Dreamliner yaanza safari kwa kishindo: Tiketi za Mwanza na KLM tayari zimeisha mpaka tarehe 18 Agosti 2018

TRA watakapokuwa wabakufata ofisini kwako pia usiwakimbie mpe Hongera Rais Magufuli, maana hilo dude linaingiza hasara, na ili kufidia itabid mwananch wa chini Aumie,

Kwahiyo sitarajii kuona Ukileta uzi humu kuwa TRA inakubana na kodi zimeongezeka
Linaingizaje hasara kabla halijaanza kazi
 
mie mwenyewe hilo dude nalitamani kinoma, bahati mbaya sipo kwenye hz ruti.
 
Mkuu watanzania ndivyo tulivyo... mimi. natamani bei ziwe affordable na endelevu na si kukomoana... wote tufurahie mema ya nchi!!
 
Watanzania hao3000 watapanda air Tanzania tu?wengi wanaenda nje Kwanza sio traveling within elewa Hilo alaf hili soko huria sio ujamaa
kwani ATCL wanazo ndege za kubeba watu 3000 kwa siku? hata hizo ndege za watu binafsi bado zinapata wateja na kuna watu wanaziamini zaidi. si kweli watu hawatumii au hawapendi kutumia ndege safari za ndani la bei zipo juu na wakati mwingine bila sababu hivyo wacha ndege ziwe nyingi zinaweza kusaidia watu kutumia ndege zaidi na wakati mwingine bado watanzania hawajajengwa kisaikolojia mara nyingi tunawajenga watu kujikataa kuliko kujikubali kitu ambacho si sahihi sana.
 
Pia, eleweni tu Bombardier zilizokuwa zinatumia hiyo route sasa zinakosa abiria na ni hasara kuzipaki kwa huo mwezi mzima.

Akili mbovu sana hizi. Hivi unafikira kuwa ndege zote za atcl kwa siku moja huwa zinaelekezwa uelekeo mmoja yaani mwanza au kia? Sio kwamba hizo bombardier zuko programmed ziende mwanza tu. Dreamliner ikienda huko hizo zitaongeza routes za sehemu zingine.
 
Mkuu watanzania ndivyo tulivyo... mimi. natamani bei ziwe affordable na endelevu na si kukomoana... wote tufurahie mema ya nchi!!
mi naimani siku zijazo tutaweza tu kumudu hata jinsi ya kumiliki gari haikuwa kawaida tulivyozoea tukaweza.
mimi naamini jinsi vision na mission zetu ndizo zinazoamua hali yetu. tunaona nini kufanikiwa au kutofanikiwa kama unaona kufanikiwa lazima utafute mission ya kufanikisha tunachoona. kwa mfano unaweza kuamua kaunzia leo kwetu mwanza nitaenda na ndege na itawezekana ambayo unaweza ukapunguza gharama za mafuta kutoka 20,000/- kwa siku na kuwa 15,000/- kwa kupunguza safari zisizo za lazima au kutumia public transport pale pasipo na umuhimu wa kutumia gari ndani ya miezi minne inatosha kupata nauli ya kwenda na kurudi.
elimu inatakiwa zaidi watu uwezo wanao ila wamefundishwa kulia njaa na wewe utakuwa shahidi matajri wengi wasioenda shule maisha yao wengine ni mabovu bila sababu.
 
mbona hamtaji hizo nauli tujuee.. nataka nami chokermbaya nione kama ntaweza kulidandia
 
TRA watakapokuwa wabakufata ofisini kwako pia usiwakimbie mpe Hongera Rais Magufuli, maana hilo dude linaingiza hasara, na ili kufidia itabid mwananch wa chini Aumie,

Kwahiyo sitarajii kuona Ukileta uzi humu kuwa TRA inakubana na kodi zimeongezeka
[emoji16][emoji3]
 

Uwongo mtupu, mbona bado nafasi zipo 19, 20, 21 july 2018...... acheni ushabiki wa kijinga
 
we jamaa ni mwongo sana..... mbona website ya ATCL nimefanya booking nafasi zipo hata tarehe 20 july?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…