Elections 2010 Dr. Slaa aongoza kwa 73% - CACT

MIMI ITAKUWA YA PILI, mpaka sasa anakura mbili hata kama hatajipigia.

Mi pia nitampa kura Dr Slaa, Na mbunge na diwani wake.Mtu makini na mwenye kuona mbali kama mimi ni lazima apige kura ya mabadiliko na sio ya mazoea.Msiipigie CCM,maisha yatakua magumu kuliko miaka g iliyopita.ChaguaCHADEMA
 
Mi pia nitampa kura Dr Slaa, Na mbunge na diwani wake.Mtu makini na mwenye kuona mbali kama mimi ni lazima apige kura ya mabadiliko na sio ya mazoea.Msiipigie CCM,maisha yatakua magumu kuliko miaka g iliyopita.ChaguaCHADEMA


KURA ZENU MOJA MOJA ZINA MAANA KUBWA SANA, LAKINI ZITAKUWA NA FAIDA ZAIDI PALE MTAKAPO WASHAWISHI NA WATU WANAOWAZUNGUKA POPOTE PALE, IWE NYUMBANI, NYUMBA YA KUPANGA, BAR, KAZINI, SHULENI, KWENYE BUS AU DALADALA, STAND, HOTELINI NA KWINGINEKO. FAIDA YAKE NI USHINDI WA DR. SLAA (PHd).
 
Bullet
nilazima ujue kutofautisha tafiti za kisayansi na polls za media, hivi unajua ni watanzania wangapi wanaishi vijijini na hawana access na hizo media polls, ni aibu mkuu
Ukipita maeneo ya mijini na kuhoji watu hasa wasomi asilimia kubwa watakuambia wanataka upinzani, lakini je niasilimia ngapi kulinganisha na wa vijijini ambao wao CCM ni kila kitu,
Upinzania wanashindwa kuelewa nguvu ya CCM ipo wapi ili hali wanajua fika, Nguvu ya CCM ipo vijijini ambapo watu wakiamua wanaamua kweli na ndio maana hata hao wapinzani sehemu walizo shinda nyingi ni vijijini maana ukiwaelimisha wanakuelewa kweli na si kama mijini ambapo wapinzani wamepatolea macho na wanashindwa kupata majimbo mengi mijini.
Hivyo basi polls za media hazina ukweli wowote kitaalamu maana unaweza kuvote hata mara 100 ukiweza
Na kila chaguzi mambo huwa hivi hivi, kauli za watz waleo sio wa jana, wameamka nk. lakini mwisho wa siku matokeo ya tafiti kama za REDET ndio yanayotoa picha halisi ya matokeo ya uchaguzi
 
wewe hukuona jamaa wa REDET kuyatangaza alisema najua mtasema sana lakini habari ndio hiyo. huoni kama ile Tafiti imekaa kiumbea umbea!!
SI KWASABABU WANAONGOZWA NA MWANAMIPASHO (JK).. We unategemea nini hapo....!??
 
REDET ni mojawapo ya MASHINE ZA KUPUMULIA za CCM. Mashine za kwanza walizochomeka ziliisha chaji. Ama watahaha kwa aibu mwaka huu. Halo halo!!!!!

Kura yangu, ya mke wangu, nyumba ndogo zangu kadhaa, na wakwe zangu, shemeji zangu na wanangu zote zitaenda kwa DR. SLAA; ndoo mtajua hamna chenu mwaka huu.
 
in other words a sample can be named as not representing/reflecting population. this is a result of sampling error.

mfano kama unaenda kureserarch on watu ambao wana maradhi ya kansa na ukaenda hospital ya ocean road kila mgonjwa ukawa unamhoji sitashangaa kuona kwamba unaconclude kwamba asilimia 90 ya watanzania wanayo kansa. Huu utakuwa ni utapeli, ukilaza usikuwa na mfano.
 

Nakubaliana na wewe katika hili, watu wa vijijini ni waaminifu sana, mtu kama Mnyika angewekeza juhudi zake kuwapigania watu wa jimbo la Kijijini saiz angekuwa anasubiri kuapishwa tu lakini kwa longolongo za Watz wa mjini, usijeshangaa akapoteza tena!!
 
Kura za maoni ORIGINAL itakuwa Oktoba 31, 2010. Kiherere na mshawashwa wa nini?
 
