#COVID19 Dunia yashtuka msimamo wa Hayati Magufuli kuhusu COVID-19


Utter non sense questions ,hujui hata unauliza kitu gani.

Ebu Pitia Survival of the fittest - Only The Strong Will Survive - Halafu Pitia watu waliokuwa kwenye risks ya kupata corona na kuwasumbua kisha uangalie utumbo ulioliza....Inaonekana hata haujui corona ni kitu gani.
 
Ulifanya tafiti gani hadi ukaja na majibu kuwa Tanzania watu walikufa kidogo siyo kama Asia?
 
Kwanini machadema mnapata wivu sana mkiona hayati Magu anasifiwa?
Anaeumia sana ni wewe ambae uliweka moyo wako pamoja na tumaini lako kwa mtu badala ya kuweka moyo wako pamoja na tumaini lako kwenye katiba,sheria na kwenye mifumo imara na thabiti.

Sasa kwa sababu ulifanya ujinga huo ni umepigwa tatu sifuri kwa Magu kufa na sasa hivi upo kama kifaranga asie na mama kwa sababu huna tena pa kuweka moyo wako pamoja na tumaini lako.Hakika amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu-(Yeremia 17:5)
 
amrudishe Ben na Azory kwanza ndio tuendelee na huo upuuzi
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] Acha kuteseka ndugu! Magufuli bado anadunda kupitia kazi zake na sasa amepata mrithi wake ambae ni Samia!

Kubwa kuliko, ccm ndio ipo madarakani! Na bado utaumia sana
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] Acha kuteseka ndugu! Magufuli bado anadunda kupitia kazi zake na sasa amepata mrithi wake ambae ni Samia!

Kubwa kuliko, ccm ndio ipo madarakani! Na bado utaumia sana
Magufuli anadunda kwa kuacha legacy pamoja na kazi zake maarufu zifuatazo:

1.Kuondoka duniani wakati hahitajiki.

2.Kuteka wapinzani wake kama akina Azory Gwanda ili yeye ajihakikishie kutawala milele.

3.Kutesa wapinzani wake kwa kuwaweka ndani kila siku kwa kesi fake ambazo hazina dhamana.

4.Kuua wapinzani wake na wakosoaji wake kama akina Ben saanane na kuwapiga wapinzani wake risasi kama ilivyokuwa kwa Tindu Lissu.

5.Kuua uhuru wa vyombo vya habari.

6.Kuua uhuru wa kujieleza kwa wananchi kama vile kufungia mitandao ya kijamii kama twitter na kukamata wanaotumia mitandao mingine kumkosoa.

7.Kuiba kura kwa kutumia Polisi,jeshi,TISS pamoja na tume ya uchaguzi.

8.Kuua biashara za watu kupitia sera mbovu za uchumi.

9.Kudanganya katika takwimu za ukuaji wa uchumi wa nchi.

10.Kuweka mihimili yote mitatu mfukoni mwake,yaani mhimili wa urais,bunge na mahakama.

11.Kuua uchumi wa nchi kupitia sheria mbovu za uwekezaji.

12.Kuua watu kwa Corona kupitia leadership negligence.

13.Kuhakikisha kuwa akina Ben Saanane na Azory Gwanda walikipata cha mtema kuni.

14.Ukabila kwa kuhamishia rasilimali nyingi za nchi katika wilaya ya Chato na kujaza wasukuma serikalini.

15 Ukanda kwa kupeleka SGR mwanza wakati siyo economic viable zone.

16.Ubaguzi wa rangi kwa kuwakandia wanawake weusi.Imagine mtu anafanya ubaguzi wa rangi karne ya 21!Is this not insane?

17.Kugandamiza demokrasia kwa kukataza vyama vya upinzani kufanya siasa wakati CCM kufanya siasa ni ruksa.

18.Kunyanyasa malaika-watoto wa kike wasirudi shule wakipata mimba.

19.Ufisadi wa kutisha kwa kufanya miradi mikubwa bila budget kupita bungeni.

20.Wizi wa kutisha wa mali ya uma kupitia kampuni yake ya Mayanga constructions LTD.Mfano uwanja wa Chato umetengenezwa na kampuni hii bila tenda kuitwa.

21.Kubambikizia kesi za kuhujumu uchumi wapinzani wake nchi nzima na kuwatupa korokoroni bila dhamana.

22.Kugushi report ya CAG ya hasara za mabilion za ndege za ATCL na kuilazimisha ATCL watoe gawio fake kwa serekali.

23.Kupora utajiri halali na wa jasho wa matajiri wa Tanzania kwa kuwabambikizia kesi fake za kuhujumu uchumi na kuwalazimisha wakiri makosa ya uwongo kisha kuwafilisi mali zao.

24.Ufisadi na wizi wa kutisha kama ulivyoibuliwa na CAG mara baada ya dikteta kufa
 
Hiyo ni kwa mujibu wako wewe na ndio maana ya uhuru wa maoni
 
Kwa maoni yangu, msimamo wake ni vigumu kuu'support' kwa ushahidi wa kisayansi (justification). Yeye kama mwanasayansi alipaswa kuweka wazi utafiti wake ili uchambuliwe na kuona ni jinsi gani alivyoweza kufikia hitimisho (stand). Kwa mfano, ungetokana na utafiti ambao angeufanya na kuuchapisha, labda hapo ndipo mtu angeweza kuu'support' baada ya kuona methodolojia yake na jinsi alivyofikia hitimisho au mapendekezo kwa wanasayansi wengine watakaotaka kufanya urafiti zaidi. Lakini kama mimi ukiniuliza nashindwa kuu'support' kwa sababu sitakuwa na sababu za kisayansi za kuutetea hoja. Kwa maneno mengine, kwenye hesabu ukisema: 'jibu la swali hili ni 4'; mwalimu angetaka aone njia uliyoitumia kupata 4 na bila hiyo njia hawezi kusema umejibu swali lake kikamilifu.
 
Mbona nyengine huzitaji??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…