Dunia ya kwanza(USA) F shuleni Finaanzia 59 kushuka chini, sisi F inaanzia 29 kushuka chini

Dunia ya kwanza(USA) F shuleni Finaanzia 59 kushuka chini, sisi F inaanzia 29 kushuka chini

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
kwakweli hili suala linafikirisha sana. Marekani high school alama F inaanzia 59 kushuka ambayo huku ni C ya kibabe sana. Huku F inaanzia 29, yaani mtu akipata 30 kafaulu. hata logic inakataa, mtu aliyepata chini ya nusu anakuwaje kapata!!? Nafikiri ubora wa wasomi wetu unaanzia hapa.

gredi 1.jpg
gredi 2.png
gredi 3.jpg
 
Jamaa yetu Benji alitoka huku na “Zero” alienda US akawa kinara


Sasa tujitafakari
Huku alikua anaenda shuleni akiwa hajakula, hivyo asingeweza kuelewa. Tofauti na kule alikua anaenda shuleni kwanza kashakula msosi wa nguvu na shuleni alikua anapata mlo break time
 
Sasa mkuu unataka kweli kufananisha na sisi ambayo hatuna hata madarasa watoto hawana hata chakula n mahitaji muhimu na unataka utufananishe na states? Em Kua serious
Solution ndiyo kushusha grades za ufaulu?
 
Solution ndiyo kushusha grades za ufaulu?
Soln tuanze na mazingira rafiki yamwanafunzi kusoma na hio ikienda sambamba na lishe nzuri Ili watoto wasidumae wakiwa wadogo then tukimaliza yote hayo tutaanza Kuja kwenye grades, na hivo hivo hata kwenye michezo n.k huwezi mchukua fei Toto ukaenda kumfananisha na Phil foden eti utegemee awe Sawa never maandalizi huanzia chini ...
 
Acha kufananisha msuli wa bongo na utopolo wa hao jamaa mkuu, elimu yetu ngumu balaa ni full theory yani unasimuliwa kitu hujawahi hata kukiona na unatakiwa ujibu vile vile ulivyosimuliwa hata kama ulisimuliwa miaka 7 nyuma.

Huko kwao ukijaza jina lako vizuri ni marks, jina la mwalimu wako wa somo ni marks, unapendelea kula nini ni swali na ni marks,

2+2 = ukajibu nimeaahau kidogo itakuwa 5, unapewa nusu marks

Kwa style hiyo hata hiyo 59 kuanzia F wamewapendelea ilibidi ianzie 89
 
Solution ndiyo kushusha grades za ufaulu?
Nafikiri watoto wote wana akili sawa za kuweza kumudu masomo. huyo mto awe wa Kenya, TZ, au Burundi.Ila tuseme mazingira wanayosomea wanafunzi yana influence kubwa na matokeo yaani kuelewa au kutoelewa masomo. Maksi za kushinda nadhani zina utatta kidogo Kwa mfano mimi siafiki na ushindi uliyo chini 50% katika somo.

hapo juu nimesema mazingira ndiyo factor kubwa katika mafanikio. Mimi nina mfano halisi wa binti Mtanzania ambaye shuleni kwake huko vijijini alikuwa alikuwa darasa la nne, hajui kusoma wala kuandika jina lake. Kaka yake naye alikuwa siyo mzuri darasani.
Huyu binti alihamia USA baada ya mama yake kuolewa huko.

Huyu binti aliingia darasa la nne huko USA hajui hata kuandika jina lake. Mhula wa kwanza alikuwa kama zezeta darasani. Huko shuleni alipewa mwalimu special wa kumsaidia hasa Kingereza. Baada ya mwaka huyo binti alianza kujuwa kusoma, kuandika, na hesabu. Alipingia middle school alianza kufanya vizuri, na alihitimu darasa la 8 na A tupu.

Sasa hivi huyu binti yupo shule ya sekondari ya vipaji (darasa la 9). Huyu binti kwa maneno yake anasema kule kijijini shule alikuwa "yupo yupo tu". Alikuwa hajui sababu gani yupo shule. Anasema yeye ameweza kufanya vizuri huko USA kwa sababu "nikikosea naelekezwa na TZ nikosea nachapwa". Anadai walimu walikuwa hawafundishi ila kuwa wakali muda wote. Alipofika USA alikutan walimu wanafundisha na hawachapi, na ukikosea hasa nidhamu taarifa zinaenda nyumbani.

