Dr. Slaa: Kikwete mmiliki wa DOWANS...

Baba yetu Dk Slaa wa ukweli emu endelea kukanyaga icho kichwa cha wenda wazimu coz uku uraiani tushachoka! usiache kitu maana hana cha kujitetea, ndo mana siku izi hata kutoka OUT haendi tena!

Yan nakuomba usiache chochote, we toa tu coz raia tushaelekeza tumaini letu lote kwako, huyu jamaa hana nia nzuri na sisi, Afu ningeomba hii issue ya katiba ifanyiwe kazi very early once bunge likianza afu uwape ramani nzima vijana wako bungen where to start and how to tackle the situation ili wasibabaike, isitoshe tunawaamini mabro zetu wote walioko mjengoni kuwa wote wameenda shule na wamekomaa kweli na kitabu na si cha kubabaisha km hao madokta wa gentle men digriz, we watumie vizuri, naamini kauli mbiu yetu ya kuwa MWAKA 35 NI WA KUZIKA CCM NA MWAKA WA 36 NI KUANUA MATANGA itatimia tu!.

Big up mzee for your real uzalendo of this blessed nation but rich with corrupted leaders like Kikwetes.
 
Kesi ya Dowans yaiva Dar

• Pingamizi la wanaharakati kuanza kusikilizwa Mahakama Kuu

na Mwandishi wetu

HATIMAYE Kituo cha Msaada wa Kisheria na Haki za Binadamu (LHRC) kwa kushirikiana na mashirika 16 ya wanaharakati wamepokea hati ya kuanza kusikilizwa kwa pingamizi lao la kupinga nia ya serikali kutaka kuilipa fidia ya sh bilioni 94 Kampuni ya Dowans.

Novemba 15, mwaka jana Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara (ICC), chini ya Mwenyekiti Gerald Aksen na wasuluhishi, Swithin Munyantwali na Jonathan Parker iliamuru TANESCO iilipe Dowans fidia ya sh bilioni 94 kwa kuvunja mkataba baina yake na kampuni hiyo kinyume cha sheria.

Kufuatia uamuzi huo, Januari 25 mwaka huu Dowans iliwasilisha Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam maombi ya usajili wa tuzo yake hiyo kupitia kwa Wakili wake, Kenedy Fungamtama, ili ulipwaji wa fidia yake hiyo ufanyike kisheria.

Maombi hayo ya Dowans yalikwisha kusajiliwa na kupewa namba ya usajili wa madai namba 8 ya mwaka 2011, na tayari yameshapangiwa jaji wa kuyasikiliza.

Lakini LHRC kwa niaba ya mashirika mengine ya wanaharakati waliwasilisha rasmi pingamizi lao wakiainisha hoja za msingi saba kupitia Kampuni ya uwakili ya South Law Chambers Advocates.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu, Mkurugenzi wa Ushawishi na Utetezi wa LHRC, Harold Sungusi, alisema wamepokea hati hiyo ya kuitwa mahakamani na kwamba kesi yao imepangwa kuanza kusikilizwa Machi 2, mwaka huu.

Alisema kesi hiyo ilipangiwa jaji aliyemtaja kwa jina moja la E. Mushi, bila kutaja ni namba ngapi iliyopewa.

Katika hoja ya kwanza ya pingamizi hilo, wanaharakati hao wanadai kuwa hawakuridhika na tuzo hiyo iliyotolewa na ICC kwa Dowans kwani TANESCO ni shirika la umma linalomilikiwa na Serikali ya Tanzania.

Walidai kuwa ingawa TANESCO inaendeshwa kwa fedha zinazotokana na huduma zake, lakini sehemu ya fedha hizo zinatokana na Watanzania walipa kodi.

Katika hoja ya pili wanadai kuwa hakuna mkataba wa kisheria uliofungwa baina ya TANESCO na Kampuni ya Dowans uliosababisha kuwepo kwa mgogoro ulioilazimu ICC kutoa tuzo hiyo kwa kampuni hiyo.

Sambamba na hoja hiyo, wanaharakati hao wameambatanisha na mkataba baina ya TANESCO na Kampuni ya Richmond ambao Dowans iliurithi, unaodaiwa kuwa na mashaka kisheria, kama kielelezo.

Hoja ya tatu wanadai kuwa chini ya sheria za Tanzania, mkataba na tuzo hiyo kwa Dowans ni batili na umejaa dosari za kisheria.

Katika hoja ya nne, wanaharakati hao wanadai kuwa chini ya sheria za Tanzania, Kampuni ya Richmond haikuwa na nguvu ya kisheria kuingia mkataba na Serikali ya Tanzania au na TANESCO kwa niaba yake ambao unaweza kutekelezwa.

Wanaharakati hao wametia nguvu hoja yao hiyo kwa kuambatanisha na kielelezo cha taarifa ya matokeo ya uchunguzi wa Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza uhalali wake.

Wanaharakati hao wanadai katika hoja yao ya tano kuwa kutokuwepo kwa mkataba hai kati ya Richmond na TANESCO, jukumu lilitakiwa kutekelezwa na wajibu pingamizi wa kwanza na wa pili, ambalo ndilo lilisababisha kutolewa kwa tuzo hiyo kuwa batili.

Hivyo, kwa mazingira hayo, wanaharakati hao katika hoja yao hiyo wanadai kuwa tuzo hiyo iliyotolewa na ICC haiwezi kukubaliwa wala kutekelezwa na uamuzi wa Mahakama Kuu ya Tanzania.

Hoja ya sita ya pingamizi hilo, wanaharakati hao wanadai kuwa tuzo hiyo ilitolewa hata kabla ya mgogoro mwingine katika mahakama nyingine ya Houston nchini Marekani, baina ya Richmond na Dowans Tanzania Limited juu ya umiliki wa mashine za kuzalishia umeme, ambazo zinahusiana na tuzo hiyo.

Katika hoja ya saba ya pingamizi hilo, wanaharakati hao wanadai kuwa maombi ya usajili wa tuzo iliyotolewa na ICC ambayo yamewasilishwa Mahakama Kuu hayapaswi kukubaliwa kwa kuwa imetokana na mkataba batili baina ya Richmond na TANESCO.

Hoja za wanaharakati hao zitakuwa zikikabiliana na hukumu ya ICC ambayo kwenye ukurasa wa 89 majaji watatu waliotoa uamuzi huo walitamka kuitambua Richmond Development Company LLC kuwa ni kampuni halali kwa mujibu wa sheria za Texas, Marekani, kinyume cha ilivyotafsiriwa na Kamati Teule ya Bunge.

Katika kukazia hukumu hiyo ya ICC, majaji hao watatu walitumia hukumu mbalimbali za siku zilizopita za huko Texas zilizotumia kile walichokieleza kuwa ni ‘parole evidence' katika kuhalalisha uwepo wa Richmond kisheria huko Texas na hivyo kuufanya mkataba wake na TANESCO kuwa halali.

Wakati ICC ikikubaliana kwamba Richmond Development Company, LLC ni jina la kibiashara la RDEVCO, LLC, Kamati Teule ya Bunge katika ripoti yake ilieleza bayana kwamba uchunguzi wao walioufanya Texas kwa kushirikiana na taasisi za kisheria za huko ulithibitisha kwamba kampuni hiyo ilikuwa haina hadhi ya kuwa kampuni halali.

Mbali ya hiyo, ICC katika ukurasa wa 41 wa hukumu yake hiyo inasema taratibu za kuhamishwa kwa mkataba kutoka Richmond kwenda Dowans zilizingatia sheria za Tanzania na kwamba ziliridhiwa na TANESCO.

ICC inaeleza kuwa Desemba 4, 2006 Dowans Holdings SA (Costa Rica) iliiandikia barua TANESCO ikieleza kwamba ilikuwa inakusudia kuanzisha na kusajili kampuni nchini itakayoendesha na kusimamia utekelezaji wa majukumu ya RDEVCO.

Hukumu hiyo katika ukurasa wa 54 inaonyesha kwamba Desemba 21, 2006, TANESCO waliridhia uhamishwaji wa mkataba wa Richmond kwenda Dowans, hali ambayo iliiwezesha kampuni hiyo ya Costa Rica kuanza kuzalisha umeme wa awali wa megawati 20 kuanzia Januari 26, 2007.
 
Mitambo ya Dowans kuwashwa

Tuesday, 15 February 2011
Mwandishi Wetu

MITAMBO ya kuzalisha umeme wa dharura ya Dowans iliyoibua mjadala mpana katika jamii kutokana na utata wa mkataba wake, huenda ikawashwa wakati wowote kwa malengo ya kupunguza tatizo la mgawo wa umeme linaloendelea nchini.

Habari zilizopatikana jana mjini Dodoma na kuthibitishwa na baadhi ya wabunge waliohudhuria kikao cha Kamati ya Nishati na Madini walisema kuwa hoja ya kuwashwa kwa mitambo hiyo ilijadiliwa kwa lengo la kupunguza makali ya umeme nchini.

Chanzo chetu cha habari kilisema kwamba wajumbe wa kamati hiyo walikuwa wakijadili ama waitaifishe mitambo hiyo au waingie mkataba wa dharura ili ianze kutoa umeme kwa siku mbili zijazo.

"Suala lililozua mvutano baina ya wabunge ni ama kutaifisha au kuwapo mkataba wa dharura na kampuni inayomiliki mitambo hiyo,"alisema mbunge mmoja aliyekuwapo katika kikao cha kamati hiyo.

Vyanzo hivyo vya habari vilieleza Mwananchi kuwa mpaka jana usiku kikao kilikuwa kikielendea na kwamba baada ya kumaliza kikao hicho wangeshauriana na Spika wa Bunge kueleza msimamo wao.

Alipoulizwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, January Makamba kilichokuwa kikijadiliwa ndani ya kikao, alisema : " Kikao bado kinaendelea. Tutashauriana na Spika baada ya hapa. Tunatarajia kufanya maamuzi yenye maslahi ya kwa nchi nzima."

Awali jana asubuhi wakizungumza katika kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 , Makamba, Waziri Kivuli wa Nishati na Madini, John Mnyika walipendekeza yafanyike maamuzi magumu ili kuwezesha mitambo ya Dowans kuwashwa ili kupunguza makali ya mgao.

Kwa mujibu wa Makamba, mitambo ya Dowans inazalisha MW 120 na itasaidia kupunguza makali ya mgao kwa asilimia 60 mpaka 70. Wote walitambua uwepo wa suala la Dowans mahakamani.

Hata hivyo, Mnyika alipendekeza sheria ya uhujumu uchumi itumike katka suala la Dowans huku akisema kuwa hawezi kwenda ndani zaidi.

Mniyka alimaanisha kuwa mitambo ya Dowans inapaswa kutaifishwa kwa sababu ya ukweli kuwa mkataba wa Dowans/Richmond ni wa kitapeli na huwezi kuwa na mgawo wakati mitambo iko pale imezimwa.

Wakati huo huo, Makamba alipendekeza kuwa usainiwe mkataba wa muda mfupi wa miezi mitatu na hao wenye mitambo ili kuiwezeshwa kuwashwa.

Alipendekeza uangaliwe utaratibu ambao hautaathiri kesi iliyopo Mahakamani.

 
Tatizo la hii serikali ni kuwa mitambo ya DOWANS kwa mujibu wa hukumu iliyotolewa TEXAS MAREKANI kati ya DOWANS na RICHMOND gharama za kununuwa mitambo hiyo ni kiasi cha dola za marekani 15 milioni tu na zipo hazihitaji order kuzipata......................kinachoizuia serikali hii ya wahuni kununua mitambo mipya kwa hizo fedha na kuendelea kushirikiana na kikundi cha kifisadi cha DOWANS ni nini?

Do we really know GOD or we are mere hypocrites?
 
