Elections 2010 Dr Slaa asante kwa kukubali kutuongoza ukiwa rais wa Tanzania na watanzania

13. Kawe, 14: Ulanga kwa Prof. Mlambiti,

Ni vema kuwa tunatoa matokeo halali wala si tetesi au awali. ITV sasa hivi wametangaza matokeo ya ulanga, kilosa.
majimbo yote mawili yameenda CCM. Prof. Mlambiti amekuwa wa pili kwa matokeo.
Matokeo ya Kawe bado tunasubiri ingawa kuna uwezekano mkubwa Halima Mdee anaweza kushinda
 

Unamaanisha kujitolea kugombea au amechaguliwa kuwa rais, maana mimi sikuelewi.
Matokeo ya Urais bado na kwa yale yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi jana katika majimbo 14 yaliyotangazwa JK wa CCM anaongoza kwa kura nyingi sana katika majimbo 12 ambapo Slaa kashinda jimbo moja na Lipumba nae moja. Mambo bado magumu kwa wapinzani katika Urais. Tuwe wavumilivu kupata matokeo rasmi
 
Tunashukuru kwa taarifa lakini nasikitika kukuambia kuwa Shinyanga mjini limerudishwa kwa CCM hivyo kusababisha mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga kujiuzulu na wananchi kuchoma moto ofisi za manispaa ya Shinyanga. Na kukutaa matokeo kwa Masha kulisababisha maelfu ya watu kufanya fujo ikiwa ni pamoja na kuichoma moto ofisi ya CCM Nela hapa jijini Mwanza.

Ilemela imemalizika vizuri kabisa baada ya Diallo kukubali kusaini mapemaaa bila tatizo lolote.

Chademaaaaaa oyeee!!!!!!!!!!!!!!
 
Mtazamo chanya kama huu unanenepesha mifupa na kuleta faraja na matazamio ya namna ya pekee; hii ni sala ya namna ya pekee inayotolewa na wazalendo wa nchi hii wakati ambapo ni dhahiri timu ya NEC imeshaanza kuchakachua kura za watanzania kwa Dr Slaa na watanzania. Tuendelee kumlilia MUNGU ili muujiza wa namna fulani utokee, mafisadi waaibike.

MUNGU Ibariki Afrika MUNGU Ibariki Tanzania; MUNGU Kibariki CHADEMA!
 
Mtazamo chanya wakati ambapo JK na timu yake ya NEC wanachakachua kura za thamani zilizopigwa na watanzania waliochoka na CCM na ufisadi wake; kura zilizopigwa ili kumuinging Dr Slaa madarakani. Shukrani hii kwa Dr Slaa ni sala ya pekee ya imani kwa ajili ya kuhakikisha uchakachuaji haufanikiwi. Tuombe bila kukoma, ili uchakacuaji unaoendelea hivi sasa usifanikiwe.

MUNGU ibarikin Africa; MUNGU ibariki Tanzania na CHADEMA! Amen!
 

Msengapavi, unazidi kugusa machozi yangu ya furaha, kwa jinsi Dr Slaa alivyojitoa kuwa Rais, unaniliza zaidi, asante.
 
Kiongozi wa kweli huitwa na watu awatumikie , dr slaa aliitwa akaomba ridhaa ya wana wa karatu wakakubali kutupa watanzania zawadi ya kiongozi wa ukweli. Wabarikiwe sana wooote, wanazuoni, wana wa karatu na watanzania kwa ujumla. Mungu bariki taifa letu tanzania.

Amen
 

Sawa Mujungu, Dr. Slaa aliitwa kuwa Rias wa Tanzania na Watanzania akaitika ili kuwahudumia raia wake na kurudisha heshima ya nchi yetu iliyopotea kwa sababu ya ufisadi na umoja unaomomonyoka kwa sababu ya CCM na timu ya kampeni ya JK.
 
Jamani mbona mnataka kunichanganya tena!

Mimi najua Maswa Magh/Mash ndiyo zimeenda CHADEMA. Hii ya BARIADI kwa Wanyantuzu sijaipata bado au umechanganya badala ya Maswa umesema Bariadi???
Nahitaji Details please.
 

Rais wa Tanzania na Watanzania ni Dr. Slaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…