Redep wanajinyonga na kujidhalisha wao wenywe huku nyuma niliwahi kuhoji QMS yao (quality management system yao) In short REDEP ni garbage IN garbage OUT. Hata kwenye recycle bin hawafahi.
 



HA HA HA HA HA HA HAAA!!! nikumbushe ile hospital alolazwa mwl.nyerere. thats where CCM spend their last time.
 
Inawezekana Redet walijisahau wakasoma matokeo KINYUMENYUME. Matokeo halisi yalipaswa kuwa Slaa; 68%, Kikwete; 12%, Lipumba; 10%, Waliobaki 10%.
 

Hiyo ni kampuni hewa, mpaka sasa ofisi zake hazijukani
 

Naona wewe hujui kinachoongelewa hapa ndo maana unadiriki kusema REDET ni watafiti. kama wewe ni mwanaccm sina haja ya kukuambia chochote maana wafuasi wa ccm ni watu wenye njaa na uwezo mdogo sana wa kuelewa kiasi kwamba hawezi kuhoji chochote juu ya maisha kama vile wafuasi wa dini. Lakini kama umepungukiwa ufahamu juu ya REDET kwa bahati mbaya naomba uende pale UDSM ukatafiti kuhusu REDET na hapo ndipo utajua jinsi REDET ilivyoanzishwa, utajua pia uhusiano uliopo kati ya Benson Bana, Rwekaza Mkandala na Kikwete pia utajua malengo ya kuanzishwa REDET. Utajua pia sample wanayotumia REDET ktk kukusanya maoni inatakiwa kuwa na sifa gani.
Utapata jibu pia kwamba ni kwanini ktk utafiti(uchwara) wa REDET uliopita ilionekana waTZ wengi hupata habari zao kwa kupitia gazeti la Daily news.
 
REDET wamewadhalilisha wasomi na wahadhiri wa vyuo vikuu. Nashiwishika kufikiria kwamba kama wasomi na wanataaluma wa vyuo vikuu ambao ndiyo tegemeo kwa tafiti mbalimbali ndani ya nchi wanadhubutu kutoa taarifa ya namna hii, basi si ajabu kwa wasomi hao kuvurunda mara waingiapo katika nyanja za siasa. Tumewaona maprofessor wengi waliopewa nafasi kubwa serikalini zikiwemo za uwaziri wakifanya madudu ya waziwazi, kumbe ni maprofessor waliopata hizo nafasi kutokana na kupika data na kutumiwa na wanasiasa. Ndiyo maana hawana uwezo wa kufanya la maana wakiwa kwenye nafasi zao.

Kwa namna nyingine naona kama vile REDET imetumiwa kisiasa na CCM Ili kuwaandaa wananchi kisaikolojia kwa ajili ya kupokea matokeo yatakayochakachuliwa na CCM mwezi wa kumi. Maana kama REDET wasingetoa matokeo haya, ni dhahiri kwamba watanzania wasingekubaliana na matokeo yoyote yanayoonyesha kwamba Dr Slaa ameshindwa. Lakini pia kwa mtizamo huu wa kusambaza message ya kuchafuana and the likes, naamini kwamba uwezekano wa kuzipiga mwaka huu unabaki kuwa mkubwa sana. Mungu atuepushie mbali na hilo.
 

Kwani hujashangaa kisa cha NKASI, mtafiti anasema asilimia 100% Ukistajaabu ya Musa...utayona ya REDET=CCM B
 


Nakubaliana na wewe.

Nimesahau kutumia msemo wa 'No research no right to speak'.
 

Ndugu yangu usiidhalilishe sayansi, utafiti wa REDET sio wa kisayansi kwa sababu kisayansi kuna aina tofauti za sampling na kila aina ina mazingira yake. REDET wametumia random sampling. Aina hii ya sampling huweza kutumiwa katika mazingira ambayo sample space yake haina mgawanyiko mkubwa na kikawaida ni ndogo mfano unapotaka kujua wanafunzi katika darasa fulani la shule let say ya seminari wanapenda kusomea aina gani ya kazi hapo unaweza kutumia random sampling maana ktk darasa hilo migawanyiko sio mikubwa. Lakini katika sample space kama nchi nzima ya TZ ambamo kuna tofauti za kijinsia, kidini, kikabila, kiuchumi, kielimu na kimtazamo ni mbumbumbu tu ndiye anayeweza kutumia random sampling na hivyo utafiti kama huo hauwezi kuwa wa kisayansi hata kidogo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…