Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 23,566
- 24,891
Underdog huwa anaanzia nyumbani ili ajenge confidence. Halafu mambo ya kulalamikia kupangiwa mwarabu si ya kimichezo. Kama timu imeingia kwenye mashindano, haina budi kuwa tayari kucheza na yeyote, sio kulalamika eti upangiwe na fulani. Mwaka 2003 Simba ilianza nyumbani kama underdog, lakini ikawang'oa mashindanoni mabingwa watetezi wa kombe la Klabu Bingwa Afrika, yaani Zamalek, tena kwa wakati ambao ndio walikuwa wametoka kutwaa tena kombe la ligi ya Misri. Jamaa walikuwa wamepanga kufanya sherehe ya ubingwa wa nchi yao baada ya mechi na Simba, lakini wakalazimika kuifuta sherehe kutokana na hali iliyotokea kiwanjani