Mnyika: Dowans wafute fidia ICC
• Asema hilo litaepusha mitambo yao kutaifishwa

na Mwandishi wetu


WAZIRI Kivuli wa Nishati na Madini, John Mnyika (CHADEMA) amewataka wamiliki wa Kampuni ya kuzalisha umeme ya Dowans kujitokeza hadharani na kufuta fidia ya shilingi bilioni 94 ambazo wanatakiwa kulipwa na Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (TANESCO).
Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ubungo, alisema iwapo wamiliki hao wa Dowans wataweza kutekeleza pendekezo lake la kufuta fidia hiyo iliyoamriwa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICC) wanaweza kuiokoa mitambo yao ya kuzalisha umeme iliyopo Dar es Salaam kutotaifishwa.
Mbunge huyo kijana, alisema mbali ya kufuta kwa hiari yao fidia hiyo, wamiliki hao wa Dowans wanapaswa kukiri pia kwamba walirithi mkataba wenye utata wa Richmond kwa kupotoshwa na kampuni hiyo na vyombo vya serikali.
Alisema anaamini iwapo Dowans watafanya hivyo, basi wanaweza kujijengea uhalali wa kuingia mkataba mpya wa kuzalisha umeme na TANESCO.
"Kampuni ya Dowans kama inataka kuepusha kutaifishwa basi wamiliki wake popote pale walipo duniani wajitokeze hadharani wakiri kwamba walipotoshwa na Richmond pamoja na vyombo vya kiserikali wakati wa kuhamishwa mkataba ili wajijengee uhalali wa kufanya majadiliano, ikiwamo ya kufuta madai ya fidia inayotaka kutolewa kwa mujibu wa hukumu ya ICC," alisema Mnyika katika taarifa yake ya maandishi kwa vyombo vya habari aliyoitoa jana.
Mnyika alilazimika kutoa taarifa hiyo ili kusahihisha habari zilizochapwa katika gazeti moja la kila siku jana (si Tanzania Daima), ambalo lilimkariri mbunge huyo akitaka Dowans ipewe mkataba wa miezi mitatu wa kuzalisha umeme ili kupunguza makali ya mgawo wa umeme.
"Sijawahi kutoa kauli popote ya kushauri Dowans ipewe mkataba wa miezi mitatu kama ilivyonukuliwa na chombo kimoja cha habari," alisema Mnyika.
Mbunge huyo alisema katika kauli yake iliyonukuliwa kwa makosa kutokana na mahojiano aliyoyafanya juzi kupitia TBC, alisema aliitaka serikali itumie sheria hususan ya uhujumu uchumi kuiwasha mitambo husika (Dowans) kwa masilahi ya taifa.
"Ningependa kutumia fursa hii kusisitiza mtazamo wangu kwamba ni muhimu ili kupunguza adha ya mgawo wa umeme, serikali itumie mamlaka yaliyopo kwenye Katiba na sheria ikiwemo sheria ya uhujumu uchumi, sheria ya kupambana na rushwa, sheria ya mali zilizopatikana isivyo halali itaifishe mitambo hiyo haraka iwezekanavyo na kuiwasha kwa masilahi ya umma," alisema Mnyika katika tamko lake la maandishi jana.
Akiendelea, Mnyika alisema kwamba Kampuni ya Dowans ilirithi mkataba kutoka Kampuni ya Richmond ambayo ilithibitishwa kwa maazimio ya Bunge kuwa ilipata mkataba katika mazingira ya ukiukwaji wa sheria, ikiwamo sheria ya kupambana na rushwa.
Mbali ya hilo, Mnyika alieleza pia kwamba hata kampuni yenyewe ya Dowans imeonekana kuwa na utata katika usajili, umiliki na uhamishaji wa mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura kutoka Richmond.
Mnyika alisema pia kwamba wananchi wanapaswa kutambua kuwa kiasi cha megawati 120 za Dowans hakiwezi kuziba pengo la takriban megawati 240 ambalo linalikabili taifa hivi sasa.
Alisema kwa sababu hiyo basi Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, anapaswa kutoa maelezo ya kina kuhusu hatua ambayo serikali inataka kuchukua ya kukodi mitambo ya MW 260.
"Waziri atoe ufafanuzi wa kutokukamilika kwa mipango ya serikali wakati ambapo dharura ya umeme ilijulikana tangu mwaka 2002, serikali ikaijadili kwa kina mwaka 2006, Bunge likapitisha maazimio mwaka 2008 na serikali ikaahidi tena mwaka 2009 kuweka utaratibu wa kukabiliana na dharura hiyo," alieleza Mnyika, mmoja wa wabunge vijana makini katika kujenga hoja na kuchanganua mambo.
Mbunge huyo wa Ubungo alisisitiza haja ya Bunge kupatiwa fursa ya kujadili kwa kina suala la umeme katika mkutano unaoendelea wa Bunge kama jambo la dharura ili kuweza kulinusuru taifa.
Mnyika ambaye nia yake ya kutaka suala hilo la mgawo wa umeme lijadiliwe kwa dharura ndani ya Bunge juzi ilipingwa na Spika wa Bunge, Anne Makinda, akisema alikuwa akikusudia kutoa tamko lake rasmi wakati wowote.
"Nitatoa tamko la kina hivi karibuni kwa nafasi yangu ya uwaziri kivuli kuhusu suala la umeme, kwa kuzingatia hali ya mgawo inavyoendelea sanjari na kupanda kwa gharama za nishati hiyo kunakoongeza ugumu wa maisha kwa Watanzania walio wengi baada ya majadiliano na baraza kivuli na mamlaka nyingine husika," alisema.
 
Mnyika amkaanga Waziri Ngeleja kuhusu umeme Send to a friend Wednesday, 16 February 2011 21:16

Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika

Boniface Meena
MBUNGE wa Ubungo (Chadema), John Mnyika amemtaka Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja atoe maelezo ya kina kuhusu hatua ambayo serikali inataka kuchukua ya kukodi mitambo ya kuzalisha megawati za umeme 260 ili kuziba pengo la takribani megawati 240 ambalo linakabili taifa kwa sasa.

Mnyika alieleza hayo jana akimtaka waziri Ngeleja atoe ufafanuzi wa kutokukamilika kwa mipango ya serikali wakati ambapo dharura ya umeme ilijulikana toka mwaka 2002, serikali ikaijadili kwa kina mwaka 2006, bunge likapitisha maazimio mwaka 2008 na serikali ikaahidi tena mwaka 2009 kuweka utaratibu wa kukabiliana na dharura hiyo.

"Ni muhimu kwa Waziri wa Nishati na Madini kutoa maelezo ya kina kuhusu hatua ambayo serikali inataka kuchukua ya kukodi mitambo ya MW 260. Aidha, Waziri atoe ufafanuzi wa kutokukamilika kwa mipango ya serikali,"alisema Mnyika.

Alisema katika muktadha huo ni muhimu kwa bunge likapata fursa ya kujadili kwa kina suala la umeme katika mkutano unaoendelea wa bunge kama jambo la dharura ili kuweza kulinusuru taifa.

Hata hivyo tayari Spika wa Bunge, Anne Makinda ameishatoa msimamo kwamba suala la uhaba wa umeme halitajadiliwa na katika kikao cha bunge kinachoendelea mjini Dodoma na badala yake ameiagiza Kamati ya Nishati na Madini ya Bunge kuliofanyia kazi suala hilo.

Spika alitoa msimamo huo juzi kufuatia hoja ya dharura ya Mnyika aliyetaka bunge kujadidi suala la umeme mara baada ya Ngeleja kutoa kauli ya Serikali bungeni kuhusu suala hilo.

Katika maeleo yake bungeni, Ngeleja alitaja orodha ndefu ya miradi ya serikali inayotarajiwa kukamilika katika muda wa kati ya miaka miwili hadi sita, huku akibainisha kuwa ili kulikabili tatizo la sasa kuna mpango wa kukodi mitambo ya kuzalisha megawati 260 za umeme ili kufidia pengo lililopo hivi sasa.

Jana katika taarifa yake, Mnyika alisema ikumbukwe kwamba kampuni ya Dowans ilirithi mkataba toka kampuni ya Richmond ambayo ilithibitishwa kwa maazimio ya bunge kuwa ilipata mkataba katika mazingira ya ukiukwaji wa sheria ikiwemo sheria ya kupambana na rushwa.

Alisema suala zima likitazamwa kwa undani wake yakirejewa yaliyojiri Costa Rica na Tanzania, hata kampuni Dowans kuna utata kuhusu usajili, umiliki na jinsi ilivyorithi mkataba wa kuzalisha umeme kutoka Richmond.

"Kampuni ya Dowans kama inataka kuepusha kutaifishwa basi wamiliki wake popote pale walipo duniani wajitokeze hadharani wakiri kwamba walipotoshwa na Richmond pamoja na vyombo vya kiserikali wakati wa kuhamishwa mkataba, ili wajijengee uhalali wa kufanya majadiliano ikiwemo ya kufuta madai ya fidia inayotaka kutolewa kwa mujibu wa hukumu ya ICC,"alisema Mnyika.

Alisema mtazamo wake ni kwamba ili kupunguza adha ya mgawo wa umeme serikali itumie mamlaka yaliyopo kwenye katiba na sheria ikiwemo sheria ya uhujumu uchumi, sheria ya kupambana na rushwa, sheria ya mali zilizopatikana isivyo halali itaifishe mitambo hiyo haraka iwezekanavyo na kuiwasha kwa maslahi ya umma.

"Nitatoa tamko la kina hivi karibuni kwa nafasi yangu ya uwaziri kivuli kuhusu suala la umeme kwa kuzingatia hali ya mgawo inavyoendelea sanjari na kupanda kwa gharama za nishati hiyo, kunakoongeza ugumu wa maisha kwa Watanzania walio wengi baada ya majadiliano na baraza kivuli na mamlaka nyingine husika,"alisema.

Juzi mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura ya Dowans iliyoibua mjadala mpana katika jamii kutokana na utata wa mkataba wake, ilitangazwa huenda ikawashwa wakati wowote kwa malengo ya kupunguza tatizo la mgawo wa umeme linaloendelea nchini.

Habari zilizopatikana juzi mjini Dodoma na kuthibitishwa na baadhi ya wabunge waliohudhuria kikao cha Kamati ya Nishati na Madini zilieleza kuwa hoja ya kuwashwa kwa mitambo hiyo ilijadiliwa kwa lengo la kupunguza makali ya umeme nchini.

Chanzo chetu cha habari kilisema kwamba wajumbe wa kamati hiyo walikuwa wakijadili ama waitaifishe mitambo hiyo au waingie mkataba wa dharura ili ianze kutoa umeme kwa siku mbili zijazo.

"Suala lililozua mvutano baina ya wabunge ni ama kutaifisha au kuwapo mkataba wa dharura na kampuni inayomiliki mitambo hiyo,"alisema mbunge mmoja aliyekuwapo katika kikao cha kamati hiyo.

Vyanzo hivyo vya habari vilieleza Mwananchi kuwa mpaka juzi usiku kikao kilikuwa kikielendea na kwamba baada ya kumaliza kikao hicho wangeshauriana na Spika wa Bunge kueleza msimamo wao.

Alipoulizwa Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, January Makamba kilichokuwa kikijadiliwa ndani ya kikao, alisema : " Kikao bado kinaendelea. Tutashauriana na Spika baada ya hapa. Tunatarajia kufanya uamuzi wenye maslahi ya kwa nchi nzima."

Awali jana asubuhi wakizungumza katika kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1 , Makamba, Mnyika alipendekeza ufanyike uamuzi mgumu ili kuwezesha mitambo ya Dowans kuwashwa ili kupunguza makali ya mgao.

Kwa mujibu wa Makamba, mitambo ya Dowans inazalisha MW 120 na inaweza kusaidia kupunguza makali ya mgao kwa asilimia 60 mpaka 70. Wote walitambua uwepo wa suala la Dowans mahakamani.

Hata hivyo, Mnyika alipendekeza sheria ya uhujumu uchumi itumike katka suala la Dowans huku akisema kuwa hawezi kwenda ndani zaidi.

Mnyika alimaanisha kuwa mitambo ya Dowans inapaswa kutaifishwa kwa sababu ya ukweli kuwa mkataba wa Dowans/Richmond ni wa kitapeli na huwezi kuwa na mgawo wakati mitambo iko pale imezimwa.

Wakati huo huo, Makamba alipendekeza kuwa usainiwe mkataba wa muda mfupi wa miezi mitatu na hao wenye mitambo ili kuiwezeshwa kuwashwa.

Alipendekeza uangaliwe utaratibu ambao hautaathiri kesi iliyopo Mahakamani.



Comments




0 #4 mama Twins 2011-02-17 07:19 Hivi huyo Anna Makinda anaelewa vizuri maana ya BUNGE??????????? Ni kwanini wambunge watake kuleta hoja bungeni halafu spika akatae???? nini kimejificha hapo?
Quote









+1 #3 elibariki yerald 2011-02-17 06:28 KAZA BUTI KAKA ILA MABOMU YALIYOLIPUKA JANA SERIKALI YOTE IJUZULU INAKUWAJE KILA SIKU MADUDU YALEYALE? WAATHIRIKA WA MBAGALA HAWAJALIPWA FIDIA STAHIKI LEO ,,TENA GONGO LA MBOTO?


TUANDAMANE NCHI NCHI WALIOHUSIKA WAJIUZULU NA KIONGOZI MKUU PIA MAANA WAMESHINDWA KUYAHIFADHI MAISHA YETU, NA WAMETUWEKA REHANI?, WANAPIGANA VIJEMBE TU BUNGENI WAKISAHAU MAMBO YA MSINGI NA KULIPUKA HUKO KWA MABOMU SABABU MOJAWAPO NI KUKATIKATIKA KWA UMEME,,,TWENDE MBELE HAIWEZEKANI MBONA WANACHEZEA MAISHA YETU?

Quote









0 #2 Mhifadhi 2011-02-17 05:28 Kuendelea kutegemea umeme wa maji ni kuendelea kukaribisha umasikini huu kila siku. Swala la mabadiliko ya tabia nchi halitatuacha tufaidi hiyo rufiji. Unaweza kushangaa kukuta rufiji ikiwa haina maji ya kuzalisha hata 100MW baada ya muda mfupi takribani miaka 15. Ni wakati wa kujifunga kibwebwe na tuhamue kutumia teknolojia mbadala kama zile za kinyuklia na hayo makaa ya mawe japo twajua yachafua mazingira kiasi kama tusipoyatumia kwa teknolojia muafaka. Lakini nionavyo serikali ama watendaji wake wataendelea na uzembe huu ili mradi kuwe na dharura maana humo ndipo penye maslahi binafsi. Ni aibu sana kwa taifa
Quote









0 #1 kunji 2011-02-17 04:56 Jamani, wanasihasa na wataalam wote wa maji na nishati. Tanzania inayo hazina nzuri ya bonde katika mto Rufiji, Stiegler Gorge, linauwezo wa kuzalisha umeme mara mbili ya mahitaji ya nchi (2100MW). Kwanini Nchi isielekeze nguvu zote kupata suluhisho la kudumu. Ni wakati muafaka wa kuivunja TANESCO na kuanzisha Wakala wa Umeme Tanzania (WAUTA) ambae atasimamia na kuongoza (regulate) nishati ya umeme, na kuacha vyombo kama RUBADA (Rufiji Basin Development Authority) vikizalisha umeme wa uhakika. Hapo Dowans etal itakuwa ni Historia.
Quote

 
Hatuhitaji kukodisha mitambo ya mtu yoyote yule tunachohitaji ni serikali itoe dola 35 milioni kuagiza mitambo miwili kutoka kule kule ambako DOWANS walinunua mitambo yao..........................na hapo tutakuwa na 240MW.......................kila mtambo wa 120MW gharama yake ya kuununua ni dola 15 milioni na gharama nyinginginezo waongezee milioni 5...........kwa mitambo miwili ni 30 milioni dola za marekani.............................