Kwangu mimi huu ni ushahidi kamili kuwa walimu wanatakiwa kutafakari namna ya kufundisha na kuwasaidia watoto kuelewa. Na huenda ni sababu hizihizi huwafanya watoto wa English Medium TZ kufaulu vizuri kwa sababu walimu wamejikita kwenye kuwasaidia watoto kuelewa masomo kuliko kukimbilia fimbo kuwaelimisha watoto, hasa wale wadogo.
 
Nafikiri watoto wote wana akili sawa za kuweza kumudu masomo. huyo mto awe wa Kenya, TZ, au Burundi.Ila tuseme mazingira wanayosomea wanafunzi yana influence kubwa na matokeo yaani kuelewa au kutoelewa masomo. Maksi za kushinda nadhani zina utatta kidogo Kwa mfano mimi siafiki na ushindi uliyo chini 50% katika somo.
hapo juu nimesema mazingira ndiyo factor kubwa katika mafanikio. Mimi nina mfano halisi wa binti Mtanzania ambaye shuleni kwake huko vijijini alikuwa alikuwa darasa la nne, hajui kusoma wala kuandika jina lake. Kaka yake naye alikuwa siyo mzuri darasani.
Huyu binti alihamia USA baada ya mama yake kuolewa huko. Huyu binti aliingia darasa la nne huko USA hajui hata kuandika jina lake. Mhula wa kwanza alikuwa kama zezeta darasani. Huko shuleni alipewa mwalimu special wa kumsaidia hasa Kingereza. Baada ya mwaka huyo binti alianza kujuwa kusoma, kuandika, na hesabu. Alipingia middle school alianza kufanya vizuri, na alihitimu darasa la 8 na A tupu. Sasa hivi huyu binti yupo shule ya sekondari ya vipaji (darasa la 9). Huyu binti kwa maneno yake anasema kule kijijini shule alikuwa "yupo yupo tu". Alikuwa hajui sababu gani yupo shule. Anasema yeye ameweza kufanya vizuri huko USA kwa sababu "nikikosea naelekezwa na TZ nikosea nachapwa". Anadai walimu walikuwa hawafundishi ila kuwa wakali muda wote. Alipofika USA alikutan walimu wanafundisha na hawachapi, na ukikosea hasa nidhamu taarifa zinaenda nyumbani.

Kwangu mimi huu ni ushahidi kamili kuwa walimu wanatakiwa kutafakari namna ya kufundisha na kuwasaidia watoto kuelewa. Na huenda ni sababu hizihizi huwafanya watoto wa English Medium TZ kufaulu vizuri kwa sababu walimu wamejikita kwenye kuwasaidia watoto kuelewa masomo kuliko kukimbilia fimbo kuwaelimisha watoto, hasa wale wadogo.
Hata hapa bongo wapo watu hubadilikia madarasa ya juu. Mtu yupo yupo tu class. Akifika lasita anakuwa smart either wa kupata mwalimu mpya anayefundisha na kutilia mkazo au yeye mwenyewe kujitambua.

NB. Mtoto anatakiwa pia naturally awe smart. Kuna ambao uwezo wao ni ndogo akipelekwa popote
 
Tuwekee na mitihani yao.
Kule kusoma kuelewa
Huku kusoma kumeza maneno.
 
Mfumo WA grading na assessment WA USA ni tofauti na huku tz, tunafuata mfumo WA UK ambayo ni mgumu linapokuja swala la mitihani. Anglia ufanano WA grades UK na us.
IMG_20220218_053317.jpg
 
Kule hata wakiandikiwa F opportunities zipo.

Huku kwetu F automatically psychological torture inaanza. Kwamba umefeli. Unaonekana kilaza tu huna maana utaishia kuwa kibaka tu.

Kule wana accesss na second chances kibao za kutusua maishani bila hata kufaulu kupitia elimu. Kwetu ufaulu wa kimaisha unakuwa judged kupitia shule.

System yetu ina shida mahali.
 
Back
Top Bottom