka serikali ya Salmini mwanzoni ukiachilia akina Shamhuna waliokuja juzi juzi. Inasemekana Shein alikuwa ndiye (Naibu) Waziri pekee alioyeonyesha msimamo wa kumuunga mkono Amani tangu wakiwa katika Serikali ya Salmini.

Shein huyu huyu aliongoza Nchi vizuri tu wakati Mkapa akipata matibabu huko Uswisi ikiwa ni pamoja na kutengua maamuzi ya Prof Mwandosya ya kumuachisha kazi Kanali Nalingigwa aliyekuwa Mkurugenzi wa Tume ya Mawasiliano.

MWACHENI SHEIN WA WATU!
 


aw,aachwe aendelee kula mshahara bila kazi kwa sababu ana sifa ya kiongozi bora. Anyways, kila la heri mheshimiwa vice president.
 
aw,aachwe aendelee kula mshahara bila kazi kwa sababu ana sifa kiongozi bora. Anyways, kila la heri mheshimiwa vice president.

Mama si umeshaambiwa anafanya kazi. Wanamwita Mzee wa Mikasi (Ya kukata utepe lakini siyo ile mingine) Kwa watu walio karibu na Dk Shein wanasema ni mchapa kazi ila ni mtu asiyependa 'misifa'. Inawezekana kabisa JK hakupenda Shein awe Mgombea Mwenza na inawezekana kabisa System ya JK ilim-neglect Dk Shein siku za nyuma. We mwenyewe si uliona akina EL walivyokuwa wakitafuta umaarufu kwa kujipa 'urais mtarajiwa' Sasa Dk Shein angefanya nini? Tangu Lowassa aondoke madarakani JK amekuwa karibu sana na Shein kuanzia kwenye uteuzi wa Waziri Mkuu. Kumbuka Shein alikuwa Tanga na ikabidi aahirishe ziara ile. Ilivyo ni kwamba Shein anaweza naye akaanza kutafuta nguvu za kisiasa unategemea JK atamfanya nini AU watu wanataka tuje tushuhudie yale ya Rawlings wa Ghana na Makamu wake ya kutwangana ngumi hadharani? Kwenye nchi kama yetu ambayo ndiyo kwanza tuko darasa la kwanza kwenye Shule ya Msingi ya Demokrasia tunawahitaji watu kama Dk Shein. Angalia kule Rwanda ambako Rais alikuwa Pastor Bizimungu na Makamu wake Paul Kagame. Bizimungu alipotaka kutumia nguvu zake za Urais, Kagame akamuundia zengwe yuko wapi leo zaidi ya kuishia 'Lupango' anakooza na Kagame kampa masharti kwamba akitaka kutoka huko 'aape' kwamba hatajihusisha na Siasa! Angalia 'gomvi' la Thabo Mbeki na Makamu wake Rais Jacob Zumah! Shein angekuwa na uchu wa madaraka angeweza kujitengeneza akawa Zumah wa Bongo.

Kwa vurugu hizi za Wazenj kuhusu Muungano, tunawahitaji watu kama kina Shein na yule mtangulizi wake Omar Juma wenye siasa za mlengo wa kati. Kumbuka Salmini alivyoanza chokochoko ya kutaka kurudi madarakani, yule Marehemu alikuwa ni mtu wa kwanza kwa viongozi wa kitaifa 'kumrushia' makombora Komandoo na lile lilirahisisha kazi Ben kumtolea nje!
 
Ahhhh.., sielewi wala sioni huo uchapa kazi wake!

Yaani kwa jinsi mambo yanavyo kwenda kombo yeye anamsaidiaje JK? sidhani kama kukaa kwake kimya ni busara hata kidogo, tena huyu ni muoga ambaye hafai kabisa kuwa kiongozi! Yuko wapi katika kukemea woga wa mwenzake wa kuto taka kugusa mafisadi, kama yeye ni mtu safi amsaidie mwenzie ama apaaze sauti yake, 'he is not a baby by the way', kwanini asiseme? Tuache kumpaka viungo vya pilau kukubali kwake kugeuka boya manake hafai kuwa kiongozi period!
 