Hatuhitaji kuenbdelea kujidhalilisha kwa mafisadi................labda kama CCM ionatka yaliyowakuta akina Ghadafi. Hosni Mubarak na Ben Ali yawakute hapa..............................ingawaje hata wakilikwepa hili nguvu ya umma bado itawang'oa tu.................................
 
Tunataka umeme uwake


TUMEGUSWA na hali mbaya ya maisha inayoendelea nchini, ambayo inatokana na kupanda bei kwa bidhaa na huduma mbalimbali kila kukicha.
Kupanda kwa bei za vyakula hususan nafaka katika masoko yetu hapa nchini na kupanda kwa bei za nishati ya mafuta, mkaa, gesi na umeme kumeyaweka maisha ya wananchi wengi hususan wa kipato cha chini katika hali ngumu ya maisha.
Hivi karibuni serikali kupitia Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) ilitangaza kuongeza nauli kutoka asilimia 16 ya awali hadi 185, kwa sababu ya kile kilichoelezwa kuwa gharama za uendeshaji zimepanda.
Kupanda huko kwa nauli za daladala na mabasi ya mikoani kutazidi kuyaweka maisha ya Watanzania wengi katika hali ngumu zaidi, kwani vipato vyao ni vidogo sana kuweza kumudu nyongeza hiyo ya nauli huku wakikabiliwa na mahitaji mengine ya msingi katika maisha yao ya kila siku kama chakula, ambavyo navyo vimepanda bei.
Yako wapi yale maisha bora tuliyoahidiwa kwa kasi mpya, nguvu mpya na ari mpya? Iko wapi Tanzania yenye neema tuliyoahidiwa kwa kasi zaidi, nguvu zaidi na ari zaidi? Inasikitisha kwa taifa kubaini kuwa lilidanganywa na serikali iliyoko madarakani.
Ili taifa letu lisiingie kwenye machafuko ya wananchi kupinga ugumu wa maisha uliosababishwa na uongo au uzembe wa serikali, tunatoa rai kwa serikali kwa kushirikiana na Bunge kupitia upya na kwa haraka sera na mipango yake na kutekeleza ufumbuzi wa haraka utakaoshusha gharama za maisha bila kuathiri uchumi wetu.
Tunaitaka serikali kwa mara nyingine kwa kushirikiana na Bunge kuacha siasa na kuhakikisha inalimaliza tatizo la umeme haraka, taifa haliko tayari kusubiri umeme wa uhakika hadi mwaka 2033 kama ilivyotaarifiwa jana kwenye vyombo vya habari.
Tunaandika tukiitaka serikali kuhakikisha umeme wa uhakika unawaka haraka iwezekanavyo kwani taifa halipo tayari tena kupozwa na siasa, hasa katika tatizo ambalo si la dharura, kwani ukubwa wake ulikwisha kujulikana tangu enzi za kuletwa kwa Richmond - tunaamini serikali na vyombo husika vilifanya uzembe katika kulinusuru taifa na kadhia hii.
Tunasema hivyo tukitilia maanani kuwa nchi yetu ina vyanzo vingi asilia; tuna maji ya kutosha, upepo, gesi na hata uranium, vyote hivyo vingeweza kutupatia nishati ya uhakika ya umeme ambao ungeweza si tu kututosha wenyewe lakini pia hata kuwauzia wenzetu, hatuna sababu ya kuendelea kutegemea umeme wa kudunduliza.
Tunaamini pasipo shaka yoyote ile kwamba tumefikishwa hapa na uzembe wa serikali iliyoko madarakani, kwa kushindwa kufanya uwekezaji wa miradi mikubwa ya kuzalisha umeme na badala yake kubakia kutegemea mvua inyeshe katika mabwawa ya Mtera, Kihansi na kwingineko.
Kwamba, mvua isiponyesha mkakati wao siku zote umekuwa ni kutumia mabilioni ya kodi za wananchi kuagiza mitambo ya dharura ili izalishe umeme na kutuliza tatizo ambalo halina hadhi wala sababu za msingi za kuitwa la dharura.
Tunaituhumu serikali kwa uzembe, tukizingatia kumbukumbu zilizopo zinazoonyesha kuwa dharura ya umeme ilijulikana tangu mwaka 2002, tatizo lilijadiliwa tena mwaka 2006, Bunge nalo lilipitisha maazimio mwaka 2008 na mwaka 2009 serikali iliahidi kulimaliza lakini hadi leo hatuna uhakika wa umeme.
Hapa serikali inapaswa kusukumwa, kuwajibika na kuwajibishwa - wanaopaswa kufanya hivyo ni wananchi, tukiwa chombo makini cha habari tunawahamasisha wananchi kuibana serikali kwa njia mbalimbali zilizo halali ili umeme wa haraka na wa uhakika upatikane na walioukwamisha au kuuchelewesha washughulikiwe.
Tunautaka umma wa Watanzania uchukue wajibu huo wa kuisukuma serikali sasa ili iwajibike kwa haraka, kwa kuhakikisha umeme unawaka na miradi ya uhakika ya umeme inaanzishwa haraka ili katika siku za usoni nchi yetu yenye utajiri wa rasilimali isitumbukie tena kwenye fedheha kubwa kama hii.
 
Wanasheria wapinga mkataba mpya na Dowans

Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 16th February 2011 @ 23:56 Imesomwa na watu: 189; Jumla ya maoni: 0








WANASHERIA nchini wameonya kuwa kutaifisha mitambo ya kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Dowans, au kuingia nayo mkataba mpya kwa madai ya kulinusuru Taifa na mgawo wa umeme, ni kujitia kitanzi cha kuilipa kampuni hiyo mabilioni mengine ya fedha.

Wameeleza kuwa endapo mpango wa mkataba mpya utawasilishwa bungeni na kupitishwa ili utekelezwe na Serikali, utalisababishia Taifa hasara kubwa, kwa kuwa Dowans haitaupinga kwa kuwa inafanya biashara na kujali maslahi yake zaidi ya Watanzania.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, kwa masharti ya kutotajwa gazetini, wataalamu hao waliishauri Serikali iwe makini na mapendekezo au ushauri inayopewa na wabunge wake, ili kuepuka ‘mitego' inayoweza kuingia kwa kivuli cha maslahi ya Taifa.

Mtaalamu wa kwanza alihoji uhalali wa Serikali kutumia Sheria ya Uhujumu Uchumi kwa kuuliza kama kampuni hiyo iliwahi kushitakiwa kwa kosa la jinai la kuhujumu uchumi wa Tanzania na kushindwa.

"Ninachofahamu ni kwamba Dowans hawajahujumu uchumi wala kushitakiwa kwa kosa hilo la
jinai, sasa sheria ya kuhujumu uchumi kwa suala lao itaingilia mlango gani?

Unataka kuniambia Serikali itatumia ubabe kuwataifishia mitambo? "Wakati huo sheria itakuwa wapi?

Hamwoni hapo ndipo tutakapoharibu na kudaiwa mabilioni mengi zaidi ya tunayodaiwa sasa na kampuni hiyo? Au ilikwishawahi kuisamehe Tanesco (Shirika la Umeme Tanzania) ili tuseme Serikali ilimalizana nayo?"

Alihoji mtaalamu huyo wa sheria. Mtaalamu mwingine wa masuala ya sheria pia akifafanua kuhusu suala hilo la uhujumu uchumi, alisema wabunge wanapaswa kukumbuka kuwa Dowans ndio walioshinda kesi ya madai iliyoamuliwa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC) kuitaka Tanesco iilipe.

"Sasa haya yatakuwa ni maajabu kwa Serikali kushauriwa kuitaifisha Dowans kwa sababu haijahujumu uchumi.

Na kisheria, anayehujumu uchumi ndiye anayepaswa kuwajibishwa kwa sheria hiyo tena kwa kutaifishiwa mali, sasa labda watwambie kama kuna kilichohujumiwa na kampuni hiyo, halafu tukafichwa, ili tusidhani kuwa Serikali inawekewa mtego," alisema.

Alieleza kuwa kwa mujibu wa sheria, endapo Serikali itakubali kutumia sheria hiyo,
italazimika kuilipa Dowans fidia ya mitambo yake kulingana na bei inayotumika sokoni, ambayo hata hivyo alisema inaweza kuwa mzigo mkubwa tofauti na inavyofikiriwa na wanaotoa ushauri huo.

Mtaalamu huyo wa sheria, alitaja Ibara ya 24(1) na (2) ya Katiba na kuonya kuwa kipengele hicho kikitafsiriwa vibaya au kuchukuliwa kiholela, kinaweza kuleta matokeo mabaya.

"Katiba ya Jamhuri ya Muungano inatamka wazi kwenye ibara niliyoitaja pamoja na ibara zake mbili ndogo kuwa; kila mtu ana haki ya kumiliki mali, na ya kuhifadhi mali aliyonayo kwa mujibu wa sheria.

"Ibara ndogo ya 2 inasema; bila ya kuathiri masharti ya ibara ndogo (1), ni marufuku kwa mtu yeyote kunyang'anywa mali yake kwa madhumuni ya kuitaifisha au mengineyo bila idhini ya sheria ambayo inaweka masharti ya kutoa fidia inayostahili," alisema.

Kuhusu wazo la kuingia mkataba mpya na Dowans wa kuwasha umeme japo kwa miezi mitatu ili kunusuru hali ngumu ya umeme iliyopo nchini kwa sasa, wataalamu hao walisema kushauri hivyo ni kuiingiza Serikali kwenye mtego wenye maslahi ya watu binafsi na wala si ya Taifa.

"Nilisikiliza hotuba ya Rais siku fulani na kumsikia akisema kuwa wataalamu wa sheria watatumika kuona watakavyofanya ili Tanesco isilipe deni hilo.

Rais aliitaka isiharakishe malipo hayo na nadhani alifanya hivyo kiuzalendo. "Sasa hawa wanaotaka Dowans ikodishwe tena na kuzalisha umeme wakati shauri la kwanza bado
halijaisha na Mahakama inayolishughulikia haijatoa uamuzi, wanalitakia mema Taifa hili kweli?

Au wanafanya hivyo bila kujua madhara yake baadaye kwa kampuni inayoidai Serikali?" Alihoji mtaalamu huyo.

Alionya kuwa kitendo hicho kitaipa kampuni hiyo nguvu maradufu za kusimamia uhalali wake na kusisitiza juu ya malipo yake ya awali.

"Nashauri busara itumike katika suala hili, kwa sababu linamgusa kila Mtanzania, mambo yachunguzwe kwa kina na mwenye maslahi yake asipewe nafasi ya kutoa ushauri, sidhani
kama Serikali haina namna nyingine zaidi ya Dowans. Nashauri iepukwe ili kutowachanganya wananchi," alisema.

Vyombo mbalimbali vya habari nchini jana vilimnukuu Mbunge wa Bumbuli na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, January Makamba, akisema kuwa Kamati yake inajadiliana juu ya uwezekano wa kuishauri Serikali iingie mkataba na Dowans wa kuzalisha umeme wa dharura kwa miezi mitatu ili kumaliza tatizo la nishati hiyo.

Pamoja na mambo mengine, alikaririwa akisema itakapobidi, watatumia Sheria ya Kuhujumu Uchumi ili kutaifisha mitambo ya Dowans.
 
Mgawo wa umeme wadaiwa ni hujuma


*Yadaiwa lengo kushawishi kuwasha Dowans
*Bosi wa TANESCO akiri kusikia, akanusha


Na Waandishi Wetu

WAKATI mgawo wa umeme ukizidi kulitikisa taifa habari za hivi
karibuni zimesema kuwa ni hujuma iliyoandaaliwa kitalaamu ili kuweka mazingira ya kununua au kukodi mitambo ya Dowans kwa kisingizio cha kuinusuru nchi.

Tayari hatua hiyo ya kuwasha mitambo ya Dowans imeelezwa kuwa inaweza kuliingiza taifa katika matatizo makubwa.Habari za uchunguzi ambazo limelifikia Majira zimesema kuwa mbali na matatizo ya maji yaliyoanza kujitokeza siku za karibuni, mgawo wa umeme ulianza muda mrefu ukihusishwa na kuharibika kwa mitambo kadhaa ya kufua umeme, jambo ambalo limetajwa na chanzo chetu kuwa ni sehemu ya mkakati huo.

Ingawa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Bw. William Mhando alikanusha kuwapo kwa mpango huo, alikiri kuwapo kwa madai hayo akisema yameshafanyiwa uchunguzi na kubaini kuwa hayana ukweli kwa kuwa mgawo huo hautokani na hujuma.

Mmoja wa wabunge waliozungumza na Majira ambaye hakutaka kutajwa gazetini, amesema anazo taarifa kuwa sh milioni 500 zimetengwa na kuwalipa baadhi mafundi wa shirika la umeme TANESCO kuhujumu mitambo ya shirika hilo ili tatizo la umeme lionekane kubwa na kushawishi umma katika matumizi ya mitambo hiyo.

