Dully alaumu wasanii ambao hawakuja kumzika baba yake

chibi

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2013
Posts
240
Reaction score
65
Hbr wakuu hivi haya malalamiko ya mr misifa juu ya baadhi ya wasanii kutohudhuria mazishi ya baba yake na kudai kuwa hawamjali na kusisitiza kuwa wengine wanajifanya kumuita brother lakini hawakutokea na kudai kuwa sasa ashajua nani mkweli kwake na nani sio mkweli Je malalamiko yake yana msingi



Source; Amplifaya ya clouds

==========
==========

 
siamini ila km ni kweli,hzo ni tabia za kike ......
 
inaamaana yeye alikuwa makini kiasi hicho hata akafahamu kwamba nani amekuja na nani hakuja?......huo muda aliutoa wapi?
 
Ehh huyu naye so alikuwa haombolezi alikuwa akipepesa macho tu
 
Hayo ya kuitwa brother sijui sisster nchi nyingi za west africa mbona wanaitana my brother my sister hata katika kusalimiana na aimaanishi mtu kakuchukulia kama ndunguye bali kakuheshimu zaidi ya kukuita kidude sijui kinani.

Hawa wasaniii wanadhani kuwa kila mtu aache shughuli aende msibani wakati utakuta ndugu zao wenyewe sio wote walikuwepo msibani. kama mtu kakupa pole na labda hayupo mjini hapo lazima mtu aelewe maana kila mtu ana shughuli zake.

Wangapi wanakuwa marafiki na baadae kuona urafiki haumwendei na wanawakatia watu na inakuwa basi?

inabidi watu wamche Mungu na kuanza kuishi maisha ya kutotegemea wasanii wengine ndio watawaletea umaarufu au kuwapendeshea misiba yao.

nimesoma matusi mengi wasaniii wanatukanwa sababu ya wivu, hapo watu wanaotukana hata kuishi vizuri na majirani zao labda tabu. wakifa wao hata mbwa wa jirani hatahudhuria...

ni kujifunza nani ni nani na kusonga mbele ila sio kutengeneza na kukuza habari eti brother sijui sister sijui najua kwao sijui nini... wamwachie Mungu na kusonga mbele.
 
Mpuuzi kweli,, au alikua kavuta wee.?
 
Nilumsikia dogo anavyolalamika hata mimi aliniboa sana kwa lawama za kitoto kama hizo…ni maisha ya kiswahili tu ndio tatizo…ndio maana unafiki ni mwingi huku uswaz!!mtu msibani anafika kutoa lawama sio ku_feel tatizo!!
 
Duuuh,,!! Ajirekebishe mambo kama hayo ya msiba ya msingi sana kuhudhulia maana leo kwako kesho kwangu,, au yeye yakimfika zari na wema ndio watakao mpa company labda
 
Ww Umeenda Kwny Msiba Kuzika.Au Umeenda Kuchunguza Nani Kafika Na Nani Hajafika.Kama Alimpgia Simu Mfiwa Na Kumtaka Udhuru Ww Unajuaje.Acheni Kuendekeza Majungu Majungu Fanyeni Yenu.Kama Ww Ulifanikiwa Kufika Ongera Yako Kw Kutimiza Wajibu Wako.Lakini Husijione Bora Kuliko Wengine Ambao Hawakupata Nafasi Ya Kuudhurua.Wabongo Ndoman Hatuendelei.Kwsbb Tumekalia Majungu Tu Mpk Misibani
 
Wabongo kwa maneno kwan ni lazima aende kwenye mazishi si ataenda hata kuhan loo na hamumshushi ng'oooooooo
 
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Dully Sykes, ameshangazwa na kitendo cha wasanii wengi kutojitokeza katika mazishi ya baba yake mzazi, Ebby Sykes

"Nilitegemea kwakuwa tunampumzisha baba yangu hapa hapa Dar es Salaam, wangekuja wasanii wengi ambao ni marafiki zangu, lakini hali ilikuwa tofauti kabisa," .

"Sijui walijua nitakuja kuwaomba fedha zao, mimi nilishapata michango mingi kutoka kwa watu wengine mbalimbali, ukweli wasanii tuache roho za kimasikini," alisema.

Sykes aliendelea kusema amegundua asilimia kubwa ya wasanii wamekuwa wakipendana wakati wa raha tu, lakini inapofika muda wa matatizo kila mmoja hukimbia.


Chanzo: EATV
 
Inamaana duly hakuwa ktk hali ya majonzi Alikuwa akiangalia nani kaja na nani hakufika?
Ajifunze kitu sasa hao ndio binadam.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…