Duh! kati ta wahamiaji haramu 1,634 waliokamatwa Msumbiji, 1,561 ni Watanzania

Duh! kati ta wahamiaji haramu 1,634 waliokamatwa Msumbiji, 1,561 ni Watanzania

Maji siku zote hayasahau njia yake hata iwe miaka elfu yatarudia tu njia yake! hofu yangu nikwamba wamsumbiji wamewafukuza wanamsumbiji wenzao! kuna uhusiano mkubwa sana wa kimaisha katika mipaka yetu ya nchi za kiafrika hususani katika lugha,vyakula na tamaduni zao! kuziingilia hizi tamaduni kwa njia neno FUKUZA ni ufinyo wa uelewa kihistoria na impact yake ni kutengeneza UADUI ambao gharama yake ni mbaya mno! mfano leo yakatokea mafuriko au vita vya wenyewe kwa wenyewe nani atampokea wa msumbiji! kungewekwa taratibu nzuri za kutokudhalilishana ili kuhifadhi hadhi ya ujirani mwema! ushauri wangu kwa wote ni huu, Tusiwe wepesi kupandikiza chuki kwani daima itakudhuru na wewe siku moja!

Dah ushauri mzuri, ila pia ungewashauri uhamiaji wa Tanzania pale ulikua una wapakia kwenye malori Wanyarwanda na Warundi waliokua wanaishi na Watanzania kwenye maeneo ya mpakani.
Nilisoma sehemu kwamba mliwafurusha hata hamkuruhusu wapakie mifugo yao, wengine wameishi hapo zaidi ya miaka 40. Kuna taarifa pia kwa jinsi mlikua na mihemko, mliishia kuwafurusha hata Watanzania wenzenu ambao walishindwa kudhihirisha Utanzania wao vizuri, hamkuwa mnawapa muda wa kuweka sawa.
 
Dah ushauri mzuri, ila pia ungewashauri uhamiaji wa Tanzania pale ulikua una wapakia kwenye malori Wanyarwanda na Warundi waliokua wanaishi na Watanzania kwenye maeneo ya mpakani.
Nilisoma sehemu kwamba mliwafurusha hata hamkuruhusu wapakie mifugo yao, wengine wameishi hapo zaidi ya miaka 40. Kuna taarifa pia kwa jinsi mlikua na mihemko, mliishia kuwafurusha hata Watanzania wenzenu ambao walishindwa kudhihirisha Utanzania wao vizuri, hamkuwa mnawapa muda wa kuweka sawa.
Labda nikusahihishe kidogo ndugu! ukifuatilia vyema utaelewa anayefanya mazoezi au utekelezaji huu sio RAIA bali ni vyombo vya dola! hivyo nadhani haipendezi kutumia sentensi za majumuisho utakuwa hutendi haki! kwa 100% raia kwa raia wa pande mbili za nchi jirani ndio hutengeneza joto la upendo na kukaribishana ila anayehoji uhusiano huo ni serikali,kwanini huoji? bila shaka ni kwa misingi ya katiba zao! si ilaumu Tanzania kwa jinsi ilivyo nyumbani kwa kila aliyepakana nasi,ila kilichotokea kama ulivyo andika nadhani kulikuwepo na kukithiri kwa wakaazi au wahamiaji au ndugu zetu walio tumia fursa hiyo ya UPOLE wa tanzania kuanzisha vitendo vya ujambazi na uporaji nk! Msumbiji wamefanya ya kwao,ila sisi hatujambugudhi hata mmoja wao! hili ni somo pia! Sio kwamba hawapo!
 
Hatimaye Msumbiji wametoa taarifa rasmi kuhusu vituko vya hivi majuzi ambapo wageni walifurushwa na kupokea kichapo na kunyang'anywa mali. Polisi wa Msumbiji wamesema shughuli yenyewe imerasimishwa na ipo kwa ajili ya kuwasaka wahamiaji haramu wanaochuma kule migodini.

Takwimu zinaonyesha kwamba Watanzania 1,561 ni miongoni mwa hao wahamiaji 1,634 waliokamatwa. Wengine 73 wametokea kwenye nchi tofauti kama vile Gambia, Senegal, Thailand and Mali

================================================
Mozambican authorities have arrested 3,220 people suspected of involvement in illegal mining in Cabo Delgado Province, local media said.

According to DW Radio, 1,634 of those arrested were foreign nationals.

DW Radio quoted the Cabo Delgado Province police boss, Mr Abdul Chaguro, saying “1,561 were Tanzanian nationals. The other 73 people were from Gambia, Senegal, Thailand and Mali”.

“The operation which started on February 9 in Montepuez District, will continue at different points of mineral exploration,” Mr Chaguro was further quoted.

Related stories

Cabo Delgado which is 1,663km north of Maputo, boasts of minerals such as gold, grenadines, aquamarines, tourmalines, blue topaz and green tourmalines.

Cabo Delgado is the northernmost Mozambican province, which borders Tanzania and is divided into 16 districts, with an area of 77,867 km² and a population of 1,893,156.

The province's capital is Pemba with other important cities including Montepuez and Mocimboa da Praia.

Tanzanian authorities reported following the situation.

“The main responsibility of the Tanzanian government through the embassy in Maputo is to make sure the law is respected,” DW Radio quoted the Tanzanian Foreign Affairs Permanent Secretary, Mr Aziz Mlima.

“We will make sure the nationals are safe and the logistics for their return to Tanzania is in order,” Mr Mlima said.

Mozambique nets 1,634 foreign illegal miners
Zipo sheria za uhamiaji.Kama waliingia huko bila kufuata sheria ni sawa kuwafukuza.Watu ni lazima wafuate sheria.
 
Siungi mkono uhamiaji haram, ila najiuliza tu kuhusu hizo takwimu kukosa mmalawi hata mmoja!??
 
Back
Top Bottom