Mtoa habari wetu alisema kuna kituo kimojawapo jijini Dar es Salaam mafundi wa TANESCO walilazimishwa na bosi wao kuingiza umeme mkubwa zaidi ya uwezo wake, na walipofanya hivyo ukalipuka.

"Wamepewa tip ya milioni 500/-, linapokwisha tatizo hili linajitokeza jingine, lengo ni kushinikiza Watanzania waone kuna tatizo, ili serikali iruhusu mtambo wa Dowans kuzalisha," alisema.

Akifafanua suala hilo, Bw. Mhando alisema madai hayo yalijitokeza kwenye kituo kidogo cha Kipawa ambacho kina uwezo wa kuzalisha kv 132, na ndio umeme ulioingia na si zaidi ya hapo.

"Kama ungeingia umeme unaofikia kv 400 hapo tungesema sawa kuna hujuma," alisema. Bw. Mhando na kufafanua kuwa uchunguzi wa tuhuma hizo ulifanywa na mafundi wa ndani na nje ya nchi.

Taarifa hizo zimejitokeza wakati mitambo ya Dowans imeanza kupigiwa chapuo na baadhi ya wanasiasa akiwamo Mwenyekiti mpya wa Kamati ya Nishati na Madini, Bw. Januari Makamba, kuwa iwashwe kwa mkataba maalumu wa miezi mitatu ili kuinusuru nchi ambayo inaelekea kuwa gizani.

Tayari kauli hiyo ya Bw. Makamba iliyokaririwa juzi kwenye Kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na TBC1, imeelezwa inaweza kuliingiza taifa katika majanga mengine makubwa.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino, Profesa Mwesiga Beregu kauli zilizotolewa na baadhi ya viongozi kutaka mitambo ya Dowans iwashwe ili kunusuru tatizo la umeme nchini ni hatari kwa taifa na zitakuwa hatua za zimamoto ambazo hazitasaidia nchi kuondokana na tatizo.

"Hizi ni hatua za zimamoto. Tunatoka katika janga hilo na tunaingia katika janga jingine bila ya kufikiria. Ni lazima watu watambue kwamba kuna sheria za kimataifa zimetawala kwenye hiyo Dowans, wasikurupuke," alisisitiza.

Alisema kama watu hawatafikiria kwa makini na kisha kulazimisha mitambo hiyo ya Dowans iwashwe, Tanzania itaingia katika matatizo mengine mapya, ambapo alisisitiza kwamba kabla ya maamuzi wafikirie kwanza wasije wakaingiza nchi katika majanga hayo.

Prof. Beregu alisema kuwa tatizo la serikali bado inajikanyaga, haijajiandaa kuweka mikakati ya muda mirefu bali wanayozungumzwa ni zimamoto.

"Tatizo ni kwamba hakuna mikakati madhubuti ya kuzalisha umeme nchini, eneo hili limegubikwa na ufisadi wa namna fulani, ndio maana tumefikia hapa tulipo sasa na ndio maana yote yanayoongelewa ni kama zima moto," alisema.

Alisema kuwa maamuzi Tanzania yamekuwa ya ovyo onyo, hakuna changamoto ya kufikiri na matokeo yake miaka mitano imepita lakini hakuna kitu ambacho Watanzania wanaweza kusherehekea.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), Bi. Ananilea Nkya aliitaka serikali kuwaeleza kwa kina wananchi kwa nini Taifa limefikia hapa lilipo sasa.

Bi. Nkya alisema kuwa tatizo kubwa la viongozi walioko madarakani wamekuwa wakidharau wananchi na ndio maana nchi inakwenda shaghalabaghala.

"Taifa lilipofikia sasa ni hatari serikali ieleze wananchi ni kwa nini imewafikisha katika hali hii ngumu ni kwa nini wanadharau wananchi, wamekaa kimya bila ya kutoa maamuzi yoyote kuhusu umeme wanafikiria nini,"alihoji.

"Wananchi wanahitaji umeme, sasa angalia Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI) limesema viwanda 50 kati ya 280 huenda vikafungwa na vingine kupunguza uzalishaji endapo makali ya mgawo wa umeme yataendelea hadi mwezi ujao, serikali inafikiria nini," alihoji.

Katika kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1, ambacho kilikuwa kikijadili hali ya umeme nchini juzi, Bw. Makamba alisema ni ujinga kuruhusu gridi ya Taifa izimike huku kukiwa na mtambo wa Dowans uliozimwa.

"Hatuwezi kuwa katika dharura huku kuna mtambo umezimwa kwa sababu ya kisiasa...tutumie hata sheria za kuhujumu uchumi mitambo iwashwe

"Wote tutaonekana hatuna akili wakati tukokosa umeme huku kuna mtambo wa Dowans ambao una uwezo wa kuzalisha megawati 120. Uwashwe hata kama ni kwa mkataba wa siku 90," alisema.

Akichangia hoja hiyo, mbunge mmoja wa CCM ambaye hakupenda kutajwa jina lake kutokana na ugumu wa suala hilo anavyoliona alisema anaweza kuzungumzia jambo lingine lolote atakaloulizwa lakini si
kuzungumzia masuala ya umeme na Dowans.

“Unaweza kuzungumza lolote na mimi lakini hili la mitambo ya Dowans naomba nisichangie kwa sababu miongoni mwetu wabunge wa CCM wapo wenye maslahi yao, hivyo unaweza kutoa maoni ukawa katika hali mbaya,� alisema.

Waziri wa zamani wa Ujenzi, Bw. Nalaila Kiula alisema kuwasha mitambo ya Dowans ni kujivuruga wenyewe na kutengeza mazingira ya kuonesha kwamba mkataba ulivyunjwa kimakosa.

Mkataba ulivyunjwa kwa sababu za msingi, serikali ikijiingiza katika kutatua matatizo ya umeme kwa faida ya muda mfupi itakuja kusumbua baadaye ni bora mitambo hiyo isiwashwe.

Alisema mvua ziko karibuni kunyesha, maji yatajaa katika mabwawa yetu umeme utapatikana na pia alirejea hoja la aliyekuwa Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa kuwa kama hilo linaonekana litachelewa ni vyema wakakodi wataalamu wa kutengeza mvua wafanye hivyo ili kujaza mabwawa kwa muda hadi masika.

“Dowans tuna matatizo nao alafu unataka kuwasha mitambo yao, tutakuwa tunafuta makosa na kuonesha tulikosea kuvunja nao mkataba, mambo haya yanaweza yakawa ya kisiasa, tuzingatie maadili tusikubali kutumika,� alisema.

Bw. Kiula alisisitiza kwamba mitambo hiyo isiwashwe kwani TANESCO ndio wanaohusika na masuala ya umeme nchi nzima, bado hawajatoa wazo la kuwasha mitambo hiyo ya watu wenye utata.

Alisisitiza kwamba wazo hilo linawezekana kuwa la kisiasa ili kuwanusuru waliojiingiza na kuleta kampuni hizi ili Dowans ionekane kuwa ni halali kwa kuwa walirithishwa na Kampuni ya Richmond.

Mbunge wa Ukonga (CCM), Bi. Eugen Mwaiposa akizungumzia hilo alisema anaunga mkono hoja ya kuwasha mitambo ya Dowans kwa sababu mahitaji yaliyopo ni kupata umeme.

Alisema kukosekana kwa umeme kunaathiri sana wafanyabiashara ndogondogo hivyo kama kuna uwezekano wa kuwasha hizo mashine ziwashwe ili kuondokana na kiza.

“Sijajua Serikali itaingia gharama kiasi gani katika kuwasha mitambo hiyo lakini naunga mkono iwashwe,� alisema.

Wakati huo huo, Mbunge wa Jimbo la Ubungo (CHADEMA), Bw. John Mnyika amekanusha taarifa zilizomkariri akishauri kampuni ya Dowans ipewe mkataba wa miezi mitatu.

Bw. Mnyika alisema kuwa gazeti moja (sio majira) lilimnukuu vibaya, likidai alitoa kauli hiyo wakati akizungumza katika mahojiano katika Kipindi cha Jambo cha TBC1.

"Napenda watanzania wenzangu wakumbuke kwamba kipindi hicho kilirushwa moja kwa moja, na katika kipindi husika hakuna kauli yoyote niliyoitoa ya kutaka mitambo ya Dowans iwashwe kwa mkataba wa miezi mitatu, badala yake niliitaka serikali itumie sheria hususani ya uhujumu uchumi kuiwasha mitambo husika kwa maslahi ya taifa," alisema.

Sambamba na hilo alisema atatoa tamko la kina hivi karibuni kutokana na nafasi yake ya uwaziri kivuli kuhusu suala la umeme kwa kuzingatia hali ya maisha ilivyo nchini.

Bw. Mnyika alisema kwa mtazamo wake ni muhimu ili kupunguza adha ya mgawo wa umeme, serikali itumie mamlaka yaliyopo kwenye katiba na sheria ikiwemo sheria ya uhujumu uchumi, sheria ya kupambana na rushwa, sheria ya mali zilizopatikana isivyo halali na sheria nyinginezo, itaifishe mitambo hiyo haraka iwezekanavyo na kuiwasha kwa maslahi ya umma.

"Ikumbukwe kwamba kampuni ya Dowans ilirithi mkataba kutoka kampuni ya Richmond ambayo ilithibitishwa kwa maazimio ya bunge kuwa ilipata mkataba katika mazingira ya ukiukwaji wa sheria ikiwemo sheria ya kupambana na rushwa, na pia kampuni hiyo ina utata kuhusu usajili, umiliki na uhamasishaji wa mkataba wake kama suala zima likitazamwa kwa undani wake yakirejewa yaliyojiri Costa Rica na Tanzania," alisema Bw. Mnyika.

Alisema wakati mjadala kuhusu MW 120 za Dowans ukiendelea na kwa kuwa kiasi hicho hakiwezi kuziba pengo la takribani MW 240 ambalo linakabili taifa hivi sasa, ni muhimu kwa Waziri wa Nishati na Madini kutoa maelezo ya kina kuhusu hatua ambayo serikali inataka kuchukua ya kukodi mitambo ya MW 260.

"Waziri atoe ufafanuzi wa kutokukamilika kwa mipango ya serikali wakati ambapo dharura ya umeme ilijulikana tangu mwaka 2002, serikali ikaijadili kwa kina mwaka 2006, bunge likapitisha maazimio mwaka 2008 na serikali ikaahidi tena mwaka 2009 kuweka utaratibu wa kukabiliana na dharura hiyo.

"Katika muktadha huo ni muhimu kwa bunge kupata fursa ya kujadili kwa kina suala la umeme katika mkutano unaoendelea wa bunge kama jambo la dharura ili kuweza kulinusuru taifa," aliongeza.




21 Maoni:


Malkiory Matiya said... Januari Makamba ni mtoto wa Fisadi. Hapa kilichobakia ni kumwondoa joka pangoni kwakwe kama walivyofanya Misri.
February 16, 2011 11:07 PM
the farmer said... Mmeanza kumsuta January na kumpamba Mnyika,waswahili kwa unafiki mmehitimu!Sote tulisikia alichosema Mnyika,hakika aliunga mkono mitambo ya Dowans kuwashwa,kipi kimemfanya leo asahihishe kauli yake?Unafiki tu wa kisiasa!Na huyo Profesa Baregu naye aongee kama msomi,haitoshi tu kusema kuwasha mitambo ya Dowans kutaingiza nchi katika matatizo mengine...YAPI HAYO,kama anayajua si ayaseme?Anataka nani afikiri badala yake?Naye huyu Mama Nkya ajifunze kunyamaza!
February 16, 2011 11:33 PM
Anonymous said... Hilo sipingani nalo huyu na wabunge wake wa ccm hawana jipya kwani DOWANS ni mhasibu wa ccm na baba yake makamba ni katibu mkuu wa ccm. HIVYO ROSTAM NA MAKAMBA CHAI WANAKUNYWA PAMOJA,LUNCH PAMOJA NA VINYWAJI PAMOJA!!!!!!!!!!hatutegemei sikio likakua likazidi kichwa na ndio maana january anatetea tena tumlipe dowans!!1
February 16, 2011 11:45 PM
the farmer said... Someni magazeti yote ya leo na mtakuta wanasheria wakisema hivi:"Ninachofahamu ni kwamba Dowans hawajahujumu uchumi wala kushitakiwa kwa kosa hilo la
jinai, sasa sheria ya kuhujumu uchumi kwa suala lao itaingilia mlango gani?"Mnyika anaelewa sheria sawasawa?I mean,we must seek a legal solution to a legal problem,not a political solution to a legal problem!!!