...same applies to the entirely CCM CC, NEC, (most) MPs, Prime Minister, Permanent Secretaries, Tanzania Ambassadors, etc etc
 
Ukiangalia harakaharaka utaona Shein anatengwa Hata mimi nimewahi kufikiri hivyo.
lakini katiba inampa nafasi ya Waziri mkuu kufahamika zaidi kuliko makamu wa raisi.Inawezekana kweli JK hampi nafasi sana shein but bado nafasi yake kama makamu wa raisi ipo pale pale.Kama tukienda juujuu unaweza kuuliza kwa nini Rice anaonekana ana nguvu kuliko makamu wa raisi.Ni mambo ya kiutendaji tuu haya ingawa anaonekana ceremonial!Who knowa kama haziivi na mkuu wa kaya?
 


yawezekana anafuata sera yao ya kukosoana vikaoni na anavyoonekana probably amesema sasa ameona haisaidii ameamua kuacha mambo yaende kama yatakavyokwenda!
 
Naomba kuuliza kuchapa kazi ni kuonekana kwenye vyombo vya habari? Maana sisi tunategemea habari kuwa anachapa kazi kwa matukio ya nje(Ziara). Pia kuna kazi za ndani mfano muda mwing hapa JF tunahoji Mkuu wa kaya anasafiri sana, files, na documents nyingine anapitia nani ambazo Mkuu wa kaya angetakiwa kupitia?

Pia hamna mmoja wetu anayeingia kwenye vikao vya mawaziri na kujua kuwa yeye anakaa tu kimya kwa haagizi mawazi husika kushughulikia maswala kama ufisadi n.k.

Kwangu sina cha kuchangia kuhusu Dr shein maana sina full info za utendaji wake. Habari nazotegemea ni TV, magazeti etc.. Kule ofisini kwa ndani sijui nini anafanya.
 
..Ofisi ya Makamu wa Raisi ina wizara zipi na bajeti kiasi gani?

..moja ya njia za kuipa nguvu nafasi ya makamu wa Raisi ni kuongeza wizara zitakazokuwa chini ya usimamizi wake.
 


kazi kweli kweli. Hata mimi niko puzzled kinamna.
 
Ni kweli kabisa kuna wapemba wana akili mahodari wa kazi na biashara kuliko waunguja
 
Dr. Shein ndiyo mtu wa pili kwa madaraka katika Tanzania. Hata hivyo, majukumu yake yameanishwa kwenye Katiba vizuri tu:

Sasa, atakuwa amebaguliwa au anabaguliwa endapo Rais akiondoka basi haruhusiwi kufanya kazi za Rais; kwamba maamuzi yeyote ya serikali hapewi taarifa; kwamba akimuita waziri yeyote kupata taarifa waziri huyo anagoma na kusema "namsubiri Rais" n.k Kuna ushahidi wa jambo la namna hiyo?

Kwamba Rais hajawahi kumwagiza kufanya jambo lolote kwa niaba yake na anaamua kumruka na kumpa Waziri mwingine au Waziri Mkuu wakati Makamu yupo na hana jingine la kufanya, hapo atakuwa amebagugliwa

Kwamba anakatazwa kumsaidia Rais kufanya shughuli mbalimbali za siku kwa siku. Kwa maneno mengine Makamu anaweza kumuita na kumhoji au hata kufuatilia jambo lolote linalomuangukia Rais siku kwa siku. Endapo kuna ushahidi kuwa Shein amekataliwa kufanya hilo jukumu lake la Kikatiba hapo tutasema amebaguliwa!

Na Waziri Mkuu je anakaribiana na cheo au majukumu na yale ya Makamu wa Rais?

Katiba inasema hivi (pamoja na mabadiliko yake ya baadaye)

Angalia tofauti ya majukumu yake na yale ya Makamu wa Rais kuhusu shughuli za Muungano.

Na pia Katiba inaongeza majukumu yafuatayo:


Sasa utaona kuwa kwa mtindo huu Waziri Mkuu atakuwa anasikika zaidi na kuonekana zaidi kwa sababu yeye ndiye anasimamia utekelezaji wa shughuli mbalimbali za serikali kila siku. Makamu wa Rais yuko kwenye "background".
 
Kuna uwezekano rais hamu-assign kazi vice president au anamuassign kazi ya kusoma mafile ambayo sio lazima tuione directly.
 
haitaji kum-assign kwani nafasi yake ni ya Kikatiba, anaweza kufanya jambo lolote ambalo anajua anamsaidia Rais na kwenye mambo mengine Rais anaweza kumuagiza kitu fulani, lakini kila asubuhi hasubiri maelekezo kutoka kwa Rais.

Ni kwa sababu hiyo utaona kuwa Rais aliamua kuweka wizara fulani chini ya VP, ile ya Mambo ya Muungano, Mazingira, n.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…