Amalinze
JF-Expert Member
- May 6, 2012
- 6,780
- 5,305

Msanii Dudubaya aka Kapafona aka Mapafu ya mbwa ameingia katika Skendo nyingine baada ya kushutumiwa kutaka kuiba simu ya mdau mkubwa wa Twanga pepeta ajulikanae kama Mapao ambae alikuwa amekaa naye meza moja pale Mango Garden huku Twanga Peteta wakiburudisha Tarehe 14 March.
Tukio hilo la fedheha lilitokea usiku wa Jumamosi kwenye ukumbi wa Mango Garden , Kinondoni Jijini Dar es Salaam , ambapo msanii huyo galacha licha ya kuwa mbabe lakini alijikuta akilainika na kuinamisha kichwa chini kutokana na kukutwa na simu ya ‘Pedeshee' Fredito Mopao.
Dudu Baya ambaye alikaribishwa kwenye meza ya Mopao na Mpambe mkubwa wa Mopao anayefahamika kwa jina la John Cena , alikaa hapo huku wote wakifurahia ofa zilizokuwa zikitolewa na Mopao lakini haikufahamika ni muda upi msanii huyo alikwapua simu.
Wakati Mopao alipotaka kuondoka ukumbini hapo ndipo aliposikika aking'aka simu yake aina ya Samsung Note4 iko wapi. Wakaanza kuulizana taratibu katika meza ile lakini hakupata jibu lililoeleweka akaanza kuchachamaa kuidai.
Wakati Mopao ‘akikoroma' ndipo mtu mmoja alimshuku msanii huyo na kusema wamsachi miguuni na ndipo simu hiyo ikakutwa imefichwa kwenye soksi.
Wadau mbalimbali na mashabiki pamoja na Mopao mwenyewe walitaka kumuangushia kichapo lakini wengine wakatumia busara na kumwacha msanii huyo akibaki kaduwaa kwa aibu.
Mkurugenzi Mtendaji wa bendi ya Twanga Pepeta Asha Baraka amesema amesikitishwa sana na kitendo hicho kwani Dudu Baya alipokelewa kwa heshima zote kama msanii.
"Dudu Baya ni msanii mkongwe hivyo hatukutarajia kabisa kama angeweza kufanya kitendo cha fadhaa kama kile, hii yote ni tamaa walizonazo wasanii inasikitisha, nina imani kubwa hata John Cena aliamua kumpeleka katika meza ile maalum ya Mopao kutokana na heshima yake na mchango mkubwa alioutoa katika muziki wa kizazi kipya katika sanaa lakini sasa amejiharibia" alisema Asha.