February 16, 2011 11:52 PM
Anonymous said... Ama kweli sisi wadanganyika ndio tunaoliwa na kama tutaendelea kuwa na mawazo ya kijinga kiasi hiki basi safari yetu kufikia maendeleo na maisha bora kwa kila Mdanganyika itatugharimu miaka kama 1,000 hivi, Mimi nasema ninyi WATAWALA, HAWA WATANZANIA MNAOWAONA KAMA MBUMBUMBU siku zaja ambazo HAMTAONA pa kutokea, na mkumbuke siku itakapotokea FUJO ndani ya nchi yetu ninyi ndio mtakaokuwa wa kwanza kufa, MSIDHANI MTAKUWA SALAMA! ANZENI sasa kujenga usawa ACHENI KUJIGAWIA MALI YETU! kwa Watanzania kukaa kimya msidhani kuwa HAWAMJUI DOWANS NI, MNAJIDANGANYA. NANI
February 17, 2011 12:12 AM
BEN said... HIVI JAMANI, HEBU TUAMBIANE UKWELI, TUACHE USHABIKI, TUULIZANE KWANZA, NI NCHI NGAPI HAPA AFRIKA ZINAZOPITIA HALI HII? NILITAMANI SANA NIJUE NANI MWENZETU KATIKA HILI NA WANAFANYA NINI KUEPUKANA NA JANGA KAMA HILI. NA KAMA HAKUNA WA KUFANANA NAE, KWA NINI SISI? HIVI NCHI ZOTE ZINA MITO NA MABWAWA YA KUTUNZIA MAJI KAMA SISI? WANATUMIA UMEME GANI BASI? MBONA MAMBO KAMA MIPANGO YA KODI TUNAIGA KWA WENGINE, KWA NINI MAZURI PIA TUSIIGE KWAO? HIVI TUTAENDEKEZA SIASA HADI LINI? INACHEKESHA PALE AMBAPO TUNAJIDAI TUNA SERIKALI, HUKU JAMBO MOJA TU KAMA HILI TUNASHINDWA KULIPATIA UFUMBUZI MIONGO KIBAO! NAOMBA NIIASE TU SERIKALI, MIPANGO YA MAENDELEO HAIPANGWI NA KAMATI KUU YA CHAMA, NI KAZI ZA WATAALAMU NA SIO WANASIASA, TUWAACHIE KWA NAFASI NCHI ISONGE MBELE TUONDOKANE NA AIBU HII. SASA TUNAWATAFUTA WAWEKEZAJI WA NINI HUKU UMEME HATUNA, HUU SI UTAKUWA UTAPELI JAMANI? AAH! MUNGU TUSAIDIE WATANZANIA TUIONE NJIA....
February 17, 2011 1:04 AM
Anonymous said... Huyu January Makamba amewekwa hapo kwa maslahi ya kundi fulani.Dowans hatuitaki,afadhali tuendelee na mgawo wa umeme kuliko kurudiana na Dowans.Hivi mke mliyekatiana talaka,na mko kwenye kutathmini madai juu ya haki zake;unawezaje kuimbia mahakama Ha! naomba huyu mke turudiane???? Hawa viongozi wetu wajue wana dhamana ya kuongoza nchi siyo kundi la mafisadi.Naomba viongozi wabadilike.Waache tamaa.Ni bora mtanzania akae giza mwaka mmoja,halafu baadae tujenge vyanzo vyetu.Hizi dharura ni miradi ya mafisadi ambao wana nafasi za juu serikalini.
February 17, 2011 1:15 AM
Anonymous said... Wee unayejifanya ni Farmer hujui dili za viongozi wa nchi hii.Ungejua usingesema hivyo.Hali hii ya kutokuwa na umeme wa kutosha imefanywa na viongozi wa juu kabisa kwa makusudi ya kuleta mikataba ya dharura ili wapate pesa zao hapo.Au kama unajua basi wewe ni rafiki wa mafisadi.
February 17, 2011 1:20 AM
Anonymous said... Kumbe wabunge wengi hakuna kitu kabisa.Sikutegemea kama wataleta wazo la kutumia tena Dowans.Hii inaonyesha Tanzania haina viongozi bali wababaishaji tu.
February 17, 2011 1:25 AM
Anonymous said... Naomba mjue kuwa wapo viongozi wa juu serikalini ambao wanatumia mashirika ya umma kujipatia pesa.Hawana mpango na kumsaidia mtanzania masikini.Viongozi wa haya mashirika wanaendeshwa na walioshika nchi na hivyo kutumia mbinu yoyote ile ili kuchota pesa za walipa kodi.
February 17, 2011 1:29 AM
Anonymous said... Nchi ina wataalamu wa kutosha lakini hawawatumii.Wanaweka watu wao kila sehemu ili wachote vizuri pesa za walipakodi.Kama tungeamua kutumia wataalamu wetu hata watano tu kwenye nishati, Tanzania inaweza kupata umeme wa kutosha kwa miaka 50 ijayo.Lakini kwa sababu za wanasiasa basi hali hii ya kubabaisha katika umeme itaendelea tu hadi watapoondolewa kama Misri na Tunisia.
February 17, 2011 1:34 AM
Anonymous said... KWANI DUNINI MOOOTE KUNA MITAMBO YA DOWANS PEKEE YA KUFUA UMEME???????????

HUU UFISADI UTATUMALIZA.
SIJAWAHI KUONA VIONGOZI WANAJIPANGA KUIHUJUMU NCHI KAMA TANZANIA.

SASA MAKAMBA KUIPIGIA DEBE DOWANS MAANA YAKE NINI?

February 17, 2011 1:36 AM
Anonymous said... Watanzania wezangu hili swala la kuwasha mitambo ya dowans limepangwa mezani na wahusika wanaohitaji hizo 95 bilioni,hivi sasa wanahujumu tanesco ili ionekane kwa sisi wadanganyika kuwa kuna shida kubwa ya umeme,ameandaliwa january makamba, kwanza awe mwenekiti wa kamati ya madini na nishati hilo wakashinda. la pili january kuonyesha sisi wadanganyika jinsi alivyo na uchungu na swala hili ,na hatua za haraka zijukuliwe ambalo kutumia mitambo ya DOWANS...JAMANI'' hivi kweli nchi yetu inaelekea wapi, kundi la watu wachache tu wanalitikisa taifa letu huku tunajua na kuona.wazee wetu, wahasisi wetu wapo kimya yote haya wanayaona lakini hawana huruma tena na kizazi hiki na lijalo,tayari watu hawa washajikamilisha na hivi sasa kilicho baki ni kupigiwa magoti.. wazee wetu iwapo mmetuacha watoto wenu tutapigania haki yetu japokuwa tutakufa wengi lakini msilie kwasababu mmetutenga..MUNGU TUBARIKI IBARIKI NCHI YETU..AMIN
February 17, 2011 1:45 AM
Anonymous said... Wanasiasa wa Tanzania watumieni wataalamu walioko vyuoni. Msijifanye tumewachagua kwa kuwa mna akili sana au mnajua mambo yote ya uchumi, sheria, fedha, na UMEME?

Heshimuni umma mnaowaongoza.

February 17, 2011 1:46 AM
Anonymous said... Janauary makamba ninashuku hiyo nafasi ya uwenyekiti wa Nishati na madini, tunaelewa ulivyo karibu na JK na kwa hivyo upo karibu na Rostam pamoja na Lowassa na kwa hivyo inawezekana utakuwa umewekwa hapo kwa sababu maalum. Mzee wangu Shelukindo ktk jimbo lako ambaye umerithi viatu vyake huko aliko anatikisa kichwa kwa masikitiko, kijana wa jimbo lake unavyotaka kuendeleza na kufanikisha maslahi ya mafisadi. Tuna wasiwasi hata upungufu huu wa umeme kuwa yawezekana ni hujuma kwani mafisadi wana nguvu sana ya kifedha, wanaweza hata kuamuru maji yafunguliwe kwenye mabwawa ili tu ku-create situation mbaya na huku mkianzisha hoja ya kuwasha mitambo ukiwa kijana umewekwa kitini.

Ni maajabu kampuni Dowans inatudai 94Bl za kifisadi then uanze kuipa biashara ya kufua umeme kwa siku 90, watch out young boy, mwanaume hawi hivyo, ni sawa kama mtu akatembea na mkewo na kesi iko mahakamani then kwa shida zako ukakubali akuletee vyakula na nguo kwa watoto wako kisa unashida.

Jambo la kufanya, mkurugenzi wa TANESCO atathimini hali iliyopo kuwa ni ya dharura then afanye utafiti wa kampuni yenye mashine zilizo tayari kuletwa nchini for installation (for renting), aipe zabuni yenyewe peke yake (single sourcing) then mkataba uandaliwe haraka na baada ya muda mfupi tutaweza kupata mtambo unaohitajika kwa muda mfupi. Sheria ya manunuzi ina mruhusu kufanya hivyo ili mradi tu serikali ihakikishe fedha zipo kwa hitaji hilo.

February 17, 2011 2:25 AM
Anonymous said... ndugu zangu tanzania kuna chuo kimoja tu cha muhimbili vingine vyote walivyosoma kina mnyika hakuna kitu hata kwenye vyuo bora 2000 duniani havimo?vyuo vinafundisha watu kuongea sanaaaaaaaaaaa utaalam hakuna poleni sana wabongo
February 17, 2011 2:25 AM
Anonymous said... WALA SIONI AJABU KWANI WATANZANIA TUNAVUNA TULICHOKIPANDA OKTOBA 31, 2010!!!! ULIONA WAPI NCHI IKAONGOZWA NA RAIS ANAYEOGOPA KUZUNGUMZIA MATATIZO! WAKATI WOTE YEYE KIMYA TU UTAFIKIRI TATIZO LA UMEME LIPO NCHI NYINGINE NA YEYE YUPO NCHI NYINGINE! HALI INATISHA NDG ZANGU. AMKENI WATANZANIA, HAKUNA TENA KILICHOBAKI ISIPOKUWA WANASIASA KUWA WAHANDISI NA WAHANDISI KUWA WAKULIMA!!!!!
February 17, 2011 2:37 AM
Anonymous said... Kwani Majira haikuona breaking news ya last night? mabomu kama ya mbgala huko Gongolamboto! Mbon basi kimya hawajafanya coverage yoyote, wao pao na dowans tu! Mtakufa kwa na dowans mwaka huu! ripotini habari moto moto, dowans, dowans, richmond richmond, wenzenu weshachukua caho nyie mnabaki mnapiga kelele!
February 17, 2011 3:32 AM
Anonymous said... Kama Tanesco walizuia mitambo ya watu ya Dowans toka kipindi hicho kwa misingi gani wakati mitambo si yao?

Ina maana basi walipanga kuzalisha umeme wa Dowans toka zamani. Kisha acheni kumshambulia Makamba wa watu wenye Dowans wamo humo humo Tanesco ila kwa kuwa nyinyi mmegubikwa na Rostam, Rostam, Rostam wakati nchi inaliwa na wachaga, kalaghabaho!

Tena wachaga hawa ni wakubwa na wazito, mke wa mmoja wa wakurugenzi wa Dowans ni mchaga, mtoto wa mchaga mmoja maarufu! Lakini wanapeta tu sasa na kubaki kumlaumu Rostam. Rostam kama alihusika na Richmond wakati huo hahusiki na Dowans sasa hivi! Mkurugenzi mmoja wa Dowans aliwahi kuwa mkurugenzi wa uzalishaji hapo hapo Tanesco! Kila kitu kiko hapo hapo Tanesco. Tegueni hicho kitendawili, kinawashinda kutegua kwa kuwa mmeng'ang'ania siko, toeni mji tuwape majibu!

Kalaghabaho,

February 17, 2011 4:40 AM
Anonymous said... hatutaki mitambo ya DOWANS unless imetaifishwa
February 17, 2011 5:51 AM
Anonymous said... MWALIMU KAMBARAGE ALISEMA IKULU SI PANGO LA WALA RUSHWA, WEZI NA MAFISADI, NADHANI HATUKUMWELEWA VIZURI. MIPANGO YA DOWANS IMESUKWA IKULU(MSIFIKIRI NGELEJA YUKO PALE KWA BAHATI MBAYA NA JANUARY KUONGOZA KAMATI HIYO NI BAHATI). NI MPANGO KABAMBE AMBAO ULIANZIA KUMTAFUTA SPIKA WA BUNGE ATAKAYELINDA MAASRAHI YA WEZI, UKAFAULU. ANGALIA SPIKA ANAVYOWAPINGA WANAOTAKA KULETA HOJA ZINAZOPINGANA NA MAASRAHI YA WEZI. HILO HATA MTOTO WA MKULIMA ANALIJUWA. SITAKI KUMZUNGUMZIA KIKWETE, LAKINI MWANAO ANAPOKUWA NI RAFIKI WA MWIZI HUHITAJI MTAALAMU WA KUKWAMBIA TABIA ZA MWANAO. HIVI WEWE DOWANS (ROSTAM, LOWASA..., JK) HAMNA HATA CHEMBE YA UTU? YA MBAGALA NA G'MBOTO NI SALAM KWAKO JK NA GENGE LAKO, WATU WAMECHOKA, AFSA WA JESHI KUJENGA NYUMBA HADI ASTAFU BAADA YA KUPEWA MAFAO YAKE,HUKU WATU WACHACHE WANAISHI MAISHA ZAIDI YA NCHI ZILIZOENDELEA?!
February 17, 2011 11:41 AM

Post a Comment
 
Mgawo wa umeme wadaiwa ni hujuma


*Yadaiwa lengo kushawishi kuwasha Dowans
*Bosi wa TANESCO akiri kusikia, akanusha


Na Waandishi Wetu

WAKATI mgawo wa umeme ukizidi kulitikisa taifa habari za hivi
karibuni zimesema kuwa ni hujuma iliyoandaaliwa kitalaamu ili kuweka mazingira ya kununua au kukodi mitambo ya Dowans kwa kisingizio cha kuinusuru nchi.

Tayari hatua hiyo ya kuwasha mitambo ya Dowans imeelezwa kuwa inaweza kuliingiza taifa katika matatizo makubwa.Habari za uchunguzi ambazo limelifikia Majira zimesema kuwa mbali na matatizo ya maji yaliyoanza kujitokeza siku za karibuni, mgawo wa umeme ulianza muda mrefu ukihusishwa na kuharibika kwa mitambo kadhaa ya kufua umeme, jambo ambalo limetajwa na chanzo chetu kuwa ni sehemu ya mkakati huo.

