Dreamliner na Bombardier kuanza kutengeneza faida mwaka 2023: Hii ni kutoka kupata hasara ya bilioni 14 kwa mwaka kabla Magufuli hajalifufua ATCL

Kufufua shirika la ndege ni jambo zuri sana, kununua ndege mpya ni jambo zuri sana, LAKINI USIRI KATIKA MANUNUZI YA NDEGE HIZO, PESA KUTUMIKA BILA IDHINI YA BUNGE NI JAMBO BAYA SANA KULIKO UZURI WAKE.
 
Sasa kwa nn faida ije kuanzia mwaka 2023 ikiwa kila mwezi tunapiga 4.5bil hizo nyingine zinaenda wapi ikiwa ndani ya mwezi tu tunakua tumeshalipa deni tunaodaiwa na chenji ikabaki
 
sijaona mahala hao waliosababisha hyo hasara na deni la mabilioni wakiwajibishwa,au walau hata kuhojiwa.
 
Waswahili wanasema hivi..'CHARITY START AT HOME' anza kwanza kuhoji matumizi ya kopdi zetu hapo UFIPA ndio utoke huku nje
Huko nje ni wapi? Hivi CCM mnajiona fedha za Serikali ya Tanzania ni Mali ya Chama chenu? Kuna mtu amehoji matumizi ya ruzuku ya CCM hapa au amehoji matumizi ya fedha za serikali? Mbona mnajimilikisha Kichama fedha ambazo siyo Mali ya Chama. Tumieni mtakavyo ruzuku yenu na hamtasikia mpinzani yeyote akiwauliza, ila waacheni watanzania waulize matumizi ya fedha yao. Tunajua ruzuku ya vyama inatokana na fedha zetu lakini ndivyo katiba inavyosema mpewe kwa hiyo hata mkinywea chai endeleeni lakini fedha ya serikali inayojadiliwa na kupitishwa na wabunge tuliowachagua kutuwakilisha tutasema tu. Kama kuna matumizi mabaya kwenye vyama ni Kazi ya vyombo husika vinavyolipwa miahahara na posho kwa ajili hiyo kuhoji matumizi. Mkome kabisa kujifanya fedha za serikali ni fedha za Chama chenu, Mkome!
 
Mkuu kwa sababu wanalindwa kwa Mitutu ya Bunduki watatoa sababu nyingine ,iwe tuna kubaliana nao au la.
Watu waliozoea kupika takwimu siyo wa kuamini Mkuu. Akija mwingine na takwimu wanamuuliza uraia!!?
 
Hapa sijaelewa hivi ikiwa tunadaiwa 4.3 na mapato 4.5 kwa mwezi kwa nn faida ije kuanzi 2023 wakati deni ni dogo kuliko mapato?
Hapa hata mimi nitasaidiwa kuelewa, maana hadi kufikia mwaka 2017 deni lilipungua hadi kufika 4.3b , na kwa mwaka kwa sasa wanaingiza 4.5b. Je, mbona kama inachukua muda hivyo kuanza hupata faida?

Au deni harisi ni kiasi gani kwa mwezi?
 
2023 sio mbali. Hata ya makinikia yalianza hivi hivi. Wanajua 2023 mtakuwa mmeshasahau.....
 
I CAN BET WITH YOU , THIS PLANE WILL BE GROUNDED SOON, IT WILL NEVER CROSS THE BORDER OF OUR COUNTRY
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…