Ingawa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO, Bw. William Mhando alikanusha kuwapo kwa mpango huo, alikiri kuwapo kwa madai hayo akisema yameshafanyiwa uchunguzi na kubaini kuwa hayana ukweli kwa kuwa mgawo huo hautokani na hujuma.

Mmoja wa wabunge waliozungumza na Majira ambaye hakutaka kutajwa gazetini, amesema anazo taarifa kuwa sh milioni 500 zimetengwa na kuwalipa baadhi mafundi wa shirika la umeme TANESCO kuhujumu mitambo ya shirika hilo ili tatizo la umeme lionekane kubwa na kushawishi umma katika matumizi ya mitambo hiyo.

Mtoa habari wetu alisema kuna kituo kimojawapo jijini Dar es Salaam mafundi wa TANESCO walilazimishwa na bosi wao kuingiza umeme mkubwa zaidi ya uwezo wake, na walipofanya hivyo ukalipuka.

"Wamepewa tip ya milioni 500/-, linapokwisha tatizo hili linajitokeza jingine, lengo ni kushinikiza Watanzania waone kuna tatizo, ili serikali iruhusu mtambo wa Dowans kuzalisha," alisema.

Akifafanua suala hilo, Bw. Mhando alisema madai hayo yalijitokeza kwenye kituo kidogo cha Kipawa ambacho kina uwezo wa kuzalisha kv 132, na ndio umeme ulioingia na si zaidi ya hapo.

"Kama ungeingia umeme unaofikia kv 400 hapo tungesema sawa kuna hujuma," alisema. Bw. Mhando na kufafanua kuwa uchunguzi wa tuhuma hizo ulifanywa na mafundi wa ndani na nje ya nchi.

Taarifa hizo zimejitokeza wakati mitambo ya Dowans imeanza kupigiwa chapuo na baadhi ya wanasiasa akiwamo Mwenyekiti mpya wa Kamati ya Nishati na Madini, Bw. Januari Makamba, kuwa iwashwe kwa mkataba maalumu wa miezi mitatu ili kuinusuru nchi ambayo inaelekea kuwa gizani.

Tayari kauli hiyo ya Bw. Makamba iliyokaririwa juzi kwenye Kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa na TBC1, imeelezwa inaweza kuliingiza taifa katika majanga mengine makubwa.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino, Profesa Mwesiga Beregu kauli zilizotolewa na baadhi ya viongozi kutaka mitambo ya Dowans iwashwe ili kunusuru tatizo la umeme nchini ni hatari kwa taifa na zitakuwa hatua za zimamoto ambazo hazitasaidia nchi kuondokana na tatizo.

"Hizi ni hatua za zimamoto. Tunatoka katika janga hilo na tunaingia katika janga jingine bila ya kufikiria. Ni lazima watu watambue kwamba kuna sheria za kimataifa zimetawala kwenye hiyo Dowans, wasikurupuke," alisisitiza.

Alisema kama watu hawatafikiria kwa makini na kisha kulazimisha mitambo hiyo ya Dowans iwashwe, Tanzania itaingia katika matatizo mengine mapya, ambapo alisisitiza kwamba kabla ya maamuzi wafikirie kwanza wasije wakaingiza nchi katika majanga hayo.

Prof. Beregu alisema kuwa tatizo la serikali bado inajikanyaga, haijajiandaa kuweka mikakati ya muda mirefu bali wanayozungumzwa ni zimamoto.

"Tatizo ni kwamba hakuna mikakati madhubuti ya kuzalisha umeme nchini, eneo hili limegubikwa na ufisadi wa namna fulani, ndio maana tumefikia hapa tulipo sasa na ndio maana yote yanayoongelewa ni kama zima moto," alisema.

Alisema kuwa maamuzi Tanzania yamekuwa ya ovyo onyo, hakuna changamoto ya kufikiri na matokeo yake miaka mitano imepita lakini hakuna kitu ambacho Watanzania wanaweza kusherehekea.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), Bi. Ananilea Nkya aliitaka serikali kuwaeleza kwa kina wananchi kwa nini Taifa limefikia hapa lilipo sasa.

Bi. Nkya alisema kuwa tatizo kubwa la viongozi walioko madarakani wamekuwa wakidharau wananchi na ndio maana nchi inakwenda shaghalabaghala.

"Taifa lilipofikia sasa ni hatari serikali ieleze wananchi ni kwa nini imewafikisha katika hali hii ngumu ni kwa nini wanadharau wananchi, wamekaa kimya bila ya kutoa maamuzi yoyote kuhusu umeme wanafikiria nini,"alihoji.

"Wananchi wanahitaji umeme, sasa angalia Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI) limesema viwanda 50 kati ya 280 huenda vikafungwa na vingine kupunguza uzalishaji endapo makali ya mgawo wa umeme yataendelea hadi mwezi ujao, serikali inafikiria nini," alihoji.

Katika kipindi cha Jambo Tanzania cha TBC1, ambacho kilikuwa kikijadili hali ya umeme nchini juzi, Bw. Makamba alisema ni ujinga kuruhusu gridi ya Taifa izimike huku kukiwa na mtambo wa Dowans uliozimwa.

"Hatuwezi kuwa katika dharura huku kuna mtambo umezimwa kwa sababu ya kisiasa...tutumie hata sheria za kuhujumu uchumi mitambo iwashwe

"Wote tutaonekana hatuna akili wakati tukokosa umeme huku kuna mtambo wa Dowans ambao una uwezo wa kuzalisha megawati 120. Uwashwe hata kama ni kwa mkataba wa siku 90," alisema.

Akichangia hoja hiyo, mbunge mmoja wa CCM ambaye hakupenda kutajwa jina lake kutokana na ugumu wa suala hilo anavyoliona alisema anaweza kuzungumzia jambo lingine lolote atakaloulizwa lakini si
kuzungumzia masuala ya umeme na Dowans.

“Unaweza kuzungumza lolote na mimi lakini hili la mitambo ya Dowans naomba nisichangie kwa sababu miongoni mwetu wabunge wa CCM wapo wenye maslahi yao, hivyo unaweza kutoa maoni ukawa katika hali mbaya,â€� alisema.

Waziri wa zamani wa Ujenzi, Bw. Nalaila Kiula alisema kuwasha mitambo ya Dowans ni kujivuruga wenyewe na kutengeza mazingira ya kuonesha kwamba mkataba ulivyunjwa kimakosa.

Mkataba ulivyunjwa kwa sababu za msingi, serikali ikijiingiza katika kutatua matatizo ya umeme kwa faida ya muda mfupi itakuja kusumbua baadaye ni bora mitambo hiyo isiwashwe.

Alisema mvua ziko karibuni kunyesha, maji yatajaa katika mabwawa yetu umeme utapatikana na pia alirejea hoja la aliyekuwa Waziri Mkuu, Bw. Edward Lowassa kuwa kama hilo linaonekana litachelewa ni vyema wakakodi wataalamu wa kutengeza mvua wafanye hivyo ili kujaza mabwawa kwa muda hadi masika.

“Dowans tuna matatizo nao alafu unataka kuwasha mitambo yao, tutakuwa tunafuta makosa na kuonesha tulikosea kuvunja nao mkataba, mambo haya yanaweza yakawa ya kisiasa, tuzingatie maadili tusikubali kutumika,â€� alisema.

Bw. Kiula alisisitiza kwamba mitambo hiyo isiwashwe kwani TANESCO ndio wanaohusika na masuala ya umeme nchi nzima, bado hawajatoa wazo la kuwasha mitambo hiyo ya watu wenye utata.

Alisisitiza kwamba wazo hilo linawezekana kuwa la kisiasa ili kuwanusuru waliojiingiza na kuleta kampuni hizi ili Dowans ionekane kuwa ni halali kwa kuwa walirithishwa na Kampuni ya Richmond.

Mbunge wa Ukonga (CCM), Bi. Eugen Mwaiposa akizungumzia hilo alisema anaunga mkono hoja ya kuwasha mitambo ya Dowans kwa sababu mahitaji yaliyopo ni kupata umeme.

Alisema kukosekana kwa umeme kunaathiri sana wafanyabiashara ndogondogo hivyo kama kuna uwezekano wa kuwasha hizo mashine ziwashwe ili kuondokana na kiza.

“Sijajua Serikali itaingia gharama kiasi gani katika kuwasha mitambo hiyo lakini naunga mkono iwashwe,â€� alisema.

Wakati huo huo, Mbunge wa Jimbo la Ubungo (CHADEMA), Bw. John Mnyika amekanusha taarifa zilizomkariri akishauri kampuni ya Dowans ipewe mkataba wa miezi mitatu.

Bw. Mnyika alisema kuwa gazeti moja (sio majira) lilimnukuu vibaya, likidai alitoa kauli hiyo wakati akizungumza katika mahojiano katika Kipindi cha Jambo cha TBC1.

"Napenda watanzania wenzangu wakumbuke kwamba kipindi hicho kilirushwa moja kwa moja, na katika kipindi husika hakuna kauli yoyote niliyoitoa ya kutaka mitambo ya Dowans iwashwe kwa mkataba wa miezi mitatu, badala yake niliitaka serikali itumie sheria hususani ya uhujumu uchumi kuiwasha mitambo husika kwa maslahi ya taifa," alisema.

Sambamba na hilo alisema atatoa tamko la kina hivi karibuni kutokana na nafasi yake ya uwaziri kivuli kuhusu suala la umeme kwa kuzingatia hali ya maisha ilivyo nchini.

Bw. Mnyika alisema kwa mtazamo wake ni muhimu ili kupunguza adha ya mgawo wa umeme, serikali itumie mamlaka yaliyopo kwenye katiba na sheria ikiwemo sheria ya uhujumu uchumi, sheria ya kupambana na rushwa, sheria ya mali zilizopatikana isivyo halali na sheria nyinginezo, itaifishe mitambo hiyo haraka iwezekanavyo na kuiwasha kwa maslahi ya umma.

"Ikumbukwe kwamba kampuni ya Dowans ilirithi mkataba kutoka kampuni ya Richmond ambayo ilithibitishwa kwa maazimio ya bunge kuwa ilipata mkataba katika mazingira ya ukiukwaji wa sheria ikiwemo sheria ya kupambana na rushwa, na pia kampuni hiyo ina utata kuhusu usajili, umiliki na uhamasishaji wa mkataba wake kama suala zima likitazamwa kwa undani wake yakirejewa yaliyojiri Costa Rica na Tanzania," alisema Bw. Mnyika.

Alisema wakati mjadala kuhusu MW 120 za Dowans ukiendelea na kwa kuwa kiasi hicho hakiwezi kuziba pengo la takribani MW 240 ambalo linakabili taifa hivi sasa, ni muhimu kwa Waziri wa Nishati na Madini kutoa maelezo ya kina kuhusu hatua ambayo serikali inataka kuchukua ya kukodi mitambo ya MW 260.

"Waziri atoe ufafanuzi wa kutokukamilika kwa mipango ya serikali wakati ambapo dharura ya umeme ilijulikana tangu mwaka 2002, serikali ikaijadili kwa kina mwaka 2006, bunge likapitisha maazimio mwaka 2008 na serikali ikaahidi tena mwaka 2009 kuweka utaratibu wa kukabiliana na dharura hiyo.

"Katika muktadha huo ni muhimu kwa bunge kupata fursa ya kujadili kwa kina suala la umeme katika mkutano unaoendelea wa bunge kama jambo la dharura ili kuweza kulinusuru taifa," aliongeza.




21 Maoni:


Malkiory Matiya said... Januari Makamba ni mtoto wa Fisadi. Hapa kilichobakia ni kumwondoa joka pangoni kwakwe kama walivyofanya Misri.
February 16, 2011 11:07 PM
the farmer said... Mmeanza kumsuta January na kumpamba Mnyika,waswahili kwa unafiki mmehitimu!Sote tulisikia alichosema Mnyika,hakika aliunga mkono mitambo ya Dowans kuwashwa,kipi kimemfanya leo asahihishe kauli yake?Unafiki tu wa kisiasa!Na huyo Profesa Baregu naye aongee kama msomi,haitoshi tu kusema kuwasha mitambo ya Dowans kutaingiza nchi katika matatizo mengine...YAPI HAYO,kama anayajua si ayaseme?Anataka nani afikiri badala yake?Naye huyu Mama Nkya ajifunze kunyamaza!
February 16, 2011 11:33 PM
Anonymous said... Hilo sipingani nalo huyu na wabunge wake wa ccm hawana jipya kwani DOWANS ni mhasibu wa ccm na baba yake makamba ni katibu mkuu wa ccm. HIVYO ROSTAM NA MAKAMBA CHAI WANAKUNYWA PAMOJA,LUNCH PAMOJA NA VINYWAJI PAMOJA!!!!!!!!!!hatutegemei sikio likakua likazidi kichwa na ndio maana january anatetea tena tumlipe dowans!!1
February 16, 2011 11:45 PM
the farmer said... Someni magazeti yote ya leo na mtakuta wanasheria wakisema hivi:“Ninachofahamu ni kwamba Dowans hawajahujumu uchumi wala kushitakiwa kwa kosa hilo la
jinai, sasa sheria ya kuhujumu uchumi kwa suala lao itaingilia mlango gani?"Mnyika anaelewa sheria sawasawa?I mean,we must seek a legal solution to a legal problem,not a political solution to a legal problem!!!

February 16, 2011 11:52 PM
Anonymous said... Ama kweli sisi wadanganyika ndio tunaoliwa na kama tutaendelea kuwa na mawazo ya kijinga kiasi hiki basi safari yetu kufikia maendeleo na maisha bora kwa kila Mdanganyika itatugharimu miaka kama 1,000 hivi, Mimi nasema ninyi WATAWALA, HAWA WATANZANIA MNAOWAONA KAMA MBUMBUMBU siku zaja ambazo HAMTAONA pa kutokea, na mkumbuke siku itakapotokea FUJO ndani ya nchi yetu ninyi ndio mtakaokuwa wa kwanza kufa, MSIDHANI MTAKUWA SALAMA! ANZENI sasa kujenga usawa ACHENI KUJIGAWIA MALI YETU! kwa Watanzania kukaa kimya msidhani kuwa HAWAMJUI DOWANS NI, MNAJIDANGANYA. NANI
February 17, 2011 12:12 AM
BEN said... HIVI JAMANI, HEBU TUAMBIANE UKWELI, TUACHE USHABIKI, TUULIZANE KWANZA, NI NCHI NGAPI HAPA AFRIKA ZINAZOPITIA HALI HII? NILITAMANI SANA NIJUE NANI MWENZETU KATIKA HILI NA WANAFANYA NINI KUEPUKANA NA JANGA KAMA HILI. NA KAMA HAKUNA WA KUFANANA NAE, KWA NINI SISI? HIVI NCHI ZOTE ZINA MITO NA MABWAWA YA KUTUNZIA MAJI KAMA SISI? WANATUMIA UMEME GANI BASI? MBONA MAMBO KAMA MIPANGO YA KODI TUNAIGA KWA WENGINE, KWA NINI MAZURI PIA TUSIIGE KWAO? HIVI TUTAENDEKEZA SIASA HADI LINI? INACHEKESHA PALE AMBAPO TUNAJIDAI TUNA SERIKALI, HUKU JAMBO MOJA TU KAMA HILI TUNASHINDWA KULIPATIA UFUMBUZI MIONGO KIBAO! NAOMBA NIIASE TU SERIKALI, MIPANGO YA MAENDELEO HAIPANGWI NA KAMATI KUU YA CHAMA, NI KAZI ZA WATAALAMU NA SIO WANASIASA, TUWAACHIE KWA NAFASI NCHI ISONGE MBELE TUONDOKANE NA AIBU HII. SASA TUNAWATAFUTA WAWEKEZAJI WA NINI HUKU UMEME HATUNA, HUU SI UTAKUWA UTAPELI JAMANI? AAH! MUNGU TUSAIDIE WATANZANIA TUIONE NJIA....
February 17, 2011 1:04 AM
Anonymous said... Huyu January Makamba amewekwa hapo kwa maslahi ya kundi fulani.Dowans hatuitaki,afadhali tuendelee na mgawo wa umeme kuliko kurudiana na Dowans.Hivi mke mliyekatiana talaka,na mko kwenye kutathmini madai juu ya haki zake;unawezaje kuimbia mahakama Ha! naomba huyu mke turudiane???? Hawa viongozi wetu wajue wana dhamana ya kuongoza nchi siyo kundi la mafisadi.Naomba viongozi wabadilike.Waache tamaa.Ni bora mtanzania akae giza mwaka mmoja,halafu baadae tujenge vyanzo vyetu.Hizi dharura ni miradi ya mafisadi ambao wana nafasi za juu serikalini.
February 17, 2011 1:15 AM
Anonymous said... Wee unayejifanya ni Farmer hujui dili za viongozi wa nchi hii.Ungejua usingesema hivyo.Hali hii ya kutokuwa na umeme wa kutosha imefanywa na viongozi wa juu kabisa kwa makusudi ya kuleta mikataba ya dharura ili wapate pesa zao hapo.Au kama unajua basi wewe ni rafiki wa mafisadi.
February 17, 2011 1:20 AM
Anonymous said... Kumbe wabunge wengi hakuna kitu kabisa.Sikutegemea kama wataleta wazo la kutumia tena Dowans.Hii inaonyesha Tanzania haina viongozi bali wababaishaji tu.
February 17, 2011 1:25 AM
Anonymous said... Naomba mjue kuwa wapo viongozi wa juu serikalini ambao wanatumia mashirika ya umma kujipatia pesa.Hawana mpango na kumsaidia mtanzania masikini.Viongozi wa haya mashirika wanaendeshwa na walioshika nchi na hivyo kutumia mbinu yoyote ile ili kuchota pesa za walipa kodi.
February 17, 2011 1:29 AM
Anonymous said... Nchi ina wataalamu wa kutosha lakini hawawatumii.Wanaweka watu wao kila sehemu ili wachote vizuri pesa za walipakodi.Kama tungeamua kutumia wataalamu wetu hata watano tu kwenye nishati, Tanzania inaweza kupata umeme wa kutosha kwa miaka 50 ijayo.Lakini kwa sababu za wanasiasa basi hali hii ya kubabaisha katika umeme itaendelea tu hadi watapoondolewa kama Misri na Tunisia.
February 17, 2011 1:34 AM
Anonymous said... KWANI DUNINI MOOOTE KUNA MITAMBO YA DOWANS PEKEE YA KUFUA UMEME???????????

HUU UFISADI UTATUMALIZA.
SIJAWAHI KUONA VIONGOZI WANAJIPANGA KUIHUJUMU NCHI KAMA TANZANIA.

SASA MAKAMBA KUIPIGIA DEBE DOWANS MAANA YAKE NINI?

February 17, 2011 1:36 AM
Anonymous said... Watanzania wezangu hili swala la kuwasha mitambo ya dowans limepangwa mezani na wahusika wanaohitaji hizo 95 bilioni,hivi sasa wanahujumu tanesco ili ionekane kwa sisi wadanganyika kuwa kuna shida kubwa ya umeme,ameandaliwa january makamba, kwanza awe mwenekiti wa kamati ya madini na nishati hilo wakashinda. la pili january kuonyesha sisi wadanganyika jinsi alivyo na uchungu na swala hili ,na hatua za haraka zijukuliwe ambalo kutumia mitambo ya DOWANS...JAMANI'' hivi kweli nchi yetu inaelekea wapi, kundi la watu wachache tu wanalitikisa taifa letu huku tunajua na kuona.wazee wetu, wahasisi wetu wapo kimya yote haya wanayaona lakini hawana huruma tena na kizazi hiki na lijalo,tayari watu hawa washajikamilisha na hivi sasa kilicho baki ni kupigiwa magoti.. wazee wetu iwapo mmetuacha watoto wenu tutapigania haki yetu japokuwa tutakufa wengi lakini msilie kwasababu mmetutenga..MUNGU TUBARIKI IBARIKI NCHI YETU..AMIN
February 17, 2011 1:45 AM
Anonymous said... Wanasiasa wa Tanzania watumieni wataalamu walioko vyuoni. Msijifanye tumewachagua kwa kuwa mna akili sana au mnajua mambo yote ya uchumi, sheria, fedha, na UMEME?

Heshimuni umma mnaowaongoza.

February 17, 2011 1:46 AM
Anonymous said... Janauary makamba ninashuku hiyo nafasi ya uwenyekiti wa Nishati na madini, tunaelewa ulivyo karibu na JK na kwa hivyo upo karibu na Rostam pamoja na Lowassa na kwa hivyo inawezekana utakuwa umewekwa hapo kwa sababu maalum. Mzee wangu Shelukindo ktk jimbo lako ambaye umerithi viatu vyake huko aliko anatikisa kichwa kwa masikitiko, kijana wa jimbo lake unavyotaka kuendeleza na kufanikisha maslahi ya mafisadi. Tuna wasiwasi hata upungufu huu wa umeme kuwa yawezekana ni hujuma kwani mafisadi wana nguvu sana ya kifedha, wanaweza hata kuamuru maji yafunguliwe kwenye mabwawa ili tu ku-create situation mbaya na huku mkianzisha hoja ya kuwasha mitambo ukiwa kijana umewekwa kitini.

Ni maajabu kampuni Dowans inatudai 94Bl za kifisadi then uanze kuipa biashara ya kufua umeme kwa siku 90, watch out young boy, mwanaume hawi hivyo, ni sawa kama mtu akatembea na mkewo na kesi iko mahakamani then kwa shida zako ukakubali akuletee vyakula na nguo kwa watoto wako kisa unashida.

Jambo la kufanya, mkurugenzi wa TANESCO atathimini hali iliyopo kuwa ni ya dharura then afanye utafiti wa kampuni yenye mashine zilizo tayari kuletwa nchini for installation (for renting), aipe zabuni yenyewe peke yake (single sourcing) then mkataba uandaliwe haraka na baada ya muda mfupi tutaweza kupata mtambo unaohitajika kwa muda mfupi. Sheria ya manunuzi ina mruhusu kufanya hivyo ili mradi tu serikali ihakikishe fedha zipo kwa hitaji hilo.

February 17, 2011 2:25 AM
Anonymous said... ndugu zangu tanzania kuna chuo kimoja tu cha muhimbili vingine vyote walivyosoma kina mnyika hakuna kitu hata kwenye vyuo bora 2000 duniani havimo?vyuo vinafundisha watu kuongea sanaaaaaaaaaaa utaalam hakuna poleni sana wabongo
February 17, 2011 2:25 AM
Anonymous said... WALA SIONI AJABU KWANI WATANZANIA TUNAVUNA TULICHOKIPANDA OKTOBA 31, 2010!!!! ULIONA WAPI NCHI IKAONGOZWA NA RAIS ANAYEOGOPA KUZUNGUMZIA MATATIZO! WAKATI WOTE YEYE KIMYA TU UTAFIKIRI TATIZO LA UMEME LIPO NCHI NYINGINE NA YEYE YUPO NCHI NYINGINE! HALI INATISHA NDG ZANGU. AMKENI WATANZANIA, HAKUNA TENA KILICHOBAKI ISIPOKUWA WANASIASA KUWA WAHANDISI NA WAHANDISI KUWA WAKULIMA!!!!!
February 17, 2011 2:37 AM
Anonymous said... Kwani Majira haikuona breaking news ya last night? mabomu kama ya mbgala huko Gongolamboto! Mbon basi kimya hawajafanya coverage yoyote, wao pao na dowans tu! Mtakufa kwa na dowans mwaka huu! ripotini habari moto moto, dowans, dowans, richmond richmond, wenzenu weshachukua caho nyie mnabaki mnapiga kelele!
February 17, 2011 3:32 AM
Anonymous said... Kama Tanesco walizuia mitambo ya watu ya Dowans toka kipindi hicho kwa misingi gani wakati mitambo si yao?

Ina maana basi walipanga kuzalisha umeme wa Dowans toka zamani. Kisha acheni kumshambulia Makamba wa watu wenye Dowans wamo humo humo Tanesco ila kwa kuwa nyinyi mmegubikwa na Rostam, Rostam, Rostam wakati nchi inaliwa na wachaga, kalaghabaho!

Tena wachaga hawa ni wakubwa na wazito, mke wa mmoja wa wakurugenzi wa Dowans ni mchaga, mtoto wa mchaga mmoja maarufu! Lakini wanapeta tu sasa na kubaki kumlaumu Rostam. Rostam kama alihusika na Richmond wakati huo hahusiki na Dowans sasa hivi! Mkurugenzi mmoja wa Dowans aliwahi kuwa mkurugenzi wa uzalishaji hapo hapo Tanesco! Kila kitu kiko hapo hapo Tanesco. Tegueni hicho kitendawili, kinawashinda kutegua kwa kuwa mmeng'ang'ania siko, toeni mji tuwape majibu!

Kalaghabaho,

February 17, 2011 4:40 AM
Anonymous said... hatutaki mitambo ya DOWANS unless imetaifishwa
February 17, 2011 5:51 AM
Anonymous said... MWALIMU KAMBARAGE ALISEMA IKULU SI PANGO LA WALA RUSHWA, WEZI NA MAFISADI, NADHANI HATUKUMWELEWA VIZURI. MIPANGO YA DOWANS IMESUKWA IKULU(MSIFIKIRI NGELEJA YUKO PALE KWA BAHATI MBAYA NA JANUARY KUONGOZA KAMATI HIYO NI BAHATI). NI MPANGO KABAMBE AMBAO ULIANZIA KUMTAFUTA SPIKA WA BUNGE ATAKAYELINDA MAASRAHI YA WEZI, UKAFAULU. ANGALIA SPIKA ANAVYOWAPINGA WANAOTAKA KULETA HOJA ZINAZOPINGANA NA MAASRAHI YA WEZI. HILO HATA MTOTO WA MKULIMA ANALIJUWA. SITAKI KUMZUNGUMZIA KIKWETE, LAKINI MWANAO ANAPOKUWA NI RAFIKI WA MWIZI HUHITAJI MTAALAMU WA KUKWAMBIA TABIA ZA MWANAO. HIVI WEWE DOWANS (ROSTAM, LOWASA..., JK) HAMNA HATA CHEMBE YA UTU? YA MBAGALA NA G'MBOTO NI SALAM KWAKO JK NA GENGE LAKO, WATU WAMECHOKA, AFSA WA JESHI KUJENGA NYUMBA HADI ASTAFU BAADA YA KUPEWA MAFAO YAKE,HUKU WATU WACHACHE WANAISHI MAISHA ZAIDI YA NCHI ZILIZOENDELEA?!
February 17, 2011 11:41 AM

Post a Comment
 

Ngeleja: Serikali haitataifisha Dowans

Imeandikwa na Halima Mlacha, Dodoma; Tarehe: 17th February 2011 @ 23:57

SERIKALI imesema suala la kutaifisha mitambo ya umeme ya Dowans kwa ajili ya 
kukabili hali ya mgawo wa umeme, si sera ya Serikali ya CCM, kwa kuwa hutekeleza kila jambo kwa mujibu wa sheria.
 


Aidha, imewahadharisha viongozi na wanasiasa kuacha kutumia tatizo lililopo la 
umeme kutoa matamko ya kujitafutia sifa na badala yake wazingatie 
zaidi mustakabali wa Taifa.
 


Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, 
alipozungumza na HABARILEO katika mahojiano maalumu kuhusu hali ya umeme nchini.



"Kuhusu kutaifisha mitambo ya Dowans, nasema wazi na nataka ieleweke, hii si 
sera ya Serikali ya CCM, tukiendekeza mambo ya kutaifisha, leo tutataifisha 
Dowans kesho tutakwenda hadi kwenye mali za wananchi," alisema Ngeleja.
 


Alisema Tanzania inaongozwa kwa misingi ya utawala bora ambayo inazingatia 
utawala wa sheria.

"Katika mazingira haya, ili utaifishe mali ya mtu lazima 
upitie mchakato wa kisheria tena kwa kuzingatia sheria za nchi zilizopo."
 


Alisema kwa mgawo wa umeme sasa, kumekuwa na kauli mbalimbali za 
wanasiasa ambazo hazina tija na nyingi zimejaa kujipatia umaarufu, hali ambayo 
haisaidii kutatua tatizo halisi lililopo.


"Ombi langu, tujadili suala hili la upungufu wa umeme na juhudi za utatuzi wake 
kwa kuzingatia misingi tuliyojiwekea, naomba wananchi wapuuze kauli zinazotolewa 
na wanasiasa zenye majibu ya mkato kwa mambo mazito," alisema.


Aliwataka wanasiasa kuacha mara moja kutumia nafasi hiyo ya upungufu wa umeme 
kupotosha Watanzania na ulimwengu kwa kutaka sifa au umaarufu kisiasa. 
 


"Nasisitiza haya nikitambua kwamba katika mazingira yaliyopo ya mgawo wa umeme 
na hasira walizonazo wananchi kutokana na tatizo hilo, ni rahisi kwao kupotoshwa 
na wanasiasa wanaotaka sifa bila kuzingatia mustakabali wa nchi yetu," alisema 
Ngeleja.



Pia Ngeleja aliomba wananchi waunganishe nguvu kupitia viongozi wao wa dini, ili angalau mvua zinyeshe na mabwawa yanayozalisha umeme kwa kutumia maji yajae.
 


Akizungumzia suala la kauli yake aliyoitoa bungeni kuhusu umeme, alikanusha 
taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa hali ya umeme 
itatengemaa mwaka 2033 na kuongeza kuwa huo ni uzushi na kwamba upo mpango 
mkakati wa miradi ya umeme unaoanzia mwaka 2009 hadi 2033.
 


Alisema mpango mkakati huo unajumuisha miradi mingi ya muda mrefu, kati na mfupi, ambayo mingine tayari imekamilika na kutoa umeme akitolea mfano mradi wa umeme wa Ubungo wa megawati 100 na wa Tegeta wa megawati 45.
 


Alisema inasikitisha kuwa wapo baadhi ya watu wanaodhani kuwa Serikali 
haijafanya lolote kuhusu umeme ambapo alisema kama lisingekuwapo 
tatizo la umiliki katika mgodi wa Kiwira wa megawati 200 kuanzia mwaka 2005 
hadi 2010, Serikali ingekuwa na nyongeza ya umeme wa megawati 645.



Ngeleja alitoa kauli hiyo baada ya baadhi ya wabunge kutoa hoja ya kuikodi kwa miezi mitatu au kutaifishwa kwa mitambo ya Dowans ili kumaliza tatizo la umeme akiwamo Mbunge wa Ubungo, John Mnyika na Mbunge wa Bumbuli ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, January Makamba.

Februari 16 pia baadhi ya wanasheria waandamizi nchini walisema mitambo ya Dowans haiwezi kutaifishwa kwa sababu kampuni hiyo haikabiliwi na kesi ya uhujumu uchumi lakini pia kuingia mkataba mwingine na kampuni hiyo ni mzigo kwa Serikali.

 
PHP:

Pia Ngeleja aliomba wananchi waunganishe nguvu kupitia viongozi wao wa dini, ili angalau mvua zinyeshe na mabwawa yanayozalisha umeme kwa kutumia maji yajae.
 


Ukitaka kujua kiongozi kafilisika kisiasa ni huyu Ngeleja anayedai divine intervention for situations God had already empowered us to control and dictate like generation of power..........................................kama Ngeleja angelikuwa ni kiongozi wa kutumainiwa angeliagiza mitambo ya 240 MW kwa not more than 30 million dollars rather oozing out this rubbish.................
 
Siku zote mwizi hakomi kuiacha tabia yake! kila siku huwaza njia na mikakati ya kujipatia ulaji baladhuli! Kama wanataka mitambo kwa nini wasinunue mipya na kuisafirisha ASAP ! Kila siku tukodishe tukodishe hivi mpaka lini hii kukodusha! Hata hao akina makamba hivi wana uzoefu na mambo ya mikataba au mambo ya sheria? Mbona wanakurupuka Kama sungura kichakani na kuongelea vitu
 
Ngeleja hawezi kumlet down GOD FAZA wake RA, kamnyofoa toka Vodacom ( legal officer) akampa Ubunge then Uwaziri - leo hii amsaliti? Never na mkitaka kuhakikisha maneno yangu mnaona jinsi suala na Dowans linavyokuwa treated - yaani ni waziwazi RA anaichanganya serikali na wanasheria wake, jamaa ni mafia kinoma.
 
Huyu tapeli ambaye anajitia ni mmiliki wa DOWANS ni sehemu ya mchoro wa JK na Rostam Aziz kulighilibu taifa ya kuwa hii dili haina utata wowote ule...............................

maelezo ya huyu tapeli yanamtia hatiani kwenye maeneo mawili makubwa.............................

1) yeye adai ndiye mmiliki wa DOWANs lakini katika hati za kesi ya DOWANS versus Richmond jina lake halimo....................................

2) Anadai DOWANS walitumia dola za kimarekani milioni 106 kununua mitambo na baadaye kuongeza milioni 20 (zote dola za kimarekani) wakakti mawakili wa DOWANs walisema mahakamani tena kwa kiapo ya kuwa waligharimia jumla ya dola za kimarekani 7.5 milioni tu kuinunua mitambo hiyo kutoka kwa VULCAN kampuni ambayo nayo ipo marekani....................
 
Dowans yataka mazungumzo na serikali


*Anayetajwa kuimiliki ajitokeza Dar
*Akiri kumpa Rostam nguvu ya kisheria


Na Mwandishi Wetu

MFANYABIASHARA wa Oman anayetajwa kuwa ndiye mmiliki wa Kampuni ya Dowans Holdings SA na Dowans Tanzania Limited, Brigedia Jenerali
(Mstaafu), Sulaiman Mohamed Yahya Al Adawi amejitokeza na kukiri kumiliki kampuni hiyo huku akiweka wazi kuwa iko tayari kwa na mazungumzo na serikali.

Al Adawi aliyezungumza na baadhi ya wahariri wa magazeti jijini Dar es Salaam kwa sharti la kutopigwa picha wala kurekodiwa na kamera za televisheni, alisema ameamua kujitokeza kutokana kuondoa kiwingu kilichokuwa kinaizunguka kampuni hiyo hasa kuhusu umiliki wake na akakiri kwamba alimpa Mbunge wa Igunga, Bw. Rostam Aziz nguvu ya kisheria kuisimamia nchini.

"Mimi ndio mwenye hisa nyingi katika kampuni ya Dowans Holdings SA na kampuni yake tanzu ya Dowans Tanzania Limited...Nimekuja nchini kuweka sawa habari za upotoshaji kuhusu Dowans na kufahamu kama uwezekano wa kupata suluhisho la hali iliyopo," alisema.

Mfanyabiashara huyo aliambatana Bw. John Miles, aliyetambulishwa kama mwanasheria maarufu wa kimataifa ambaye amekuwa akiiwakilisha kampuni hiyo tangu ilipoingia katika mgogoro na Shirika la Umeme nchini (TANESCO) na Bw. Stanly Munai aliyetajwa kama Mkurugenzi wa Fedha wa Dowans Tanzania Limited, ambaye ni mmoja kati ya wamiliki wa kampuni hiyo waliotajwa na Waziri William Ngeleja Januari mwaka huu.

Mbali na Brigedia Jenerali Al Adawi, wengine waliotajwa ni Andrew James Tice kutoka Canada, Gopalakrishnam Balachandran wa India, Hon Sung Woo wa Malaysia, Guy Arthur Picard kutoka nchini Canada pamoja na Stanley Munai wa nchini Kenya.

Brigedia Jenerali Al Adawi alisema tangu kampuni hiyo ilipoanzishwa mwaka 2005 alikuwa amenuia kuwekeza katika mkongo wa mawasiliano katika nchi za Afrika Mashariki, lakini kwa kuwa yeye anaishi Muscat, Oman, alihitaji mtu wa kumwakilisha kufanikisha mpango wake, ndipo alipomchagua rafiki wake wa siku nyingi Bw. Rostam Aziz.

"Ili Bw. Aziz awe na mamlaka ya kutosha kusimamia kampuni yangu, mwaka huo wa 2005 nilimpa nguvu ya kisheria," alisema na kufafanua kuwa mpango huo ulibadilika baada ya kutokea mpango mpya wa mitambo ya kuzalisha umeme mwaka uliofuata.

Alisema Baada ya kampuni ya Richmond kushindwa kuzalisha umeme, Septemba 2006, Bw. Aziz aliwasiliana naye akimwelezea tatizo la umeme akimshawishi awekeze kwenye umeme, akiamini kuwa mwekezaji anayetakiwa ni mwenye uwezo na anayeweza kufanya shughuli hiyo haraka.

"Mtakumbuka kuwa TANESCO iliomba kupitia kwenye vyombo vya habari mwekezaji mwenye uwezo wa kuzalisha kuanzia megawati 1 kuwasiliana nayo kuzalisha umeme wa dharura. Gridi ya taifa ilikuwa inaishiwa umeme kabisa.

"Hatimaye, Dowans ilifikia makubaliano na Richmond, kuwa kama TANESCO ingekubali kampuni yake ingechukua nafasi ya Richmond kuchukua mkataba wa kuzalisha umeme. Tuliamini kuwa Dowans ingepokewa vizuri na TANESCO, serikali na umma kama shujaa, kinachotushangaza haikuwa hivyo.

Alisema Dowans ililipa dola za Marekani milioni 109 (kwa ajili ya mitambo, vifaa vyake na wahandisi na baadaye kuongeza mtaji wa dola milioni 20.

Al Adawi alisema kuwa watu wasiokuwa taarifa sahihi wamekuwa wakiishutumu kampuni yake wakiita ya mfukoni, lakini yeye anawapa changamoto waoneshe kampuni nyingine ya mfukoni yenye mitambo ya dola za Marekani milioni 109.

Mfanyabiashara huyo alionekana kama anajibu hoja mbalimbali zilizokuwa zikimtaja Bw. Aziz kuwa mtu mwenye mamlaka na Dowans, alisema wakati anaweka sawa kampuni yake nchini, alimwomba mbunge huyo ambaye ni rafiki yake amsaidie, pia aliwatumia wafanyakazi wa kampuni ya mbunge huyo, Caspian limited, ambao baadaye walikabidhi majukumu kwa wengine walioajiriwa na Dowans limited.

Akijibu maswali ya wahariri, mfanyabiashara huyo alisema kwa sasa ameitwa nchini na serikali kuzungumzia uwezekano wa kutumia mitambo yake kuzalisha umeme kuinusuru nchi na mgawo unaoendelea sasa.

Alipobanwa zaidi ni nani hasa serikali aliyemuita kuzungumza naye, alisema kwa sasa atazungumza na uongozi wa TANESCO kwa kuwa ndiyo inayohitaji umeme, huku akisisitiza kuwa kampuni yake imekuwa ikiuza umeme kwa gharama nafuu ya senti 4.99 kwa uniti moja, jambo ambalo anaweza kufanya hata sasa ikiwa wataelewana.

Kuhusu uwezekano wa kupunguza fidia iliyotolewa kwenye hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kibiashara (ICC), alisema ikiwa serikali itazungumza hilo atakuwa tayari kusaidia kwa nia njema.

Alipoulizwa kwa nini ameamua kujitokeza yeye mwenyewe badala ya Bw. Aziz ambaye alishapewa nguvu ya kisheria, Brigedia Jenereli Al Adawi alisema ni kwa sababu kumekuwa na maneno juu ya mmiliki wa kampuni hiyo, hivyo amejitokeza ili kuonekana.

Alipoulizwa kama anataka kuonekana kwa nini hakutaka kupigwa picha za magazeti wala televisheni, alisema yeye ni mfanyabiashara asiyetaka kufahamika kwa kuwa si vizuri kufanya hivyo kwa mtu kama yeye anayemiliki mali nyingi, akitolea mfano India anakomiliki mitambo ya mabilioni lakini picha yake haijawahi kutokea kwenye magazeti.

Akizungumzia tuzo ya ICC, Al Adawi alisema baada ya hukumu hiyo, Dowans iliwaandikia TANESCO na serikali ili kufanya mazungumzo kutafuta maelewano kwa njia mbalimbali lakini haijajibiwa.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…